Ituri: watoto waangamia katika mashambulizi ya makundi ya silaha mkoani Ituri

Ituri: watoto waangamia katika mashambulizi ya makundi ya silaha mkoani Ituri

Tangu disemba 2022, angalau watoto 60 waliuwawa katika vurugu za makundi ya silaha mkoani Ituri kaskazini mashariki mwa jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo. Takwimu hizo zilitolewa na ujumbe wa shirika la umoja wa mataifa kwa ajili ya amani nchini Kongo (MONUSCO) ofisi ya mkoa. HABARI SOS Médias Burundi

Takwimu hizo za kusikitisha zilitolewa wakati wa uzinduzi wa mazungumzo ya jamii ya Hema yanayofanyika eneo la Bunia tangu siku chache zilizopita.

Karna Soro, mkuu wa MONUSCO mkoani Ituri, anaeleza kuwa watoto hao ni kati ya wananchi 310 waliouwawa na vikundi vinavyotajwa kuwa vibaya tangu mwishoni mwa mwaka jana mkoani Ituri.

” Kati ya tarehe mosi disemba 2022 na 21 machi 2023, tumeorodhesha watu 310 waliuwawa wakiwemo watoto 60. Nadhani katika lugha zetu za Afrika, hatuwezi kupata maneno ya kutumia ili kutoa maana ya hali hiyo. Ituri, Kongo ni ikulu yenu ya dhahabu. Licha ya matatizo na changamoto, tuungane. Damu ni nyingi, mateso ni mengi, hali hiyo inatakiwa kusimama”, alibaini.

Baadhi ya mashirika ya kutetea haki za watoto yanaomba ulinzi kwa watoto upewe kipau mbele na viongozi na pia makundi ya silaha.

Previous Ngozi : mfuasi wa chama cha CNL apatikana akiwa maiti
Next Cibitoke : mtu mmoja aliuwawa na mwingine kujeruhiwa katika msitu wa Kibira

You might also like

Usalama

Kayanza: Watu 19 wang’atwa na mbwa waliozurura huko Gahombo, chanjo ya kichaa cha mbwa imeisha

Hali ya kutisha inatikisa wilaya ya Gahombo, katika jimbo la Kayanza kaskazini mwa Burundi. Tangu Februari, wakazi 19 wameng’atwa na mbwa waliozurura, lakini bado hawawezi kupata matibabu ya kutosha kutokana

Criminalité

DRC: Thomas Lubanga atangaza kuundwa kwa “Mkataba wa Mapinduzi Mashuhuri” (CRP)

Thomas Lubanga, mbabe wa zamani wa vita aliyehukumiwa na Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu, alirasimisha kutoka Uganda kuundwa kwa vuguvugu la kisiasa na kijeshi huko Ituri mashariki mwa Jamhuri ya

Haki

Burundi: kundi la waasi la Red-Tabara lashitakiwa kwa uhalifu dhidi ya ubinadamu

Ofisi ya mwendesha mashtaka wa umma ya Jamhuri ya Burundi ilitangaza kuwa imefungua kesi mbili za jinai kwa mashambulizi ya Gatumba (Bujumbura) na Buringa (Bubanza) ambayo yaliua karibu watu thelathini,