Burundi : Vijana ambao hawajafunga ndoa hawana ruhsa ya kutumia mipango ya uzazi wa majira (waziri wa afya)
Waziri wa afya Sylvie Nzeyimana alifahamisha hayo siku ya jumanne katika mji mkuu wa biashara Bujumbura. Ni kando ya kongamano kuu la akinamama viongozi.
Kwa mjibu wa waziri Nzeyimana, waliofunga ndoa peke ndio wanaohusishwa na mipango wa uzazi wa majira. HABARI ya SOS Medias Burundi
Akijibu swali wakati wa muelezo wake kando na mkutano mkuu wa akinamama viongozi, Daktari Sylvie Nzeyimana amesema hayo kwa dhahiri.
” Vijana wanatakiwa kufundishwa kuhusu afya ya uzazi. Hawawezi kufanya tendo la ndoa kwa sababu linafanywa na watu waliofunga ndoa peke” alibaini hayo waziri Nzeyimana kando na kongamano kuu la akinamama viongozi ijumanne hii.
Hata hivo amemuomba waziri wa elimu kuongeza mikutano ya kuhamasisha kuhusu uzazi wa majira mashuleni.
Kwa mjibu wa takwimu za serikali ya Burundi, asilimia 38 ya akinamama walijiunga na mpango wa uzazi wa majira katika nchi hii ndogo ya afrika mashariki.
Mashirika ya vijana wao wanafahamisha kuwa vijana kati ya miaka 15 na 24 wako katika hatari ya kufanya ngono bila kijilinda.
” Serikali na mashirika ya vijana wanakatiwa kukaa pamoja na kujadili njia nzuri ambayo kundi hilo wanaweza kunufaika na uzazi wa majira sababu ni kundi ambalo liko katika hatari kubwa”, ni mtazamo wake mwandishi wa habari wa Burundi anayefuatilia kwa karibu habari kuhusu mpango wa uzazi wa majira .
Kwa mjibu wa katibu wa shirika la akinamama kwa ajili ya amani na usalama, vijana wa kike wanatakiwa kufikiwa na huduma ya uzazi wa majira kwa sababu ” wako katika hatari ya kufanya ngono bila kujikinga na kubakwa kutokana na sababu nyingi zikiwemo zile za umasikini”.
Anaomba wazazi kuendelea na jukumu lao kwa kuzungumza na watoto wao kuhusu swala la ngono na mila na desturi za warundi, jambo ambalo anawaomba pia waziri.
You might also like
Cholera in Nyanza : drinking water funds vanish, the population pays with their health
SOS Médias Burundi Nyanza, February 3, 2026 – For more than three years, cholera has remained a persistent threat in Burundi. Officially declared in January 2023, the epidemic continues to
Ruyigi : two cases of Mpox detected in the Nyankanda refugee camp
SOS Médias Burundi Ruyigi, October 6, 2025 – The apparent calm of the Congolese refugee camp of Nyankanda, located in the district of Ruyigi, in Buhumuza province, eastern Burundi, was
Bujumbura: mripuko wa maradhi ya kipindupindu
Takriban watu 17 walipatikana na ugongwa wa Kipindupindu katika tarafa ya Kinama (kaskazini mwa jiji la biashara la Bujumbura) kulingana na waakazi. Wanahakikisha kuwa watu wawili tayari walifariki dunia. Ni
