Masisi: wakaazi wanaomba amani kupatikana kabla ya kujiandikisha kwenye uchaguzi

Masisi: wakaazi wanaomba amani kupatikana kabla ya kujiandikisha kwenye uchaguzi

Wananchi wakaazi wa wilaya ya Masisi katika mkoa wa Kivu-kaskazini wanatoa wito kwa viongozi kumaliza tatizo la usalama mdogo kabla ya kuanza kwa zoezi la kuorodhesha wapiga kura eneo hilo la mkoa wa Kivu-kaskazini. HABARI SOS Médias Burundi

Baadhi ya wakaazi wa kitongoji cha Mupfunyi-Karuba walihakikisha kuwa watajiandikisha wakati usalama utakuwa umerejea katika eneo hilo.

“Tutaanza kujiorodhesha wakati usalama utakuwa umeimarika ndani ya wilaya ya Masisi. Tuko katika hali mbaya ya usalama”, alibaini Gervais Bahati mkulima wa eneo la Karuba.

Kwa mjibu wake, haiwezekani kujiandikisha wakati ambapo wananchi wa Kongo wengi eneo hilo waliyatoroka makaazi yao.

” Jambo la kwanza ni kuona wananchi wenzetu wanaoishi katika kambi za wakimbizi wa ndani wakirejea katika maeneo yao ya asili. Hatuwezi kuanza kujiorodhesha wakati ambapo ndugu zetu wakiteseka ndani ya kambi wilayani Nyiragongo na maeneo mengine” alilalamika baba wa familla.

Jean Bosco Sebishishimbo Rubuha mbunge aliyechaguliwa eneo la Masisi anafahamisha kuwa serikali inatakiwa kumaliza tatizo la usalama mdogo ndani ya mkoa harafu badaye litafuata zoezi la kuandikisha wapiga kura”.

Idadi kubwa ya wananchi walitoroka mapigana na hawana njia ya kuwasili kwenye vituo vya kujiandikisha “, alifafanua mwakilishi huyo wa wananchi.

” Hatuelewi namna serikali yetu inaweza kuanza mchakato wa uchaguzi bila kujali maisha ya kila siku ya wananchi wa Kongo kwa jumla na hususan maisha wakaazi wa mkoa wa kivu kaskazini. Kwa mtanzamo wetu, usalama ni jambo la msingi, uandikishaji ni badaye”, alisisitiza.

Uandikishaji wa wapiga kura katika eneo la mashariki mwa Kongo ulianza alhamisi iliyopita. Mbali na katika miji kadhaa ambako wajumbe wa jamii ya wanaotumia lugha ya Kinyarwanda na kirundi wanaoishi nchini DRC pamoja pia na watutsi wa Kongo na wajumbe wa jamii ya Banyamulenge walijikuta wakinyimwa haki yao ya kujiandikisha mchakato unaendelea vizuri. Viongozi tawala walikataza wanzilishi wa vuguvugu linalotoa mwito kwa raia wengine wa Kongo na wajumbe wa CENI ” kuwatenga watu wa jamii hizo”.

Previous Muramvya: the provincial prison remains overcrowded despite the release of around twenty detainees
Next Kirundo : kiongozi wa Imbonerakure azuiliwa jela

You might also like

Security

Bukinanyana (Cibitoke) : the number of traffic accidents is skyrocketing

According to sources within road transport companies, at least 12 people have been killed in accidents and around thirty seriously injured in less than two months. This happened in Bukinanyana

Refugees

Cibitoke: when land spoliaton pushes owners into exile

In a period of three months, more than 300 people fled the communes of Rugombo and Buganda in the province of Cibitoke (north-west of Burundi). They decided to go into

Politic

Burundi: the turmoil of Rwasa

The Burundian Minister of Internal Affairs Martin Niteretse confirmed on Monday the conclusions of the extraordinary congress which placed Nestor Girukwishaka at the head of the CNL party on March