Bubanza: vijana Imbonerakure wapiga mwanaume mmoja hadi kufariki akiwa hospitali

Bubanza: vijana Imbonerakure wapiga mwanaume mmoja hadi kufariki akiwa hospitali

Lionel Nzoyisaba alikuwa akijulikana kama mwizi tarafani Mpanda mkoa wa Bubanza. Alikuwa akiiba simu katika maduka eneo hilo. Usiku wa kuamkia tarehe mosi disemba, Nzoyisaba alisimamishwa na vijana Imbonerakure akitoka kuiba ndani ya duka moja. Walimuchapa. Mwishowe, alifariki dunia akiwa kwenye hospitali ya Mpanda, mkoa wa Bubanza (magharibi mwa Burundi). HABARI SOS Médias Burundi

Kisa cha mwisho cha wizi wake kilikuwa siku ya ijumaa.

” Mwanamke mmoja alifunga duka lake bila kujuwa kuwa Lionel alikuwa ndani. Wakati akijaribu kutoka akiwa na bidhaa alizoiba, jirani alimukamata na kuomba msaada ” alifafanua jirani mwingine mkaazi wa kitongoji cha Nyabikere katika kijiji cha Musenyi.

Baada ya kusimamishwa na vijana wafuasi wa chama tawala, Lionel Nzoyisaba alipelekwa kwenye mto Gifugwe katika kijiji hicho. Vijana hao walimpiga kinyama.

” Walimumwagia maji muilini ili ateseke wakati akichapwa. Mtu huyo walimurudusha akiwa katika hali mbaya. Afisa wa polisi aliyemuhoji, alimutia jela badala ya kumupeleka moja kwa moja hospitali. Usiku huo huo akiwa katika hali mahtuti, alipelekwa kwenye hospitali kuu ya Mpanda na kufa akiwa kwenye hospitali hiyo, vyanzo vyetu vinahakikisha.

Mke wa muhanga huyo anawatuhumu viongozi wa tarafa ya Mpanda, mkuu wa kijiji cha Musenyi ” nia ya kutaka kuzimisha kisa hicho na kuacha kuwafuatilia Imbonerakure wanaotuhumiwa katika mkasa huo”.

” Nimemkosa mume wangu ambaye alikamatwa na Imbonerakure, na kupigwa katika usiku huo. Na badala ya kuwakamata watuhumiwa wa maovu hayo, wanasema kuwa kifo hicho hakina maana kwao”, anakosoa mke huyo wa hayati.

Previous Cibitoke: miili tisa ya waasi wa Rwanda ilipatikana katika msitu wa kibira
Next Burundi: angalau 25% ya wandishi wa habari walipewa kadi

You might also like

Society

Burundi : members of the LGBTQ community fear persecution after President Neva’s remarks

In Burundi, people in same-sex relationships feel they are at great risk. This came after remarks by President Évariste Ndayishimiye who called for “homosexuals to be stoned” last Friday. The

Human Rights

Beni : zaidi ya watu 70 wauwawa katika kipindi cha siku 6

Zaidi ya watu 70 waliuwawa katika kipindi cha siku sita zilizopita katika wilaya ya Beni , Kivu kaskazini katika vijiji mbali mbali mashariki mwa DRC. Waliotekeleza mauwaji hayo ni waasi

Politic

Rugombo : two Imbonerakure seriously beaten up by residents

The incident took place on the night of Sunday to Monday in the locality of Rusiga. It is in the district of Rugombo in the province of Cibitoke (northwest Burundi).