Kivu-kaskazini : vijiji vyasalia pasina wakaazi

Kivu-kaskazini : vijiji vyasalia pasina wakaazi

Vijiji vingi katika eneo la Jomba wilaya ya Rutshuru mkoa wa Kivu kaskazini mashariki mwa DRC vimesabaki pasina wakaazi kutokana na mapigano kuibuka tena alhamisi kati ya jeshi la FARDC na kundi la M23. Vyanzo eneo hilo vinaarifu kuwa watu wanakimbilia hasa nchini Uganda na kwenye vituo ambako wanaona usalama ni wa hakika. HABARI SOS Médias Burundi

Viongozi tawala wanaeleza kuwa familia kutoka eneo la Ntamugenga na Tarika wanaendelea kuwasili eneo la Rubare mji ambao uko karibu na makao makuu ya Rutshuru.

Wakati huo huo, wakaazi wa maeneo ya kibanda na Rangira wanakwenda kwa wingi kwenye makao makuu ya wilaya ya Rutshuru.

Wakaazi wa Tchengerero na Kabindi wanakimbilia Bunagana na wengi wamevuka mpaka na kuingia nchini Uganda.

Hali ni hiyo pia kwa wakaazi wa Bunagana wanaokimbia eneo hilo la mpakani na kupata hifadhi nchini Uganda.

Wananchi waliokimbilia nchini Uganda walipelekwa katika kambi ya Nakivale, mbali na mpaka.

Jeshi la FARDC ( jeshi la jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo) linaendelea kutuhumu kundi la M23 kuanzisha mapigano kwa lengo la kuzuia nenda rudi kwenye barabara kuu inayotumiwa kupeleka misaada kwa jeshi katika ukanda huo wakati ambapo waasi upande wao wanasema ni jeshi la FARDC lililoshambulia ngome zake na hivyo wakalazimika kujihami.

Previous North-Kivu: villages are emptying of their populations
Next Rwanda-DRC: DRC imetuhumu kwa mara nyingine Rwanda kusaidia kundi la M23 (tangazo)

You might also like

Security

Rumonge: 20 year- imprisonment for a man guilty of murdering his wife

Ernest Havyarimana aka Kabushemeye, 45, was sentenced by the Rumonge High Court (Southwest of the country) to a 20-year principal penal servitude sentence this Wednesday afternoon. The man is convicted

Politic

Gitega : a short arrest of members of the CNL party that leaves questions

Methuselah Nijimbere, Pascal Nyambere and Nestor Ciza were arrested Thursday early in the afternoon by Imbonerakure (members of the CNDD-FDD youth league) and the police then taken to the dungeons

Governance

Bujumbura: EAC heads of state call again for an immediate ceasefire in eastern Congo

In a most extraordinary way, the heads of the East African community members states met in Bujumbura, the economic capital of Burundi, this Saturday, February 4, 2023. The security situation