Bubanza: vijana Imbonerakure wapiga mwanaume mmoja hadi kufariki akiwa hospitali

Bubanza: vijana Imbonerakure wapiga mwanaume mmoja hadi kufariki akiwa hospitali

Lionel Nzoyisaba alikuwa akijulikana kama mwizi tarafani Mpanda mkoa wa Bubanza. Alikuwa akiiba simu katika maduka eneo hilo. Usiku wa kuamkia tarehe mosi disemba, Nzoyisaba alisimamishwa na vijana Imbonerakure akitoka kuiba ndani ya duka moja. Walimuchapa. Mwishowe, alifariki dunia akiwa kwenye hospitali ya Mpanda, mkoa wa Bubanza (magharibi mwa Burundi). HABARI SOS Médias Burundi

Kisa cha mwisho cha wizi wake kilikuwa siku ya ijumaa.

” Mwanamke mmoja alifunga duka lake bila kujuwa kuwa Lionel alikuwa ndani. Wakati akijaribu kutoka akiwa na bidhaa alizoiba, jirani alimukamata na kuomba msaada ” alifafanua jirani mwingine mkaazi wa kitongoji cha Nyabikere katika kijiji cha Musenyi.

Baada ya kusimamishwa na vijana wafuasi wa chama tawala, Lionel Nzoyisaba alipelekwa kwenye mto Gifugwe katika kijiji hicho. Vijana hao walimpiga kinyama.

” Walimumwagia maji muilini ili ateseke wakati akichapwa. Mtu huyo walimurudusha akiwa katika hali mbaya. Afisa wa polisi aliyemuhoji, alimutia jela badala ya kumupeleka moja kwa moja hospitali. Usiku huo huo akiwa katika hali mahtuti, alipelekwa kwenye hospitali kuu ya Mpanda na kufa akiwa kwenye hospitali hiyo, vyanzo vyetu vinahakikisha.

Mke wa muhanga huyo anawatuhumu viongozi wa tarafa ya Mpanda, mkuu wa kijiji cha Musenyi ” nia ya kutaka kuzimisha kisa hicho na kuacha kuwafuatilia Imbonerakure wanaotuhumiwa katika mkasa huo”.

” Nimemkosa mume wangu ambaye alikamatwa na Imbonerakure, na kupigwa katika usiku huo. Na badala ya kuwakamata watuhumiwa wa maovu hayo, wanasema kuwa kifo hicho hakina maana kwao”, anakosoa mke huyo wa hayati.

Previous Cibitoke: miili tisa ya waasi wa Rwanda ilipatikana katika msitu wa kibira
Next Burundi: angalau 25% ya wandishi wa habari walipewa kadi

You might also like

Economy

Gitega: the FRODEBU party denounces the untenable cost of living for the population

As Burundi prepares for the 2025 elections, the Sahwanya FRODEBU party denounces the high cost of living across the country. It was declared on Saturday August 17 in Gitega, the

Politic

Rwanda-DRC: the Rwandan army announces that it has repelled an aggression by Congolese soldiers

The incident took place this Wednesday around 4:30 a.m, a press release from the Rwandan army says. It took place between the district of Rusizi in the western province of

Governance

Kiremba : fertilizer delays and government inaction threaten farmers’ food security

SOS Médias Burundi Kiremba, February 26, 2026 – In the district of Kiremba, in Butanyerera province, northern Burundi, farmers are experiencing a particularly anxious season. As the second major agricultural