Kabarore: walimu walazimishwa kutoa michango
Walimu katika tarafa ya Kabarore mkoa wa Kayanza (Kaskazini mwa Burundi) walilazimishwa kutoa michango ya pesa ili kufadhili miradi ya chama tawala cha CNDD-FDD. Wahusika wanatupilia mbali kile wanachoita “ukiukwaji wa haki za binadamu”. HABARI ya SOS Medias Burundi
Tangu mwaka wa 2015, walimu katika baadhi ya tarafa za Kayanza wanalazimishwa kutoa michango kwa nguvu ili kufadhili miradi ya chama tawala nchini Burundi. Tarafani Kabarore, walezi hawachangii tena.
Vyanzo vyetu katika walimu wanatuarifu kuwa michango hiyo ni ya kila mwezi.
Walimu wakuu wa shule za msingi wanatoa kati ya 5000 na 10000 sarafu ya Burundi kutokana na idadi ya wanafunzi kwenye shule hiyo.
“Sisi walimu tunatoa elfu moja au elfu mbili. Kwa kipindi fulani walitulazimisha kutoa elfu 3 sarafu za Burundi, alieleza mwalimu.
Jambo la kusikitisha kwa mjibu wa walimu, hakuna anayeepukika.
“Hata wafuasi wa vyama vingine wanahusishwa”, anahakikisha mwalimu mwengine.
Wanaopinga kuchukuliwa kama wasiokuwa na utu.
“Mara tunaitwa mbwa , mara tunapewa jina la mbwa mwitu”, alithibitisha mwalimu mufuasi wa chama cha upinzani.
Walimu wanasema kuchoshwa na michango hiyo hasa ikizingatiwa kuwa hawajuwi inapoelekea pesa hiyo.
“Hakuna matokeo kutoka kwenye michango yetu”, analaani mwalimu mkuu wa shule, mufuasi wa chama tawala cha CNDD-FDD.
Walimu waliojieleza kwenye SOS Medias Burundi wanataja kuwa kuchangisha kwa nguvu ni “ukiukwaji wa haki za binadamu”. Wanaomba serikali na viongozi wa chama cha CNDD-FDD kwa ngazi ya taifa kuingilia kati na kusimamisha mwenendo huo.
Viongozi wa elimu katika mkoa wa Kayanza, hawakupatikana ili kujieleza juu ya madai hayo.
You might also like
Kayogoro : hali ya wasi wasi yawakabili wananchi kutokana na mazoezi ya kijeshi ya Imbonerakure
Imbonerakure, wajumbe wa tawi la vijana wafuasi wa chama tawala, wanafanya mazoezi ya kijeshi hususan usiku. Mazoezi hayo yanafanyika katika vijijini vyote vya tarafa ya Kayogoro katika mkoa wa Makamba
Burunga: wakufunzi na watahiniwa wa kuhesabu wanadai gharama zao za usafiri
Tangu kuanza kwa mafunzo hayo, wadadisi wa watahiniwa kutoka jimbo la Burunga (kusini mwa Burundi), kwa mujibu wa kitengo kipya cha utawala, wamelalamika kuwa bado hawajapokea gharama za usafiri. Mafunzo
Burundi: maseneta wana shaka kuhusu utoaji wa fedha “kubwa” kwa wizara
Wakati wa kipindi cha maswali ya mdomo cha wabunge katika mji mkuu wa kisiasa wa Gitega (katikati mwa Burundi), Waziri wa Fedha alikabiliwa hasa na maswali kuhusiana na bajeti ya
