Kakuma (Kenya): miezi mitano pasina kupewa chakula

Kakuma (Kenya): miezi mitano pasina kupewa chakula

Wakimbizi ndani ya kambi ya Kakuma nchini Kenya wanasikitishwa na hali ya kuchelewa kwa msaada wao wa pesa kwa kipindi cha miezi mitano. Wanahakikisha kuwa ” njaa inatupiga vibaya”. HABARI SOS Médias Burundi

Wakimbizi wa kambi ya Kakuma walikwenda kutupa kadi zao za benki mbele ya ofisi za HCR kama kuonyesha hasira yao kutokana na kuchelewa kwa msaada wao.

” Jiulizeni, tunaingia mwezi wa sita. Kawaida wanatupatia shilingi 100 kila mtu na kila mwezi kwa watu wa jinsia ya kiume pamoja na shilingi 350 kwa kila mwanamke na msichana. Pesa hiyo hutusaidia kununua kuni za kupikia, chumvi, sababu au vileso kwa ajili ya usafi wa mwanamke. Kwa hiyo, wanafikiri tunaishi kivipi miezi sita pasina kupewa msaada ? ” anajiuliza raia wa Burundi eneo hilo.

Ndani ya kambi hiyo, mwanamke anachukuliwa kama chanzo muhimu cha mapato.

” Kwa sasa, wanazaa watoto wengi na kadiri unapopata watoto wengi wa kike unakuwa na bahati kubwa sababu wanapewa pesa za ziada “, wa baba katika familia wanasema kwa mizaha.

Wakimbizi waliozungumza na SOS Médias Burundi wanaomba HCR ” kutukumbuka na kutuhakikishia ulinzi” kinyume na hayo shirika hilo la umoja wa mataifa litakuwa limefeli katika jukumu lake.

HCR pamoja na mashirika mengine ya misaada katika eneo la Afrika mashariki walisema ni kutokana na tatizo la ukosefu wa ufadhili mnamo siku hizi.

Kambi ya Kakuna inawapa hifadhi zaidi ya wakimbizi laki mbili kutoka mataifa mbali mbali wakiwemo warundi zaidi ya elfu ishirini.

Previous Cibitoke: general increase in the prices of basic necessities
Next Masisi: resurgence of hostilities between the FARDC and the M23

You might also like

Refugees

Tanzania: Malnutrition-related diseases threaten under five children in Burundian refugee camps

Nearly two thousand children suffer from malnutrition associated diseases in the Burundian refugee camps in Tanzania. This limits their mental and physical development, according to specialists. INFO SOS Médias Burundi

Refugees

Dzaleka (Malawi): the start of the school year reckoned bad

A week before the start of the school year, refugees in Dzaleka camp in Malawi are complaining that all the places in the camp’s only school are reserved for the

Human Rights

Mahama (Rwanda): ration quotas revised upwards for some refugees

The monthly amount in currency allocated to each refugee in the Mahama camp increases from 7,000 Frw (7 USD) to 10,000 Frw (10 USD) for the poorest (Social Category I)