Bijombo: wapiganaji wa kundi la Twirwaneho wamewauwa wanajeshi watatu wa FARDC

Bijombo: wapiganaji wa kundi la Twirwaneho wamewauwa wanajeshi watatu wa FARDC

Wanajeshi hao watatu waliuwawa katika mapigano kati ya jeshi la Kongo na kundi la silaha la Twirwaneho linaloundwa na vijana wa jamii ya Banyamulenge, jumanne hii. HABARI SOS Médias Burundi

Kwa mjibu wa vyanzo vya ndani, mapigano makali yalifanyika jumanne hii asubuhi kati ya wapiganaji wa kundi la Twirwaneho na wanajeshi wa FARDC ( jeshi la jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo). Makabiliano yaliripotiwa katika kitongoji cha Bijombo ndani ya wilaya ya Uvira mkoa wa Kivu ya kusini mashariki mwa DRC.

” Mapigano makali yalifanyika hususan katika maeneo ya kanyaga na Irango. Maeneo hayo tuliwauwa wanajeshi watatu. Wawili wengine waliuwawa siku ya jumatatu” vyanzo vya karibu na kundi la Twirwaneho vinasema.

Msemaji wa jeshi la FARDC halipatikana kwenye simu ili kujieleza juu ya madai hayo.

Lakini wakaazi walituhumu wanajeshi wa FARDC kufanya uporaji katika maeneo walikopita baada ya kushindwa nguvu na wapiganaji wa jamii ya Banyamulenge.

Mapigano hayo yalifanyika baada ya jeshi la FARDC na FDNB ( jeshi la Burundi) kuwakamata watu watano wakiwemo raia wawili wa Burundi waliokuwa wakipeleka misaada ya vyakula kundi la Twirwaneho siku ya jumamosi iliyopita.

Wadadisi wanasema kuwa kanali Michel Makanika kamanda wa kundi la silaha la Twirwaneho anafahamu vizuri eneo hilo na wapiganaji wake wako kama nyoka ambao wako katika mashimu yao binafsi.

Previous Bujumbura: police killed three suspected thieves
Next Cibitoke: miili mingine imepatikana tarafani Rugombo

You might also like

Politic

Cibitoke : Burundian soldiers injured in the DRC hospitalized in the provincial military camp

Many wounded Burundian soldiers were repatriated via the river Rusizi, bordering the DRC, on the 6th Avenue, Kaburantwa village, in the district of Buganda in the province of Cibitoke (northwest

Security

North Kivu : timid demonstration against President Macron’s arrival in the DRC

A demonstration has been organized in Goma this Thursday since the morning hours. Citizen movements and pressure groups are protesting against the arrival of French President Emmanuel Macron in the

Security

Cibitoke : 15 Congolese drowned in the Rusizi while trying to flee fighting in the DRC

While clashes between the M23 and the Congolese army intensify in South Kivu, refugees are trying to flee to Burundi. In less than 48 hours, 15 people have lost their