Nyarugusu (Tanzania) : misaada yasimamishwa kwa wakimbizi zaidi ya 200 wenye uraia wa Burundi wanaotembea na ulemavu

Nyarugusu (Tanzania) : misaada yasimamishwa kwa wakimbizi zaidi ya 200 wenye uraia wa Burundi wanaotembea na ulemavu

Idadi kubwa ya wakimbizi wenye uraia wa Burundi wanaoishi na ulemavu hawakupata msaada wao wa mkaa. Zaidi ya 200 kati yao hawakuona majina yao kwenye orodha ya wanaohitaji misaada. Wanakosoa ukiukwaji huo mkubwa wa haki zao za msingi. HABARI SOS Médias Burundi

Ni majonzi makubwa kwa wakimbizi wenye uraia wa Burundi wanaoishi na ulemavu, wale wanaosumbuliwa na maradhi yasiopona au wenye umri mkubwa. Sababu : hawako kwenye orodha ya wanaopewa msaada katika miezi ya agosti -septemba.

” Tulihesabu zaidi ya watu 200 ambao hawakupewa mkaa wao wa nishati. Kwa hiyo, jiulize vipi watu wanaotembelea kiti cha kurudumu, wazee wa zaidi ya miaka 70 au wale wanaotembea na virusi vya ukimwi wataweza kupika chakula chao kwa kipindi cha mwezi . Ni hali isiokubalika ” wanalaumu wakuu wa vijiji katika kambi ya Nyarugusu nchini Tanzania.

Watu hao kawaida wanapata msaada kutoka shirika la Danish Refugee Council, DRC. Shirika hilo liliwafahamisha kuwa hawako tena kwenye orodha ya HCR. Ni hatari iliyochukuliwa kinyume na wahusika.

” Ni kawaida HCR hatimaye imeingia katika mpango wa Tanzania wa kutulazimisha kurejea kwa nguvu. Kwanza kabisa, wajumbe wa shirika la DRC walituambia kwa kejeli kuwa tunaweza kwenda kupokea misaada yetu eneo la Mabanda ( nchini Burundi) . Kwa hiyo, sio kosa lililotokea katika data, badala yake, ni mpango uliondaliwa”, wanalaani wakimbizi.

Shirika la DRC lilikubali kuwasilisha tatizo hilo kwa HCR bila ahadi yoyote.

” Kwa nini tusipewe mkaa wakati katika ghala mkaa huo bado unapatikana na badaye wawasilishe tatizo hilo wakati wakifahamu kuwa hatuna chochote, na nguvu za kwenda kutafuta kuuni za kupikia nje ya kambi kama wengine ? Hiyo ni dalili kuwa ni mpango uliondaliwa. Hakika ni ukiukwaji mkubwa wa haki zetu wakati tuko katika kundi la watu ambao wanatakiwa kuwa katika uangalifu mkubwa wa mashirika ya misaada “, wanadai wakimbizi wa uraia wa Burundi wanaotembea na ulemavu.

Kitu na kinyume chake

Hata hivyo, upande wa wakimbizi wenye asili ya Kongo, orodha mpya zinaendelea kuandaliwa na kujumuisha watu wote bila ubaguzi kwa ajili ya kupewa misaada.

Nyarugusu inawapa hifadhi zaidi ya wakimbizi 110.000 wakiwemo zaidi ya elfu 50 wa uraia wa Burundi , wanaosalia wakiwa wakimbizi kutoka Kongo.

Previous Bubanza : shambulio la waasi kwa silaha kutoka DRC katika eneo la Buringa
Next Cibitoke : wafungwa wawili wafariki wakiwa katika gereza la polisi ya mkoa

You might also like

Wakimbizi

DRC: Hatimaye WFP yarejelea ugawaji wa chakula kwa wakimbizi wa Burundi baada ya zaidi ya miezi Kumi ya kimya

SOS Médias Burundi Bukavu, Oktoba 21, 2025 – Baada ya zaidi ya miezi kumi bila msaada wa moja kwa moja wa chakula, Shirika la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) limeanza

Wakimbizi

Musenyi: mahema ya Kupunguza msongamano kwa zaidi ya familia 80 za wakimbizi

SOS Médias Burundi Musenyi, Julai 17, 2025 – Baada ya zaidi ya miezi minne kukaa katika mazingira hatarishi katika handaki za eneo la wakimbizi la Musenyi, lililoko katika eneo la

Wakimbizi

Rwanda/Uganda: upungufu wa maji ya kunywa katika kambi mbili za wakimbizi wa Burundi

Kambi za Mahama nchini Rwanda na Nakivale nchini Uganda zimekumbwa na ukosefu wa maji ya kunywa katika siku za hivi karibuni. Sababu ni tofauti lakini matokeo yake yanatia wasiwasi wakimbizi