Kuhusu-Bunyoni: mahakama kuu imeanza uchunguzi dhidi ya Bunyoni
Korti kuu ya jamuhuri ya Burundi imeamuru kufungua uchunguzi kuhusu kushughulikia kisheria kesi dhidi ya Bunyoni. Mwendeshamashtaka mkuu wa jamuhuri amefahamisha hayo katika tangazo lake jumapili hii. Hata hivyo, tume ya kitaifa ya haki za binadamu haikueleza mahala anapozuiliwa aliyekuwa waziri mkuu mwenye nguvu. HABARI SOS Médias Burundi
Tamko lilolotolewa na mwendeshamashtaka mkuu wa jamuhuri linafahamisha kuwa waziri mkuu wa zamani Alain Guillaume Bunyoni anashikiliwa na polisi ya Burundi.
” Alikamatwa akiwa eneo la Nyamuzi, kijiji cha Mubone tarafani Kabezi katika mkoa wa Bujumbura ( magharibi mwa Burundi ) tarehe 21 aprili 2023″, linasema tangazo lililosainiwa na Sylvestre Nyandwi.
Kwa mjibu wa mwendeshamashtaka mkuu wa jamuhuri, taasisi za Burundi zilianza rasmi kumutafuta Bunyoni tarehe 17 aprili baada ya polisi kutomukuta nyumbani kwake wakati wa msako ulioruhusiwa na ofisi yake.
” Jemedali wa polisi Alain Guillaume Bunyoni kwa sasa yuko mikononi mwa polisi. Matokeo ya msako na ushahidi mwingine utatathminiwa hivi karibuni na kuwekwa mahala pake, kwa kuzingatia utaratibu wa kushughulikia makosa”, tangazo hilo linamalizia.
Kama CNIDH ( tume huru ya kitaifa ya haki za binadamu), mwendeshamashtaka mkuu wa jamuhuri hakufahamisha pia mahala anakozuiliwa waziri mkuu wa zamani.
Lakini vyanzo vya karibu na faili hiyo vimethibitishia SOS Médias Burundi kuwa anazuiliwa katika gereza la SNR ( idara ya kitaifa ya ujasusi) ndani ya jiji la kibiashara la Bujumbura.
” Hajapata haki ya kupewa wakili. Ni kiongozi wa CNIDH aliyekwenda nyumbani kwake kumuletea nguo za kubadilisha”, vyanzo vyetu vinasema.
Alain Guillaume Bunyoni analengwa na vikwazo vya Marekani. Nchi hiyo yenye nguvu duniani inamutuhumu kuhusika na visa vya ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu nchini Burundi.
” Marekani haiwezi kuomba serikali ya Burundi ashughulikiwe na mahakama za kimataifa kwa sababu, marekani ilimuzuia tu kuwasili kwenye ardhi ya marekani”, alitoa tathmini hiyo mwakilishi wa shirika la kiraia aliyetoroka nchi.
Kwa mjibu wa vyanzo vyetu, ” mazungumzo yanaendelea ili adhabu ya Bunyoni iweze kupunguzwa”. Baadhi ya vigogo wa chama madarakani, viongozi tawala, wanajeshi wa vyeo vya juu kutoka kundi la zamani la waasi wa ki hutu la CNDD-FDD wanataka Bunyoni aweze kuadhibiwa vikali ” ili kuepusha mgawanyiko ndani ya chama cha CNDD-FDD”.
You might also like
Bubanza: Eneo wa mkakati la madini lawashusha viongozi wawili ndani ya wiki moja
SOS Médias Burundi Bujumbura, Novemba 16, 2025 – Siku mbili baada ya kufutwa kazi kwa msimamizi wa tarafa ya Bubanza mnamo Oktoba 31, kamishna wa polisi wa mkoa, Épitace Gitamira,
Kivu-kaskazini : watetezi wa haki za binadamu wako hatarini katika maeneo ya migogoro ya silaha
Watetezi wa haki za binadamu katika wilaya ya Rutshuru wanatahadharisha kuhusu vitisho dhidi yao kutoka kwa viongozi wa makundi ya waasi. Wanatoa takwimu za wanaharakati 18 waliouwawa na makundi ya
Bujumbura: Maafisa wawili wa polisi wahukumiwa kulipa faini kwa kumpiga kiongozi wa chama cha siasa
Ilikuwa ni mahakama ya Ntahangwa kaskazini mwa jiji la kibiashara la Bujumbura ambayo iliwahukumu maajenti hao wawili siku ya Jumanne. Gabriel Banzawitonde, rais wa chama cha wahanga wa APDR, anasema
