Burundi: angalau 25% ya wandishi wa habari walipewa kadi
Baraza la CNC (baraza la uandishi wa habari) siku ya ijumaa ilizindua rasmi shughuli ya kutoa kadi mpya ya uandishi wa habari. Ni idadi ndogo ya wandishi walioweza kupata kadi hiyo. CNC inafahanuwa kuwa sababu kuu ni faili za wahitaji zisizoeneza vigezo au kucheleweshwa. HABARI SOS Médias Burundi
Kwa angalau wandishi elfu moja waliowasilisha maombi ni 240 pekee waliopewa kadi, kulingana na Vestine Nahimana kiongozi wa CNC.
” Kadi zilizotolewa ni chache ukilinganisha na idadi ya walioomba wanaokadiriwa kuwa elfu moja. Idadi kubwa ya wandishi wa habari hawakuweza kupata kadi hiyo sababu hawatimizi vigezo vinavyohitajika ili kupata kadi ya uandishi wa habari. Wengine hawakuwasilisha faili kwa wakati, alifafanua.
Kwa wale waliopata kadi hiyo, aliwaomba kuitumia vizuri.
[….] kadi hiyo inawafungulia milango wandishi wa habari ili kufikia vyanzo vya habari” alisisitiza mama Nahimana.
Moja kati ya masharti ili kupata kadi hiyo mpya wa wandishi wa habari, ni kuwa na mkataba wa kazi na kulipa pesa elfu 15 sarafu za Burundi na na kurudisha kadi ya zamani.
Kadi mpya itakuwa na muda wa miaka mitano.
Tangu mzozo wa 2015 uliosababishwa na muhula mwingine ulioleta utata wa rais Pierre Nkurunziza, viongozi wa Burundi walituhumiwa mara nyingi ” kunyanyasa vyombo vya habari”.
Lakini katika miaka mitatu iliyopita, nchi hiyo ndogo ya afrika ya mashariki ilipanda kwa alama ya rikodi ya kuheshimu uhuru wa habari inayotolewa na shirika la RSF ( ma ripota wasio na mipaka) na kutoka kwenye nafasi ya 160 na kurudi nyuma kwenye nafasi ya 107.
Rikodi hiyo inatathimini mazingira ya uendeshaji kazi ya uandishi wa habari katika nchi na maeneo 180.
You might also like
Mugamba: families from the Batwa community forcibly occupy state property
Around sixty members of the landless Batwa community from the Vyuya hill and zone in the Mugamba commune in Bururi province (southern Burundi) decided to forcibly occupy state land on
Gatumba : the Minister of the Interior opposes the construction of a dike to protect the Rusizi River initiated by inhabitants in collaboration with the diaspora
In a letter to the governor of the province of Bujumbura (western Burundi), the Minister of the Interior recommends that the latter ban any initiative aimed at building a dike
Kayanza: the Rukago market without lavatories
Users of the Rukago market say they do not understand why this trading center does not have toilets, asking the Gahombo commune administration, province of Kayanza (North of the country)
