Minembwe : kundi la Mai Mai limemuuwa mzee mmoja na kupora ng’ombe 150
Ndagara Buhimba (Miaka 80) aliuwawa siku ya jumatatu alasiri. Kundi la Mai Mai lilirejuhi pia watu 2 na kuiba ng’ombe 150. HABARI ya SOSMedias Burundi
Muhanga alikuwa katika malisho yaliyo katika eneo la Monyi wakati waasi wa Mai Mai waliopomuuwa kulinga na mashahidi.Ni katika kanda ya Minembwe wilaya ya Fizi katika mkoa wa Kivu ya kusini mashariki mwa DRC.
Kifo cha mzee huyo kutoka jamii ya Banyamulenge kinathibitishwa na familia yake.
” Asubuhi hii ndipo muili wake umepatikana.Ni vitendo vya kinyama vinavyofanyika hapa. Watu wanauwawa kama wanyama wanachinjwa”, amelalamika mkaazi mmoja.
Vyanzo sehemu hiyo vinahakikisha kuwa watu wengine wawili walijeruhiwa wakati wa shambulio hilo ‘a ng’ombe 150 kuibiwa.
Msemaji wa kundi la Mai Mai hakuwa karibu ili aweze kujieleza juu ya malalamiko hayo. Wakuu wa jeshi na viongozi tawala pia hawajasema lolote.
Siku ya jumapili, kijana mdogo aliuwawa kwa kukatwa na panga na askali wa jeshi la FARDC ( jeshi la jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo ) katika eneo hilo la Minembwe , kisa ambacho kilisababisha mandamano katika shule zote ijumatatu eneo la Minembwe.
Wakaazi wa eneo la Minembwe ambao wengi wao ni kutoka jamii ya Banyamulenge wanalituhumu jeshi la Kongo kutuwahami wakati wakilengwa na mashambulizi ya makundi ya silaha.
Ni tangu miaka mitano tukiuwawa bila hata hivo jeshi la FARDC kuingilia kati ili kutulinda wakati ambapo tuko raia wa Kongo ” analalamika diwani mmoja
You might also like
Kirundo: an Imbonerakure killed by his peers
A 41-year-old man was killed on Thursday morning on Rwimbogo hill, in the Rushubije zone in Ntega commune (Kirundo province, northern Burundi). The victim, an Imbonerakure (member of the CNDD-FDD
Burundi-DRC : Burundi sends other soldiers to Congo
According to the permanent secretary of the national security council, the second group of Burundian soldiers joined Congolese territory on Wednesday. At a time when the first group which went
Goma : several dead in a shipwreck
At least 28 people died in a shipwreck near Goma on Thursday in the province of North Kivu in eastern Congo, SOS Médias Burundi has learned. Local sources speak of
