Minembwe: mwanajeshi mmoja na mchungaji waliuwawa kwa siku mbili
Mwanajeshi wa FARDC ( jeshi la jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo) aliuwawa jumatano hii asubuhi eneo la Minembwe. Ni katika wilaya ya Fizi mashariki mwa Kongo . Katika eneo hilo, mchungaji mmoja aliuwawa jumatatu, mauwaji yalidaiwa kufanywa na askali wa FARDC. HABARI SOS Médias Burundi
Mwanajeshi aliyeuwawa ni wa brigedia ya 12 ambayo inapiga kambi eneo la Minembwe. Kulingana na vyanzo vya kijeshi, watu wenye silaha waliopiga risasi wanadaiwa kuwa wapiganaji wa kundi la Twirwaneho linaloundwa na jamii ya Banyamulenge.
” Walimuuwa wakati akielekea kuchota maji katika mto wa Runandu”, wanasema askali wenzake.
Kifo cha mwanajeshi huyo kilisababisha taharuki katika kanda hiyo inayokaliwa na rai a wa Kongo wa jamii ya Banyamulenge, wanaofananishwa na makabila mengi na raia wa Rwanda.
” Wake wa askali jeshi walifanya mandamano. Wanasema kuwa wanataka kuwafukuza raia wa Rwanda watoke kwenye ardhi ya Kongo. Walipiga mawe kwenye maduka yanayomilikiwa na Banyamulenge kwenye kituo cha Madegu”, wanasema mashahidi.
Kisa hicho kilitokea baada ya mauwaji ya mchungaji mmoja wa jamii ya Banyamulenge ijumatatu.
Muzima Rugamba alikuwa katika kundi la watu wakati alipouwawa.
” Watu wengi walikuwa ndani ya nyumba kwenye kituo cha Madegu. Walikuwa wamejificha mvua. Wanajeshi walikuja na kuchukuliwa kila kitu walichokuwa nacho, simu za mkononi na pesa …..Kabla ya kwenda, walimupiga risasi mchungaji Muzima na kufariki papo hapo”, wanasema mashahidi.
Jeshi la Kongo lilifahamisha kuwa uchunguzi ulianzishwa kuhusu kesi hiyo. Kwa mjibu wa vyanzo vyetu, askali jeshi watatu waliouwa mtu huyo wa Mungu wanahudumu katika brigedia ya 12.
” Watuhumiwa walikamatwa” vyanzo vyetu katika taasisi za usalama vinasema.
Takriban raia 20 waliuwawa eneo la Minembwe tangu mwaka wa 2020, kumi kati yao wakiwa waliuwawa na wanajeshi kwa mjibu wa mashirika ya kiraia ya ndani.
Kisa kilichosababisha hasira nyingi ni kile cha kijana mwanafunzi aliyeuwawa kwa mapanga na askali jeshi mwanzoni mwa oktoba iliyopita.
Katika ukanda huo, ng’ombe laki tatu waliporwa na makundi ya silaha pamoja na FARDC tangu 2017 kwa mjibu wa viongozi wa wafugaji katika ukanda huo.
Msemaji wa kundi la silaha la Twirwaneho hakupatikana ili kujieleza kuhusu madai hayo.
You might also like
Minembwe : a soldier killed a young pupil with a machete
Mugaza Nganganyi, 16 years old, was killed on Sunday. It is a member of the FARDC (Armed Forces of the Democratic Republic of Congo) who assassinated him, according to his
Giheta : discovery of a body
The body of Jean Baraton Mizero, 34 years old, driver, was found on the morning of this Friday, March 17, 2023 in the Nyambeho valley, it is exactly in the
Bukinanyana : nearly thirty bodies wearing FARDC uniforms discovered in Kibira
At least 32 bodies of men wearing the uniform of the Congolese army, the FARDC (Armed Forces of the Democratic Republic of Congo) were discovered in the Kibira natural reserve,
