Rwanda-DRC : jeshi la Rwanda limeshambulia ndege ya kivita ya Kongo
Rwanda inathibitisha kuwa ” imechukuwa hatua za kujilinda na kushambulia ndege ya kivita ya Kongo inayokiuka jumanne hii tarehe 24 januari anga ya Rwanda”. Ni mkasa wa tatu wa aina hiyo uliyoripotiwa na viongozi wa Rwanda tangu novemba 2022. HABARI SOS Médias Burundi
Kwa mjibu wa tangazo la serikali ya Rwanda lililopitishwa kwenye ukurasa wa Twitter, tukio hilo limejiri saa 10:03 alasiri. Serikali ya Rwanda inasema ni uchokozi na kuomba DRC kuachana na aina hiyo ya uvamizi”. Anuani rasmi ya mkoa wa Kivu-kaskazini mashariki mwa Kongo kwenye mpaka na Rwanda, inahakikisha shambulio hilo.
” Ndege haikuguswa, ilijihami kwa kutumia mfumo wake dhidi ya makombora na ni mioto mulioona na moto huo umeteketeza bomu lililorushwa na Rwanda”. imesomeka kwenye anuani hiyo.
Tangu novemba 2022, ni mara ya tatu kwa viongozi wa Rwanda kudai kuwa anga yake imeingiliwa na ndege ya kivita ya Kongo. Kisa cha hivi karibuni ni cha mwishoni mwa disemba.
Tarehe 29 disemba iliyopita, Rwanda ilituhumu jeshi la Kongo kuvamia anga yake, madai yaliyopingwa na viongozi wa Kongo kupitia tangazo.
Uhusiano kati ya mataifa hayo mawili ya maziwa makuu unazidi kuzorota tangu kundi la machi 23, M23 kuanzisha mashambulizi tena.
Kundi hilo la waasi la watutsi lilichukuwa silaha tena mwishoni mwa mwaka wa 2021 likituhumu viongozi wa Kongo kushindwa kutekeleza ahadi zake kuhusu kurejesha wapiganaji wake sehemu kubwa wakiwa watutsi wa Kongo katika maisha ya kawaida.
Viongozi wa Kongo wanaendelea kukubaliana kuwa kundi hilo linaungwa mkono na Rwanda, madai ambayo serikali wa Rwanda inazidi kukanusha na kutupilia mbali.
Rais wa Rwanda Paul Kagame alituhumu mara kwa mara jamii ya kimataifa ” kupendelea viongozi wa Kongo na kusifia amani ya mdomoni” nyakati zilizopita.
About author
You might also like
Bukavu: anti-Rwanda protests have spread
Anti-Rwanda demonstrations spread this Wednesday to the city of Bukavu, capital of the province of South Kivu in eastern Congo. Organizers of the demonstrations are asking Congolese authorities to close
Photo of the week – Bubanza : former MP Fabien Banciryanino sparks controversy
On the occasion of the commemoration of the assassination of President Melchior Ndadaye, former deputy Fabien Banciryanino brought a flower on which is inscribed that the democracy that Ndadaye advocated
Minembwe: mwanajeshi mmoja na mchungaji waliuwawa kwa siku mbili
Mwanajeshi wa FARDC ( jeshi la jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo) aliuwawa jumatano hii asubuhi eneo la Minembwe. Ni katika wilaya ya Fizi mashariki mwa Kongo . Katika eneo hilo,