Kabarore: walimu walazimishwa kutoa michango
Walimu katika tarafa ya Kabarore mkoa wa Kayanza (Kaskazini mwa Burundi) walilazimishwa kutoa michango ya pesa ili kufadhili miradi ya chama tawala cha CNDD-FDD. Wahusika wanatupilia mbali kile wanachoita “ukiukwaji wa haki za binadamu”. HABARI ya SOS Medias Burundi
Tangu mwaka wa 2015, walimu katika baadhi ya tarafa za Kayanza wanalazimishwa kutoa michango kwa nguvu ili kufadhili miradi ya chama tawala nchini Burundi. Tarafani Kabarore, walezi hawachangii tena.
Vyanzo vyetu katika walimu wanatuarifu kuwa michango hiyo ni ya kila mwezi.
Walimu wakuu wa shule za msingi wanatoa kati ya 5000 na 10000 sarafu ya Burundi kutokana na idadi ya wanafunzi kwenye shule hiyo.
“Sisi walimu tunatoa elfu moja au elfu mbili. Kwa kipindi fulani walitulazimisha kutoa elfu 3 sarafu za Burundi, alieleza mwalimu.
Jambo la kusikitisha kwa mjibu wa walimu, hakuna anayeepukika.
“Hata wafuasi wa vyama vingine wanahusishwa”, anahakikisha mwalimu mwengine.
Wanaopinga kuchukuliwa kama wasiokuwa na utu.
“Mara tunaitwa mbwa , mara tunapewa jina la mbwa mwitu”, alithibitisha mwalimu mufuasi wa chama cha upinzani.
Walimu wanasema kuchoshwa na michango hiyo hasa ikizingatiwa kuwa hawajuwi inapoelekea pesa hiyo.
“Hakuna matokeo kutoka kwenye michango yetu”, analaani mwalimu mkuu wa shule, mufuasi wa chama tawala cha CNDD-FDD.
Walimu waliojieleza kwenye SOS Medias Burundi wanataja kuwa kuchangisha kwa nguvu ni “ukiukwaji wa haki za binadamu”. Wanaomba serikali na viongozi wa chama cha CNDD-FDD kwa ngazi ya taifa kuingilia kati na kusimamisha mwenendo huo.
Viongozi wa elimu katika mkoa wa Kayanza, hawakupatikana ili kujieleza juu ya madai hayo.
You might also like
Kayanza: Mgombea ubunge wa CNDD-FDD akamatwa baada ya kukutana, kesi yenye mielekeo ya kisiasa
SOS Médias Burundi Bujumbura, Mei 28, 2025 – Vincent Ndagijimana, naibu mgombea katika orodha ya chama tawala cha CNDD-FDD katika jimbo jipya la Butanyerera (kaskazini mwa Burundi), alikamatwa Jumatatu hii,
Uchaguzi wa Juni 5: Washirika wa Rwasa Waituhumu Serikali kwa Kuzuia Mashindano
SOS Médias Burundi Bujumbura, Juni 3, 2025—Siku mbili kabla ya uchaguzi wa manispaa na wabunge uliopangwa kufanyika Juni 5, upinzani wa Burundi unaibua wasiwasi. Wakati Aimé Magera, mwakilishi wa kimataifa
Burunga: Uzinduzi wa kampeni ya CNDD-FDD, kati ya matokeo ya shangwe na mashaka ya wengi
SOS Media Burundi Burunga, Mei 19, 2025 – Chama cha CNDD-FDD kilizindua rasmi kampeni yake ya uchaguzi kwa ajili ya uchaguzi wa wabunge na manispaa katika mkoa wa Burunga (kusini-mashariki),
