Bijombo: wapiganaji wa kundi la Twirwaneho wamewauwa wanajeshi watatu wa FARDC

Bijombo: wapiganaji wa kundi la Twirwaneho wamewauwa wanajeshi watatu wa FARDC

Wanajeshi hao watatu waliuwawa katika mapigano kati ya jeshi la Kongo na kundi la silaha la Twirwaneho linaloundwa na vijana wa jamii ya Banyamulenge, jumanne hii. HABARI SOS Médias Burundi

Kwa mjibu wa vyanzo vya ndani, mapigano makali yalifanyika jumanne hii asubuhi kati ya wapiganaji wa kundi la Twirwaneho na wanajeshi wa FARDC ( jeshi la jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo). Makabiliano yaliripotiwa katika kitongoji cha Bijombo ndani ya wilaya ya Uvira mkoa wa Kivu ya kusini mashariki mwa DRC.

” Mapigano makali yalifanyika hususan katika maeneo ya kanyaga na Irango. Maeneo hayo tuliwauwa wanajeshi watatu. Wawili wengine waliuwawa siku ya jumatatu” vyanzo vya karibu na kundi la Twirwaneho vinasema.

Msemaji wa jeshi la FARDC halipatikana kwenye simu ili kujieleza juu ya madai hayo.

Lakini wakaazi walituhumu wanajeshi wa FARDC kufanya uporaji katika maeneo walikopita baada ya kushindwa nguvu na wapiganaji wa jamii ya Banyamulenge.

Mapigano hayo yalifanyika baada ya jeshi la FARDC na FDNB ( jeshi la Burundi) kuwakamata watu watano wakiwemo raia wawili wa Burundi waliokuwa wakipeleka misaada ya vyakula kundi la Twirwaneho siku ya jumamosi iliyopita.

Wadadisi wanasema kuwa kanali Michel Makanika kamanda wa kundi la silaha la Twirwaneho anafahamu vizuri eneo hilo na wapiganaji wake wako kama nyoka ambao wako katika mashimu yao binafsi.

Previous Bujumbura: police killed three suspected thieves
Next Cibitoke: miili mingine imepatikana tarafani Rugombo

You might also like

Security

Minembwe: jeshi la Kongo na kundi la Twirwaneho walipoteza watu 11

FARDC (jeshi la jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo) na kundi la silaha la Twirwaneho walipigana siku ya alhamisi. Mapigano yalifanyika katika maeneo mbali mbali ya Minembwe, eneo linalokaliwa na wajumbe

Human Rights

Cibitoke : a zone chief and a local intelligence official accused of illegal money collection

Residents of the Ruziba zone, in the Mugina district and those of the Murwi district in the Cibitoke province (northwest Burundi) say they are tired of the abuse of authority

DRC En

Goma : several dead and injured in anti-Monusco demonstrations and against the EAC regional force

Several people were killed on Wednesday in the city of Goma, capital of North Kivu in the east of the DRC in demonstrations organized by a mystical-religious sect. According to