Burundi: angalau 25% ya wandishi wa habari walipewa kadi
Baraza la CNC (baraza la uandishi wa habari) siku ya ijumaa ilizindua rasmi shughuli ya kutoa kadi mpya ya uandishi wa habari. Ni idadi ndogo ya wandishi walioweza kupata kadi hiyo. CNC inafahanuwa kuwa sababu kuu ni faili za wahitaji zisizoeneza vigezo au kucheleweshwa. HABARI SOS Médias Burundi
Kwa angalau wandishi elfu moja waliowasilisha maombi ni 240 pekee waliopewa kadi, kulingana na Vestine Nahimana kiongozi wa CNC.
” Kadi zilizotolewa ni chache ukilinganisha na idadi ya walioomba wanaokadiriwa kuwa elfu moja. Idadi kubwa ya wandishi wa habari hawakuweza kupata kadi hiyo sababu hawatimizi vigezo vinavyohitajika ili kupata kadi ya uandishi wa habari. Wengine hawakuwasilisha faili kwa wakati, alifafanua.
Kwa wale waliopata kadi hiyo, aliwaomba kuitumia vizuri.
[….] kadi hiyo inawafungulia milango wandishi wa habari ili kufikia vyanzo vya habari” alisisitiza mama Nahimana.
Moja kati ya masharti ili kupata kadi hiyo mpya wa wandishi wa habari, ni kuwa na mkataba wa kazi na kulipa pesa elfu 15 sarafu za Burundi na na kurudisha kadi ya zamani.
Kadi mpya itakuwa na muda wa miaka mitano.
Tangu mzozo wa 2015 uliosababishwa na muhula mwingine ulioleta utata wa rais Pierre Nkurunziza, viongozi wa Burundi walituhumiwa mara nyingi ” kunyanyasa vyombo vya habari”.
Lakini katika miaka mitatu iliyopita, nchi hiyo ndogo ya afrika ya mashariki ilipanda kwa alama ya rikodi ya kuheshimu uhuru wa habari inayotolewa na shirika la RSF ( ma ripota wasio na mipaka) na kutoka kwenye nafasi ya 160 na kurudi nyuma kwenye nafasi ya 107.
Rikodi hiyo inatathimini mazingira ya uendeshaji kazi ya uandishi wa habari katika nchi na maeneo 180.
You might also like
Gitega: watu 24 watuhumiwa kufanya mapenzi ya watu wa jinsia moja wako jela
Wakiwa wanaume, wanawake na vijana, watu hao 24 wako gerezani tangu februari 23 iliyopita katika jiji kuu la kisiasa la Gitega (kati kati mwa Burundi). Wanatuhumiwa kuunda jenge la wapenzi
Burundi: Viongozi walikatalia kwa mara ya tatu shirika la AC-GENOCIDE Cirimoso kuadhimisha kumbukumbu ya mauwaji ya Kibimba
Shirika la AC-GENOCIDE Cirimoso halikuruhusiwa kuelekea kwenye mrana wa ukumbusho wa mauwaji ya wanafunzi 150 wa kabila la watutsi waliuwawa tarehe 21 oktoba mwaka 1993 baada ya mauwaji ya rais
Kayanza : at least 16 people bitten by stray dogs
At least 16 people from the districts of Kayanza, Gatara and Muruta in Kayanza province (northern Burundi) have been bitten by stray dogs. The population speaks of panic “especially since
