Burundi: Kipindi cha jua kali chaikabili nchi, serikali inamulilia Mungu
Tangu septemba 2022 , takriban kwenye ardhi yote ya Burundi mvua haijanyesha. Kipindi cha kipwa kinarefuka, wananchi wako katika wasi wasi mkubwa na serikali anawaomba waumini kumulilia Mungu ili mvua ipatikane. HABARI SOS Medias Burundi
Wananchi katika mikoa ya Cibitoke (kaskazini-magharibi) wanapoteza matumaini kutokana na juwa kali.
” Hakuna hata tonya la mvua tangu septemba hadi sasa. Mashamba yote yamekauka. Baa la njaa lililokuwa linapiga hodi mlangoni kwa miezi, sasa linakuja kutukuta” , atahadharisha mkaazi mmoja wa Gihanga na Rugombo katika mikoa ya Bubanza na Cibitoke.Tarafa hizo mbili ni kati ya zile zenye mavuno mengi.
Mkoani Kirundo kaskazini, viongozi tawala wanafahamisha kuwa mkoa huo unakabiliwa na ukame mkubwa. Familia nyingi zinahofia kupata matatizo makubwa katika mkoa huo ambao zamani ulikuwa kama ghala la Burundi lakini unakabiliwa na ukame kwa miaka.
Mkoa wa Muramvya (kati kati) unaopakana na msitu wa Kibira unakabiliwa na hali kama hiyo kinyume na ilivyokuwa katika misimu mingine.
Kusini mashariki mwa nchi, ukame unakabili pia eneo hilo linalopakana na Tanzania na wakaazi wa eneo hilo wanalalamika kuwa wanakabiliwa na mtihani wa joto kali nyakati za usiku. Mikoa ya Bururi na Rumonge ( kusini magharibi) haikuepukika. Mikoa hiyo haijashuhudia mvua tangu septemba.
Kutokana na hali hiyo ya nchi, viongozi wanaomba viongozi wa kidini na waumini kumulilia Mungu ili mvua ipatikane.
[….] Ninawaomba kutoa maelekezo kwa wakuu wa tarafa, anza mawasiliano na viongozi wa dini/madhehebu/Parokia/Misikiti …..tangu kesho asubuhi na jumapili, wafanye maombi ya pamoja ili kumulilia Mungu mvua ipatikane nchini Burundi. Ni pia fursa kuwahamasisha wananchi kunyunyizia maji na/ kufanya umwagiliaji mahala pote inapowezekana ” , tunayasoma hayo katika ujumbe ulitumwa kwa ma gavana wa mikoa na meya wa jiji la kibiashara la Bujumbura siku ya ijumaa.
Vyanzo katika serikali ya Burundi wanalaani kuwa sera ya rais Ndayishimiye ya kuimarisha kilimo haitaweza kutekelezwa.
“Sera ya serikali ya kuweka kipau mbele kilimo imepata changamoto. Muongozo wa rais Neva kwamba ” Kila mdomo upate chakula na kila mfuko upate pesa hauwezekani”, walibaini.
Wananchi wa burundi wanaishi kwa kilimo na ufugaji. Ukame unaoikabili nchi ni pigo kubwa kwa taifa hilo la afrika ya kati.
Kawaida kipindi cha mvua kinachodumu miezi tisa, huanza na mwezi septemba na kumalizika katika mwezi mei, mwezi juni ukishuhudia mvua kwa kiwango kidogo. Mwaka huu hamna hata tonya la mvua lililoanguka tangu septemba iliyopita.
Katika mikoa mingi, magavana na ma askofu wa dini ya katolika, wametoa tangazo la kuwaalika waumini kufanya maombi maluum wekendi hii ili mvua iweze kurejea .
You might also like
Bukinanyana: more than two hundred houses destroyed by torrential rains
220 houses and 7 classrooms demolished, several hectares of fields damaged, suggests a report of the damage caused by torrential rains mixed with hail this Tuesday September 12 and Wednesday
Muyinga: moshi unaotokana na viripuzi vinavyotumiwa katika migodi ya dhahabu husababisha maradhi ya mapaafu na kifo
Wakaazi wa kijiji cha Kamaramagambo tarafani Butihinda mkoa wa Muyinga (kaskazini mashariki mwa Burundi) wanasema kuwa moshi unaoletwa na viripuzi vinavyotumiwa kuvunja mawe makubwa ndani ya migodi na kusababisha maradhi
Mugamba: torrential rains caused several damages
This Wednesday, rain mixed with a strong wind fell on the Tora market and its surroundings. It is in the Muramba zone in the Mugamba district (Bururi province, southern Burundi).
