Burundi : Vijana ambao hawajafunga ndoa hawana ruhsa ya kutumia mipango ya uzazi wa majira (waziri wa afya)
Waziri wa afya Sylvie Nzeyimana alifahamisha hayo siku ya jumanne katika mji mkuu wa biashara Bujumbura. Ni kando ya kongamano kuu la akinamama viongozi.
Kwa mjibu wa waziri Nzeyimana, waliofunga ndoa peke ndio wanaohusishwa na mipango wa uzazi wa majira. HABARI ya SOS Medias Burundi
Akijibu swali wakati wa muelezo wake kando na mkutano mkuu wa akinamama viongozi, Daktari Sylvie Nzeyimana amesema hayo kwa dhahiri.
” Vijana wanatakiwa kufundishwa kuhusu afya ya uzazi. Hawawezi kufanya tendo la ndoa kwa sababu linafanywa na watu waliofunga ndoa peke” alibaini hayo waziri Nzeyimana kando na kongamano kuu la akinamama viongozi ijumanne hii.
Hata hivo amemuomba waziri wa elimu kuongeza mikutano ya kuhamasisha kuhusu uzazi wa majira mashuleni.
Kwa mjibu wa takwimu za serikali ya Burundi, asilimia 38 ya akinamama walijiunga na mpango wa uzazi wa majira katika nchi hii ndogo ya afrika mashariki.
Mashirika ya vijana wao wanafahamisha kuwa vijana kati ya miaka 15 na 24 wako katika hatari ya kufanya ngono bila kijilinda.
” Serikali na mashirika ya vijana wanakatiwa kukaa pamoja na kujadili njia nzuri ambayo kundi hilo wanaweza kunufaika na uzazi wa majira sababu ni kundi ambalo liko katika hatari kubwa”, ni mtazamo wake mwandishi wa habari wa Burundi anayefuatilia kwa karibu habari kuhusu mpango wa uzazi wa majira .
Kwa mjibu wa katibu wa shirika la akinamama kwa ajili ya amani na usalama, vijana wa kike wanatakiwa kufikiwa na huduma ya uzazi wa majira kwa sababu ” wako katika hatari ya kufanya ngono bila kujikinga na kubakwa kutokana na sababu nyingi zikiwemo zile za umasikini”.
Anaomba wazazi kuendelea na jukumu lao kwa kuzungumza na watoto wao kuhusu swala la ngono na mila na desturi za warundi, jambo ambalo anawaomba pia waziri.
You might also like
Bujumbura : Burundi government introduces a stabilization allowance for its doctors
The Burundian government, through the ministries in charge of Health and Finance, has taken a significant step to retain its health professionals. A joint order, signed on January 16, 2025,
Ngozi : suspension of free care at the Kiremba autonomous hospital
This measure is a very hard blow for children and pregnant women. It came after investigations carried out by the ministry in charge of health. The concerned health facility is
Bujumbura : health authorities declare the appearance of monkey pox
The Burundian Minister in charge of health announced Thursday the discovery of three cases of “monkey pox” in the commercial capital Bujumbura during this month of July. However, Dr. Lyduine
