DRC (Mulongwe) : wakimbizi wanaotafuta kuuni za kupikia waathiriwa na ubakaji

DRC (Mulongwe) : wakimbizi wanaotafuta kuuni za kupikia waathiriwa na ubakaji

Katika kambi ya wakimbizi wa Mulongwe ndani ya mkoa wa Kivu kusini mashariki mwa jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo, wakimbizi wanakabiliwa na ukosefu wa kuuni za kupikia. Wakimbizi hao hususan akinamama na wasichana wanakwenda hadi katika misitu ya karibu kutafuta kuuni. Kwa mjibu wa vyanzo kutoka viongozi katika jamii, wengi wao wanabakwa na watu wanaobebelea silaha na kunyanganywa simu zao pamoja na vifaa vya kukata kuni. HABARI SOS Médias Burundi

Kulingana na vyanzo ndani ya kambi, akinamama wakimbizi wanakwenda kutafuta kuuni ndani ya misitu ya Kaseke na Katalukulu. Ni katika misitu hiyo ambapo wanawakuta wanaume wanaobebelea silaha kama alivyofahamisha B.Marie mama wa watoto watano.

” Tunatembea kwa takriban kilometa 6 na miguu. Baadhi yetu wanabakwa ndani ya msitu huku wengine wakinyanganywa simu zao”.

Habari hizo zinathibitishwa na Deo Ntakirutimana kiongozi wa wakimbizi wenye uraia wa Burundi ndani ya kambi ya Mulongwe.

Kwa mjibu wake, kuna watu wanaoingia musituni kutafuta kuuni za kupikia lakini wanakuta matatizo hasa ubakaji.

Kutokana na ukosefu wa kuuni za kupikia, baadhi ya wakimbizi wanatumia nyasi ili kupika chakula.

Kambi ya wakimbizi ya Mulongwe inawapa hifadhi zaidi ya wakimbizi kutoka Burundi elfu 10.

Previous Cibitoke : wafungwa wawili wafariki wakiwa katika gereza la polisi ya mkoa
Next Gitega : hakuna sheria miaka 27 baada ya mauwaji ya askofu Joachim Ruhuna

You might also like

Wakimbizi

Nakivale (Uganda): Mkimbizi kukatwa kichwa, kushukiwa kuwa ni uchawi

SOS Médias Burundi Nakivale, Mei 27, 2025 – Tukio la kuogofya lilitikisa kambi ya wakimbizi ya Nakivale kusini magharibi mwa Uganda. Maiti ya mwanamke ambaye hajafahamika jina lake katika hatua

Wakimbizi

Katika kambi ya Nakivale, kiu na magonjwa vinatishia zaidi ya wakimbizi 150,000.

SOS Médias Burundi Nakivale, Agosti 19, 2025 – Mwezi mmoja umepita bila hata tone moja la maji kutoka kwenye mabomba ya umma katika kambi ya Nakivale. Madhara yake ni makubwa

Jamii

Butihinda: Kunyimwa huduma na kutelekezwa katika hospitali ya Gashoho, wakimbizi wa Kongo watelekezwa

SOS Médias Burundi Butihinda, Februari 26, 2026 – Wakimbizi wa Kongo wanaoishi katika kambi ya Kinama katika mkoa wa Buhumuza na kambi ya Musasa katika mkoa wa Butanyerera, mashariki na