Ituri: watu takriban 30 wameuwawa eneo la Djugu

Ituri: watu takriban 30 wameuwawa eneo la Djugu

Shumbulio jingine la mauwaji lilifanywa na kundi la CODECO ( shirikisho kwa ajili ya maendeleo ya Kongo) katika wilaya ya Djugu Kijiji cha Bahema-Banywagi kwenye kitongoji cha Nyamamba wekendi hii. Mashirika ya ndani yanafahamisha kuwa waasi walifanya shambulio hilo kwenye mwambao wa ziwa Albert ambako waliwauwa watu 31, 24 kati ya hao waliuwawa katika kitongoji cha Nyamamba huku saba wengine wakiuwawa katika kitongoji cha Mbongi eneo la Lossandrema ndani ya Kijiji cha kaskazini-Bahema. HABARI SOS Médias Burundi

Mashirika ya kiraia ya ndani yanafahamisha kuwa watu wengine hawajulikani walipo tangu shambulio hilo kutokea siku ya jumamosi iliyopita.

Watetezi wa haki za binadamu wanalaani kuona hadi sasa jeshi bado halijaingilia kati.

SOSMedias Burundi ilijaribu kuwasiliana na msemaji wa operesheni za kijeshi wilayani Ituri bila mafanikio.

Kanda hiyo inakabiliwa na tishio la mashambulizi ya makundi ya silaha ya ndani na nje likiwemo kundi la CODECO ( Nguvu zilizoungana kwa ajili kidemokrasia). Tangu tarehe 8 januari 2023, angalau raia wa kawaida 66 waliuwawa katika wilaya ya Djugu na Irumu na Ituri kulingana na takwimu zetu.

Waliuwawa katika mashambulizi yanayodaiwa kufanywa na makundi mawili ya silaha licha ya hatua za kusitisha mapigano kufikiwa mwezi disemba mjini Nairobi (kenya) wakati wa awamu ya tatu ya mazungumzo kuhusu mzozo wa Kongo.

Previous Musigati: wakaazi wahofia njaa
Next Bijombo: Twirwaneho fighters killed three FARDC soldiers

You might also like

Security

Ruyigi : a woman and a child injured with a machete in Kayongozi

Anne Nzeyimana was seriously injured with a machete on her face and both arms last Tuesday. The incident occured on the hill of Nkanda, in the Kayongozi zone, in the

Justice En

Rumonge : four Ugandans arrested

Cabura John, 24 years old, Balijuka Hillary Gahwa, 29 years old, Ajuna Robert, 26 years old, and Kasaija Enock, 23 years old, were arrested on Thursday. Their arrest took place

Human Rights

Ituri: zaidi ya wananchi 200 waliuwawa na waasi katika kipindi cha miezi miwili

Tangu mwanzo wa mwaka 2023, hali ya usalama inazidi kuwa ya wasi wasi na kusikitisha katika mkoa wa Ituri karibu miaka miwili tangu kuanzisha serikali ya kijeshi. Wananchi wa kawaida