Rwanda-DRC : jeshi la Rwanda limeshambulia ndege ya kivita ya Kongo

Rwanda-DRC : jeshi la Rwanda limeshambulia ndege ya kivita ya Kongo

Rwanda inathibitisha kuwa ” imechukuwa hatua za kujilinda na kushambulia ndege ya kivita ya Kongo inayokiuka jumanne hii tarehe 24 januari anga ya Rwanda”. Ni mkasa wa tatu wa aina hiyo uliyoripotiwa na viongozi wa Rwanda tangu novemba 2022. HABARI SOS Médias Burundi

Kwa mjibu wa tangazo la serikali ya Rwanda lililopitishwa kwenye ukurasa wa Twitter, tukio hilo limejiri saa 10:03 alasiri. Serikali ya Rwanda inasema ni uchokozi na kuomba DRC kuachana na aina hiyo ya uvamizi”. Anuani rasmi ya mkoa wa Kivu-kaskazini mashariki mwa Kongo kwenye mpaka na Rwanda, inahakikisha shambulio hilo.

” Ndege haikuguswa, ilijihami kwa kutumia mfumo wake dhidi ya makombora na ni mioto mulioona na moto huo umeteketeza bomu lililorushwa na Rwanda”. imesomeka kwenye anuani hiyo.

Tangu novemba 2022, ni mara ya tatu kwa viongozi wa Rwanda kudai kuwa anga yake imeingiliwa na ndege ya kivita ya Kongo. Kisa cha hivi karibuni ni cha mwishoni mwa disemba.

Tarehe 29 disemba iliyopita, Rwanda ilituhumu jeshi la Kongo kuvamia anga yake, madai yaliyopingwa na viongozi wa Kongo kupitia tangazo.

Uhusiano kati ya mataifa hayo mawili ya maziwa makuu unazidi kuzorota tangu kundi la machi 23, M23 kuanzisha mashambulizi tena.

Kundi hilo la waasi la watutsi lilichukuwa silaha tena mwishoni mwa mwaka wa 2021 likituhumu viongozi wa Kongo kushindwa kutekeleza ahadi zake kuhusu kurejesha wapiganaji wake sehemu kubwa wakiwa watutsi wa Kongo katika maisha ya kawaida.

Viongozi wa Kongo wanaendelea kukubaliana kuwa kundi hilo linaungwa mkono na Rwanda, madai ambayo serikali wa Rwanda inazidi kukanusha na kutupilia mbali.

Rais wa Rwanda Paul Kagame alituhumu mara kwa mara jamii ya kimataifa ” kupendelea viongozi wa Kongo na kusifia amani ya mdomoni” nyakati zilizopita.

Previous Rwanda : zaidi ya wakimbizi wapya 3000 kutoka Kongo wapokelewa
Next Rwanda: more than 3,000 new Congolese refugees received

You might also like

Security

Cibitoke: Rwandan FLN rebels sow fear among the population near Kibira

For two weeks now, residents of the hills near Kibira, Gafumbegeti and Rutorero Butahana zone of Mabayi commune, Cibitoke province, have said they are in panic fear of the Rwandan

Security

Rwanda-DRC : Rwandan forces killed a third Congolese soldier

The Rwandan army announced on Friday evening that it had killed a third Congolese soldier. In a press release, the Rwandan army said that the killed soldier had violated the

Security

Goma (DRC) : more than 400 students heading to Kisangani for military training

At least 400 young university students from Goma in the North Kivu province (eastern DRC) left for Kisangani on Monday for military training. They claim to want to defend the