Cibitoke: miili tisa ya waasi wa Rwanda ilipatikana katika msitu wa kibira

Cibitoke: miili tisa ya waasi wa Rwanda ilipatikana katika msitu wa kibira

Alasiri siku ya ijumaa, walinzi wa msitu waliona miili tisa ikianza kuharibika kwenye mlima wa Gafumbegeti. Ni katika kijiji cha Butahana tarafani Mabayi mkoa wa Cibitoke (kaskazini-magharibi mwa Burundi). Kijiji hicho kinapataka na msitu wa Kibira. Wakaazi wa kijiji hicho wanasema kuwa maiti za waasi wa Rwanda zimekuwa zikigundulika. HABARI SOS Médias Burundi

Mapigano ya mwisho kati ya jeshi la Burundi na waasi wanaopambana dhidi ya Kigali yalipelekea angalau waasi tisa kuuwawa kwa mjibu wa vyanzo vyetu.

” Niliona miili inayoanza kuharibika ya watu wanaovalia sare za jeshi la Kongo siku ya ijumaa alasiri tarehe 2 disemba kwenye mpaka wa msitu wa Kibira [….]” alitoa ushuhuda huo mlinzi wa msitu mmoja ambaye alikuwa wa kwanza kuona miili hiyo na kuwaambia wenzake.

Chanzo cha kijeshi upande wake, kinahakikisha kuwa mapigano makali kati ya jeshi la Burundi na waasi wa Rwanda wakiwa na makao yao nchini DRC yalipelekea jeshi la FDNB kukamata silaha nzito na zile ndogo ndogo nyingi”

Ngome zao nyingi zilikamatwa pia. Zilikuwa zinakaliwa na waasi tangu mwaka wa 2015″.

Kiongozi tawala mmoja anathibitisha hali hiyo.

” Waakazi wengi walikimbia majumba yao. Wanapewa hifadhi kwenye makao makuu ya tarafa ya Mabayi”, anasema.

Afisa mkuu anayehusika na operesheni za kijeshi tarafani Mabayi na Bukinanyana anahakikisha taarifa hizo na kudai kuwa matokeo ya operesheni hiyo ni ya kuridhisha. Anafahamisha pia kuwa ” wanajeshi wetu kwa sasa wanaendesha operesheni za kumalizia mahala popote ambako bado waasi wanaendelea kujihami huku wengi wakiwa walikimbia”. Anawaomba wananchi kushirikiana na jeshi katika kuimarisha usalama kwa kufichuwa kila kitu kinacholeta wasi wasi.

Akiulizwa kuhusu hali hiyo, mkuu wa tarafa ya Mabayi, Nicodème Ndahabonyimana anathibitisha habari hizo na kuzidi kuwa ” milio ya sihala nzito imekuwa ikisikika mara kwa mara mnamo siku zilizopita katika msitu wa hifadhi wa Kibira”.

Previous Cibitoke: nine bodies of Rwandan rebels found in Kibira
Next Bubanza: vijana Imbonerakure wapiga mwanaume mmoja hadi kufariki akiwa hospitali

You might also like

Security

Makamba : chumba cha kuhifadhi maiti hakifanyi kazi kwa takriban mwaka mmoja sasa

Kwa mjibu wa wafanyakazi kwenye hospitali hiyo ya Makamba ( kusini mwa Burundi) pamoja na familia zilizokosa watu, chumba cha kuhifadhi maiti sasa ni takriban mwaka mmoja kikiwa hakifanyi kazi.

Security

Photo of the week: nearly a hundred hostages freed in Beni and Irumu in three months

At least 98 hostages, in hands of the ADF (Allied Democratic Forces), were recently freed by the DRC and Uganda’s coalition forces. The operations took place in Beni (North Kivu

Security

Rumonge : Internal disputes within the CNDD-FDD before the village elections

SOS Médias Burundi Rumonge, August 22, 2025 – With village elections scheduled for Monday, August 25, the Kanyenkoko neighborhood, located in the city of Rumonge, in Burunga province (southern part