Ituri: watu takriban 30 wameuwawa eneo la Djugu
Shumbulio jingine la mauwaji lilifanywa na kundi la CODECO ( shirikisho kwa ajili ya maendeleo ya Kongo) katika wilaya ya Djugu Kijiji cha Bahema-Banywagi kwenye kitongoji cha Nyamamba wekendi hii. Mashirika ya ndani yanafahamisha kuwa waasi walifanya shambulio hilo kwenye mwambao wa ziwa Albert ambako waliwauwa watu 31, 24 kati ya hao waliuwawa katika kitongoji cha Nyamamba huku saba wengine wakiuwawa katika kitongoji cha Mbongi eneo la Lossandrema ndani ya Kijiji cha kaskazini-Bahema. HABARI SOS Médias Burundi
Mashirika ya kiraia ya ndani yanafahamisha kuwa watu wengine hawajulikani walipo tangu shambulio hilo kutokea siku ya jumamosi iliyopita.
Watetezi wa haki za binadamu wanalaani kuona hadi sasa jeshi bado halijaingilia kati.
SOSMedias Burundi ilijaribu kuwasiliana na msemaji wa operesheni za kijeshi wilayani Ituri bila mafanikio.
Kanda hiyo inakabiliwa na tishio la mashambulizi ya makundi ya silaha ya ndani na nje likiwemo kundi la CODECO ( Nguvu zilizoungana kwa ajili kidemokrasia). Tangu tarehe 8 januari 2023, angalau raia wa kawaida 66 waliuwawa katika wilaya ya Djugu na Irumu na Ituri kulingana na takwimu zetu.
Waliuwawa katika mashambulizi yanayodaiwa kufanywa na makundi mawili ya silaha licha ya hatua za kusitisha mapigano kufikiwa mwezi disemba mjini Nairobi (kenya) wakati wa awamu ya tatu ya mazungumzo kuhusu mzozo wa Kongo.
You might also like
Mahama : the killer hippopotamus strikes again, two Burundian refugees dead
SOS Médias Burundi Mahama (Rwanda), May 15, 2025 — Two Burundian refugees, a man in his sixties and a 22-year-old pupil, recently lost their lives in separate attacks perpetrated by
Bubanza : armed attack by rebels from the DRC in Buringa
Detonations of heavy and light weapons were heard Saturday evening in the Buringa zone, in Gihanga district, Bubanza province (western Burundi). The attackers reportedly came from Rukoko Park located along
South Kivu: General Nzabampema denies having been dislodged from his strategic positions
On Monday, the Burundian rebel leader denied reports that the Burundian and Congolese armies killed 40 of his fighters during recent fighting in South Kivu (Eastern DRC). He claims to
