Burundi: angalau 25% ya wandishi wa habari walipewa kadi
Baraza la CNC (baraza la uandishi wa habari) siku ya ijumaa ilizindua rasmi shughuli ya kutoa kadi mpya ya uandishi wa habari. Ni idadi ndogo ya wandishi walioweza kupata kadi hiyo. CNC inafahanuwa kuwa sababu kuu ni faili za wahitaji zisizoeneza vigezo au kucheleweshwa. HABARI SOS Médias Burundi
Kwa angalau wandishi elfu moja waliowasilisha maombi ni 240 pekee waliopewa kadi, kulingana na Vestine Nahimana kiongozi wa CNC.
” Kadi zilizotolewa ni chache ukilinganisha na idadi ya walioomba wanaokadiriwa kuwa elfu moja. Idadi kubwa ya wandishi wa habari hawakuweza kupata kadi hiyo sababu hawatimizi vigezo vinavyohitajika ili kupata kadi ya uandishi wa habari. Wengine hawakuwasilisha faili kwa wakati, alifafanua.
Kwa wale waliopata kadi hiyo, aliwaomba kuitumia vizuri.
[….] kadi hiyo inawafungulia milango wandishi wa habari ili kufikia vyanzo vya habari” alisisitiza mama Nahimana.
Moja kati ya masharti ili kupata kadi hiyo mpya wa wandishi wa habari, ni kuwa na mkataba wa kazi na kulipa pesa elfu 15 sarafu za Burundi na na kurudisha kadi ya zamani.
Kadi mpya itakuwa na muda wa miaka mitano.
Tangu mzozo wa 2015 uliosababishwa na muhula mwingine ulioleta utata wa rais Pierre Nkurunziza, viongozi wa Burundi walituhumiwa mara nyingi ” kunyanyasa vyombo vya habari”.
Lakini katika miaka mitatu iliyopita, nchi hiyo ndogo ya afrika ya mashariki ilipanda kwa alama ya rikodi ya kuheshimu uhuru wa habari inayotolewa na shirika la RSF ( ma ripota wasio na mipaka) na kutoka kwenye nafasi ya 160 na kurudi nyuma kwenye nafasi ya 107.
Rikodi hiyo inatathimini mazingira ya uendeshaji kazi ya uandishi wa habari katika nchi na maeneo 180.
You might also like
Kirundo : the State accused of abandoning thousands of citizens to a protracted water crisis with serious health consequences
Residents of Kiri, Kiyonza, and Ruhehe face a chronic drinking water shortage SOS Médias Burundi Kirundo, June 9, 2026 – A severe drinking water shortage has been affecting residents of
Rutana : Is the provincial director of education a victim of having eaten from the plate of the governor and the boss of the CNDD-FDD?
The provincial director of education in Rutana, Emmanuel Nsengiyumva, had taken the decision to transfer teachers and appoint school principals at the beginning of the school year. These transfers and
Kayanza: four men died after drinking forbidden beer
These four men died during the night from Thursday to Friday. The victims were with three other people who are currently under treatments. The tragedy took place in the capital
