Goma: mwandishi wa habari Jimmy Shukrani Bakomera aachiliwa huru
Mwenzetu huyo amechikiwa huru ijumaa hii asubuhi. Alikuwa katika gereza la ANR ( idara ya ujasusi ya Kongo) katika mji wa Goma (makao makuu ya mkoa wa Kivu kaskazini) tangu alhamisi mchana. Alituhumiwa “kushirikiana na kundi la M23”, kundi linalochukuliwa na viongozi wa Kongo kama kundi la “kigaidi “. HABARI SOS Médias Burundi
Jimmy Shukrani Bakomera aliambia SOS Médias Burundi kuwa ” nimeachiwa huru na niko salama na mzima, hakuna aliyeninyanyasa”.
Mwandishi huyo na ripota wa VOA( Sauti ya Amerika) alihojiwa kuhusu tuhuma dhidi yake za kushirikiana na wajumbe na watu wa karibu na kundi la M23.
” Niliulizwa kuhusu M23. Walinionyesha orodha ya wajumbe wa kundi la M23 wengi wao wakiwa raia wa Kongo. Niliwaambia kuwa sifahamu hata mmoja”, ametoa ushuhuda huo.
Ni afisa wa idara ya ujasusi ndani ya Masisi aliyesimamisha mwandishi huyo katika eneo la Karuba. Alimutuhumu kushirikiana na kundi la M23 baada ya kumukutaakifanya mahojiano na jamii ya wanaotumia lugha ya Kinyarwanda wanaoishi nchi DRC. Alikuwa akifanya ripoti kuhusu zoezi la kuorodhesha wapiga kura linalokosolewa na mashirika ya kiraia ndani ya mkoa wa Kivu-kaskazini kutokana na usalama mdogo unaoripotiwa mashariki mwa Kongo.
” Watu wanaotumia lugha ya Kinyarwanda wana haki ya kujieleza na hawatakiwi kufananishwa na washirika wa kundi la M23 na madawi wa nchi” anadai mwandishi huyo.
” Ninawashukuru wandishi wa habari na wanaharakati pamoja na watu wengine waliochangia ili niweze kuachiliwa huru”, amebaini Jimmy Shukrani Bakomera.
Tangu kuibuka tena kwa kundi la M23, wananchi wanaotumia lugha ya Kinyarwanda ambao wanaishi nchini DRC wanatuhumiwa kusaidia waasi na kufanya upelelezi kwa ajili ya Rwanda.
Kundi hilo la zamani la watutsi lililochukuwa silaha mwishoni mwa 2021 likituhumu viongozi wa Kongo kutoheshimu ahadi yake kuhusu kuwarudisha katika maisha ya kiraia wapiganaji wake, lilichukuwa udhibiti wa maeneo mengi ya Kivu kaskazini likiwemo eneo la Bunagana, jiji la mpakani na Uganda tangu mwishoni mwa juni 2022.
Viongozi wa Kongo bado wanakubaliana kuwa kundi hilo linapata usaidizi kutoka Rwanda jambo ambalo Rwanda inapinga kila siku.
You might also like
Tanzania : Nduta camp forcibly emptyed, Burundian refugees expelled amid violence and silence
SOS Médias Burundi Kigoma, April 27, 2026 — In the Nduta camp, located in the Kigoma region of northwestern Tanzania, thousands of Burundian refugees are denouncing forced expulsions carried out
Nduta (Tanzania) : a former refugee wanted by the police
He is however known for his zeal in collaborating with secret services in the camp to track down and mistreat other refugees. This Burundian who had renounced his refugee status
Gitega : three Imbonerakure suspected of murder in detention
Égide Manirambona, Sylvain Kwizera and Roger Nahayo, members of the CNDD-FDD youth league, the Imbonerakure, are detained in the central prison of Gitega (political capital). They are suspects in “the
