DRC (Mulongwe) : wakimbizi wanaotafuta kuuni za kupikia waathiriwa na ubakaji
Katika kambi ya wakimbizi wa Mulongwe ndani ya mkoa wa Kivu kusini mashariki mwa jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo, wakimbizi wanakabiliwa na ukosefu wa kuuni za kupikia. Wakimbizi hao hususan akinamama na wasichana wanakwenda hadi katika misitu ya karibu kutafuta kuuni. Kwa mjibu wa vyanzo kutoka viongozi katika jamii, wengi wao wanabakwa na watu wanaobebelea silaha na kunyanganywa simu zao pamoja na vifaa vya kukata kuni. HABARI SOS Médias Burundi
Kulingana na vyanzo ndani ya kambi, akinamama wakimbizi wanakwenda kutafuta kuuni ndani ya misitu ya Kaseke na Katalukulu. Ni katika misitu hiyo ambapo wanawakuta wanaume wanaobebelea silaha kama alivyofahamisha B.Marie mama wa watoto watano.
” Tunatembea kwa takriban kilometa 6 na miguu. Baadhi yetu wanabakwa ndani ya msitu huku wengine wakinyanganywa simu zao”.
Habari hizo zinathibitishwa na Deo Ntakirutimana kiongozi wa wakimbizi wenye uraia wa Burundi ndani ya kambi ya Mulongwe.
Kwa mjibu wake, kuna watu wanaoingia musituni kutafuta kuuni za kupikia lakini wanakuta matatizo hasa ubakaji.
Kutokana na ukosefu wa kuuni za kupikia, baadhi ya wakimbizi wanatumia nyasi ili kupika chakula.
Kambi ya wakimbizi ya Mulongwe inawapa hifadhi zaidi ya wakimbizi kutoka Burundi elfu 10.
You might also like
Mulongwe: msongamano katika shule zinazowakaribisha watoto wa wakimbizi wa Burundi kutoka kambi ya Mulongwe
Shule zinazowakaribisha watoto wakimbizi wa Burundi huko Mulongwe, katika jimbo la Kivu Kusini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), zinakabiliwa na msongamano wa kutisha. Hali hii inazua wasiwasi
Zambia: “Kufungia kwa kificho” katika kambi, wakimbizi wanakanusha vizuizi vikali vya kusogea
SOS Médias Burundi Meheba, Aprili 15, 2026 – Wizara ya Mambo ya Ndani na Usalama ya Zambia inashutumiwa na wakimbizi kwa kukaza vizuizi vikali na vya kutatanisha vya kuhama katika
Siku ya wakimbizi duniani 2025: Ukimya wa kuziba, Njaa Iliyoenea, na haki zilizokanyagwa
SOS Médias Burundi Nairobi, Juni 19, 2025 – Katika hafla ya Siku ya Wakimbizi Duniani, inayoadhimishwa kila Juni 20, SOS Media Burundi iliangazia hali ya wakimbizi katika nchi nane za
