DRC (Mulongwe) : wakimbizi wanaotafuta kuuni za kupikia waathiriwa na ubakaji

DRC (Mulongwe) : wakimbizi wanaotafuta kuuni za kupikia waathiriwa na ubakaji

Katika kambi ya wakimbizi wa Mulongwe ndani ya mkoa wa Kivu kusini mashariki mwa jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo, wakimbizi wanakabiliwa na ukosefu wa kuuni za kupikia. Wakimbizi hao hususan akinamama na wasichana wanakwenda hadi katika misitu ya karibu kutafuta kuuni. Kwa mjibu wa vyanzo kutoka viongozi katika jamii, wengi wao wanabakwa na watu wanaobebelea silaha na kunyanganywa simu zao pamoja na vifaa vya kukata kuni. HABARI SOS Médias Burundi

Kulingana na vyanzo ndani ya kambi, akinamama wakimbizi wanakwenda kutafuta kuuni ndani ya misitu ya Kaseke na Katalukulu. Ni katika misitu hiyo ambapo wanawakuta wanaume wanaobebelea silaha kama alivyofahamisha B.Marie mama wa watoto watano.

” Tunatembea kwa takriban kilometa 6 na miguu. Baadhi yetu wanabakwa ndani ya msitu huku wengine wakinyanganywa simu zao”.

Habari hizo zinathibitishwa na Deo Ntakirutimana kiongozi wa wakimbizi wenye uraia wa Burundi ndani ya kambi ya Mulongwe.

Kwa mjibu wake, kuna watu wanaoingia musituni kutafuta kuuni za kupikia lakini wanakuta matatizo hasa ubakaji.

Kutokana na ukosefu wa kuuni za kupikia, baadhi ya wakimbizi wanatumia nyasi ili kupika chakula.

Kambi ya wakimbizi ya Mulongwe inawapa hifadhi zaidi ya wakimbizi kutoka Burundi elfu 10.

Previous Cibitoke : wafungwa wawili wafariki wakiwa katika gereza la polisi ya mkoa
Next Gitega : hakuna sheria miaka 27 baada ya mauwaji ya askofu Joachim Ruhuna

You might also like

Wakimbizi

Nyarugusu (Tanzania): wizi wa kutumia silaha

Mfanyabiashara katika Zone 11 alishambuliwa nyumbani kwake na watu wenye silaha ambao bado hawajajulikana. Wakimbizi wawili akiwemo raia wa Burundi walijeruhiwa vibaya. Matukio hayo yalifanyika katika kambi ya wakimbizi ya

Wakimbizi

Nakivale (Uganda): mkimbizi wa Burundi aliyeuawa na mtani wake

SOS Médias Burundi Nakivale, Agosti 26, 2025 – Haki ya kundi la watu inajitokeza tena katika kambi ya wakimbizi ya Nakivale kusini magharibi mwa Uganda. Mkimbizi wa Burundi, anayejulikana kama

Wakimbizi

Kavumu: Watoto wakimbizi wahukumiwa njaa kwa ucheleweshaji wa utawala huko Cankuzo

Kavumu, Mei 19, 2026 – Katika kambi ya wakimbizi ya Kavumu, iliyoko katika tarafa ya Cankuzo katika mkoa wa Buhumuza, mashariki mwa Burundi, familia kadhaa za wakimbizi wa Kongo zinashutumu