Kivu-kaskazini : vijiji vyasalia pasina wakaazi
Vijiji vingi katika eneo la Jomba wilaya ya Rutshuru mkoa wa Kivu kaskazini mashariki mwa DRC vimesabaki pasina wakaazi kutokana na mapigano kuibuka tena alhamisi kati ya jeshi la FARDC na kundi la M23. Vyanzo eneo hilo vinaarifu kuwa watu wanakimbilia hasa nchini Uganda na kwenye vituo ambako wanaona usalama ni wa hakika. HABARI SOS Médias Burundi
Viongozi tawala wanaeleza kuwa familia kutoka eneo la Ntamugenga na Tarika wanaendelea kuwasili eneo la Rubare mji ambao uko karibu na makao makuu ya Rutshuru.
Wakati huo huo, wakaazi wa maeneo ya kibanda na Rangira wanakwenda kwa wingi kwenye makao makuu ya wilaya ya Rutshuru.
Wakaazi wa Tchengerero na Kabindi wanakimbilia Bunagana na wengi wamevuka mpaka na kuingia nchini Uganda.
Hali ni hiyo pia kwa wakaazi wa Bunagana wanaokimbia eneo hilo la mpakani na kupata hifadhi nchini Uganda.
Wananchi waliokimbilia nchini Uganda walipelekwa katika kambi ya Nakivale, mbali na mpaka.
Jeshi la FARDC ( jeshi la jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo) linaendelea kutuhumu kundi la M23 kuanzisha mapigano kwa lengo la kuzuia nenda rudi kwenye barabara kuu inayotumiwa kupeleka misaada kwa jeshi katika ukanda huo wakati ambapo waasi upande wao wanasema ni jeshi la FARDC lililoshambulia ngome zake na hivyo wakalazimika kujihami.
You might also like
Rwanda-DRC: a second Congolese soldier killed by Rwandan forces
The Rwandan army had killed a Congolese soldier on Saturday November 19, after he crossed the border and started shooting at his soldiers, the army statement said. INFO SOS Médias
Nyanza-Lac: a former village chief beaten up by an Imbonerakure
Patrice Ntiganzwa, former chief of Muyange vill in Nyanza-Lac district, Makamba province (southern Burundi) was seriously beaten up by an Imbonerakure (CNDD-FDD party youth league member) on Sunday night. The
DRC (Beni) : a new ADF rebel incursion kills ten people in the Banande-Kainama groupment
The Allied Democratic Forces (ADF) rebels made a new deadly attack on the night of Tuesday to Wednesday in the Vido village in the Banande-Kainama groupment, Beni-Mbau sector in the
