Burundi: angalau 25% ya wandishi wa habari walipewa kadi

Burundi: angalau 25% ya wandishi wa habari walipewa kadi

Baraza la CNC (baraza la uandishi wa habari) siku ya ijumaa ilizindua rasmi shughuli ya kutoa kadi mpya ya uandishi wa habari. Ni idadi ndogo ya wandishi walioweza kupata kadi hiyo. CNC inafahanuwa kuwa sababu kuu ni faili za wahitaji zisizoeneza vigezo au kucheleweshwa. HABARI SOS Médias Burundi

Kwa angalau wandishi elfu moja waliowasilisha maombi ni 240 pekee waliopewa kadi, kulingana na Vestine Nahimana kiongozi wa CNC.

” Kadi zilizotolewa ni chache ukilinganisha na idadi ya walioomba wanaokadiriwa kuwa elfu moja. Idadi kubwa ya wandishi wa habari hawakuweza kupata kadi hiyo sababu hawatimizi vigezo vinavyohitajika ili kupata kadi ya uandishi wa habari. Wengine hawakuwasilisha faili kwa wakati, alifafanua.

Kwa wale waliopata kadi hiyo, aliwaomba kuitumia vizuri.

[….] kadi hiyo inawafungulia milango wandishi wa habari ili kufikia vyanzo vya habari” alisisitiza mama Nahimana.

Moja kati ya masharti ili kupata kadi hiyo mpya wa wandishi wa habari, ni kuwa na mkataba wa kazi na kulipa pesa elfu 15 sarafu za Burundi na na kurudisha kadi ya zamani.
Kadi mpya itakuwa na muda wa miaka mitano.

Tangu mzozo wa 2015 uliosababishwa na muhula mwingine ulioleta utata wa rais Pierre Nkurunziza, viongozi wa Burundi walituhumiwa mara nyingi ” kunyanyasa vyombo vya habari”.

Lakini katika miaka mitatu iliyopita, nchi hiyo ndogo ya afrika ya mashariki ilipanda kwa alama ya rikodi ya kuheshimu uhuru wa habari inayotolewa na shirika la RSF ( ma ripota wasio na mipaka) na kutoka kwenye nafasi ya 160 na kurudi nyuma kwenye nafasi ya 107.

Rikodi hiyo inatathimini mazingira ya uendeshaji kazi ya uandishi wa habari katika nchi na maeneo 180.

Previous Bubanza: vijana Imbonerakure wapiga mwanaume mmoja hadi kufariki akiwa hospitali
Next Nakivale (Uganda): torrential rains cause injuries and material damage

You might also like

Economy

Bubanza : women’s informal trade, the economic pillar of households

SOS Médias Burundi Bubanza, April 28, 2025 – In Bubanza, in western Burundi, informal trade is predominantly driven by women. Thanks to their dynamism and the ingenuity of their initiatives,

Society

Bururi : drinking water shortage in Rutovu, residents sound the alarm

SOS Médias Burundi Rutovu, September 19, 2025 – The population of Rutovu, in the Bururi district, Burunga province in southern Burundi, is sounding the alarm about a drinking water shortage

Society

Rutana: a sentence of a fine of 150 thousand Burundi francs imposed on three people

A sentence of a fine of 150,000 Burundi francs per person was imposed on three people, including a prisoner caught having sex. INFO SOS Médias Burundi The prisoner’s partner as