Nyarugusu (Tanzania): Kampeni dhidi ya Malaria
Shirika la HCR kwa ushirikiano na serikali ya Tanzania imeandaa Kampeni ya kunyunyizia dawa katika majumba, maeneo ya maji taka yaliyoganda pamoja pia na maeneo ya wazi yaliyo karibu na makaazi ya watu ndani ya kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu. Badaye vyandarua vilivyonyunyiziwa dawa vitatolewa kulingana na duru kutoka HCR. Kwa mjibu wa vyanzo vyetu, ugonjwa wa malaria umeibuka ndani ya kambi ya Nyarugusu na katika nchi nzima ya Tanzania. Nchi hiyo imeimarisha vita dhidi ya ugonjwa huo katika maeneo ambayo yako hatarini yakiwemo makambi ya wakimbizi. HABARI SOS Médias Burundi
Kampeni ilianzia katika zone ya 12 na 13 ambako kulishuhudia visa vingi vya malaria na itaendelea katika maeneo mengine ya kambi ya Nyarugusu.
Kampeni hiyo inafanyika katika maeneo yanayoikaliwa na warundi kadhalika na wakongomani.
Hayo ni wakati vitanda vya hospitali vimezidiwa na idadi ya wagonjwa ndani ya kambi ya Nyarugusu. HCR na washirika wake wanataka kupunguza madhara.
” Wathiriwa zaidi ni watoto wa chini ya miaka mitano, akinamama wajawazito, pamoja pia watu wazima. Kuna waliokwisha fariki. Kwa hiyo tunatakiwa kuchukuwa hatua kwa wakati ili kukinga athari mbaya” alifahamisha afisa wa HCR.
Wakimbizi wanakaribisha kampeni hiyo. Wanatumia fursa hiyo kuomba HCR iwakabidhi vifaa vya usafi kama sabuni na vyombo vya kupikia ambapo kwa mjibu wao wamedumu navyo kwa miaka zaidi ya mitano.
Kambi ya Nyarugusu inaorodhesha wakimbizi zaidi ya laki moja na elfu 20 wakiwemo warundi elfu 49, huku wanaosalia wakiwa raia kutoka Kongo
You might also like
Musenyi : Congolese refugees welcome the easing of movement restrictions
SOS Médias Burundi Musenyi, February 2, 2026 – Congolese refugees living at the Musenyi site, located in the district of Musongati, in the province of Burunga, southeastern Burundi, have welcomed
Butezi : a second body found in the camp in a week
A body was found a few meters from the Nyankanda camp in the district of Butezi in the province of Ruyigi (eastern Burundi) on Sunday. It has not been identified.
Nyarugusu (Tanzania) : Massive repatriation of refugees resumes
More than 250 households were repatriated on Thursday, a first in over a year. Some refugees say that “we have no other choice”, blaming the untenable conditions in the Nyarugusu
