Rwanda-DRC: DRC imetuhumu kwa mara nyingine Rwanda kusaidia kundi la M23 (tangazo)
Serikali ya Kongo imetuhumu kwa mara nyingine Rwanda kuunga mkono kundi la machi 23, kundi hilo la waasi linalopigana dhidi ya serikali ya jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo, tunasoma hayo katika tangazo la serikali ya Kongo la tarehe 25 oktoba 2022. Viongozi wa Kongo wanamuhusisha pia rais wa Rwanda Paul Kagame. HABARI SOS Médias Burundi
Serikali ya Kongo ilikuwa ikizungumzia tangazo la serikali ya Rwanda la siku moja iliyopita ambalo linatupilia mbali tuhuma za kusaidia kundi la M23.
” Yaliyomo ndani ya tangazo kwa wandishi wa habari yanaonyesha wazi kuwa Rwanda inakubali kuwa inaunga mkono waasi wa M23″ hayo yanasomeka katika tamko lililosainiwa na Patrick Muyaya Katembwe, waziri wa mawasiliano na vyombo vya habari na pia msemaji wa serikali ya Kongo.
DRC inamtuhumu binafsi rais wa Rwanda Paul Kagame na kusema kuwa ana mwenendo unaoonyesha vizuri mkakati wake wa kujiingiza daima katika maswala ya ndani ya DRC” ili kudumisha hali ya usalama mdogo mashariki mwa nchi hiyo kubwa ya afrika ya kati.
Rwanda imetuhumiwa kuvunja ahadi ilizochukuwa mjini Nairobi (Kenya), Luanda (Angola) na New York katika michakato mbali mbali ya kutafuta amani na kutokomeza makundi ya waasi kwenye ardhi ya Kongo likiwemo kundi la M23.
Serikali ya Kongo inatupilia mbali kile inachosema ” Maneno yasiyo ya uadilifu ” ya Rwanda na shughuli zake za kijeshi kwenye ardhi ya Kongo na kukumbusha kuwa ” mipango ya kuingilia na kupanua nchi ya Rwanda kamwe haitavumiliwa”.
Serikali ya Rwanda kwa mara kadhaa imekanusha tuhuma hizo za viongozi wa Kongo.
Katika tangazo lake, Rwanda imekariri ahadi yake ya kutaka suluhu ya usalama na utulivu kupitia jukwa la kikanda licha ya uchokozi wa FARDC ( jeshi la jumuhuri ya kidemokrasia ya Kongo)
Hadi wakati huu, kundi la M23 linadhibiti mji wa mpakani wa Bunagana tangu tarehe 13 juni mwaka huu pamoja na maeneo mengi ya wilaya ya Rutshuru katika mkoa wa kivu ya kaskazini mashariki mwa Kongo.
You might also like
Cultural dancers under pressure : “Banned from performing for other parties, underpaid by the CNDD-FDD”
SOS Médias Burundi Makamba, May 21, 2025 –As the legislative and district elections of June 5, 2025, approach, traditional dance groups in southern Burundi are denouncing restrictions imposed by the
Gitega : a short arrest of members of the CNL party that leaves questions
Methuselah Nijimbere, Pascal Nyambere and Nestor Ciza were arrested Thursday early in the afternoon by Imbonerakure (members of the CNDD-FDD youth league) and the police then taken to the dungeons
Kigali (Rwanda): renewal of identity cards for refugees and reception of new asylum applications
Expired identity cards are those granted in 2017. The UNHCR and the Rwandan government explain that this renewal also means the revision of conditions of granting asylum. Meanwhile, new Burundian
