Burundi : tatizo la uhaba wa mafuta, majibu yake bado kupatikana
Baada ya miezi 18 ya uhaba wa mafuta ya gari, viongozi wa Burundi hawawapi moyo wananchi. Wanachukuwa hatua zisizodumu. Wanaharakati upande wao, wanaomba mkutano mkuu ufanyike kuhusiana na tatizo hilo. HABARI SOS Médias Burundi
Nchini Burundi, linapokuja swala la uhaba wa mafuta ya gari, watu wamekata tamaa wengine wamezoea . Wananchi wanatakiwa kuzowea uhaba wa mafuta ya gari na hasa uongo na majibu ya kukwepa yanayotolewa na viongozi ambao wanazidi kuhakikisha kuwa ” ghala za Burundi zimejaa ” mjini Dar Es Salam ( Tanzania).
Ukweli huo ulikaririwa alhamisi hii na msemaji wa rais Ndayishimiye.
” Kuna waagizaji wa mafuta wasiopenda nchi ambao wanaegesha lori zao nyumbani na kukataa kwenda kuleta mafuta nchini Tanzania. Hawako juu ya sheria na sio watu wasioweza kuguswa. Idara zinazohusika zinawajibika na watu hao watapelekwa mbele ya sheria wakati wowote”, alifahamisha msemaji wa rais Evariste Ndayishimiye, Rosine Guilene Gatoni katika kipindi cha wasemaji wa taasisi za umma kilichofanyika mkoani Muramvya kati kati mwa Burundi.
Kwa mujibu wake, serikali itaangalia uwezekano wa kununua lori zake na kujiandaa kujenga ghala katika ardhi ya Burundi . Na hapa hakuna maelezo yaliyotolewa.
Kwa mujibu wa watalaamu, swala la uhaba wa mafuta ya gari ni ngumu na linaomba kujadiliwa katika mkutano mkuu.
” Ni tatizo linalodumu. Limekuwa na kawaida. Warundi wanatakiwa kuona mafuta hapa, na sio katika ghala mjini Dar Es Salam. Hata Kongo ambayo inakabiliwa na mzozo na ambayo tunasaidia katika maswala ya usalama, haina matatizo ya kuagiza mafuta ya gari”, anasema Faustin Ndikumana, kiongozi wa Parcem , shirika linalopambana kwa ajili ya utawala bora.
Wadadisi wengi wanadai kuwa tatizo la uhaba wa mafuta ya gari husababishwa na uhaba wa pesa ya kigeni, na urasibu mbaya.
You might also like
Burundi: viongozi wanatatizika kusambaza mafuta lakini hawataki tena magari katika vituo vya huduma
Polisi wa Burundi walitangaza Alhamisi kwamba sasa ni marufuku kuegesha gari lako kwenye kituo cha mafuta bila mafuta. Inaibua kuwezesha trafiki barabarani na wasiwasi wa kuhakikisha usalama wa watu na
Buhumuza: Dhahabu ya Cibari yaharibu ardhi, yachochea ufisadi, na mitiririko ya Tanzania
SOS Médias Burundi Muyinga, Oktoba 30, 2025 – Huko Cibari, katika tarafa na ukanda wa Muyinga, mkoa la Buhumuza, wakazi wanaishi katika ndoto mbaya. Mashamba yao yameharibiwa na uchimbaji haramu
Kesi-Bunyoni : sheria nchini Burundi yafunga akaunti za waziri mkuu wa zamani
Benki kuu ya Burundi BRB ( benki ya jamuhuri ya Burundi) ilitoa amri kwa mashirika ya fedha yote ili yasiruhusu kuondoa au kuweka pesa kwenye akaunti za waziri mkuu wa
