Bijombo: wapiganaji wa kundi la Twirwaneho wamewauwa wanajeshi watatu wa FARDC
Wanajeshi hao watatu waliuwawa katika mapigano kati ya jeshi la Kongo na kundi la silaha la Twirwaneho linaloundwa na vijana wa jamii ya Banyamulenge, jumanne hii. HABARI SOS Médias Burundi
Kwa mjibu wa vyanzo vya ndani, mapigano makali yalifanyika jumanne hii asubuhi kati ya wapiganaji wa kundi la Twirwaneho na wanajeshi wa FARDC ( jeshi la jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo). Makabiliano yaliripotiwa katika kitongoji cha Bijombo ndani ya wilaya ya Uvira mkoa wa Kivu ya kusini mashariki mwa DRC.
” Mapigano makali yalifanyika hususan katika maeneo ya kanyaga na Irango. Maeneo hayo tuliwauwa wanajeshi watatu. Wawili wengine waliuwawa siku ya jumatatu” vyanzo vya karibu na kundi la Twirwaneho vinasema.
Msemaji wa jeshi la FARDC halipatikana kwenye simu ili kujieleza juu ya madai hayo.
Lakini wakaazi walituhumu wanajeshi wa FARDC kufanya uporaji katika maeneo walikopita baada ya kushindwa nguvu na wapiganaji wa jamii ya Banyamulenge.
Mapigano hayo yalifanyika baada ya jeshi la FARDC na FDNB ( jeshi la Burundi) kuwakamata watu watano wakiwemo raia wawili wa Burundi waliokuwa wakipeleka misaada ya vyakula kundi la Twirwaneho siku ya jumamosi iliyopita.
Wadadisi wanasema kuwa kanali Michel Makanika kamanda wa kundi la silaha la Twirwaneho anafahamu vizuri eneo hilo na wapiganaji wake wako kama nyoka ambao wako katika mashimu yao binafsi.
You might also like
Goma: wandishi wa habari kusimamishwa wakati wakiripoti juu ya mandamano dhidi ya kikosi cha EAC
Hali ya taharuki imeripotiwa katika mji wa Goma mkoa wa Kivu kaskazini mashariki mwa DRC kufuatia mandamano dhidi ya kikosi cha EAC jumatano hii. Askali polisi pamoja na wanajeshi wametumia
Gasorwe : a CNL member kidnapped
Viateur Nzigo, member of the CNL party (National Congress for Freedom) was kidnapped from his home in the district of Gasorwe in Muyinga province (northeastern Burundi) on the morning of
Gitega : a secondary school teacher found dead, clubbed to death
Gérard Mbazumutima, 47 years old, a historian by training and teacher at Sainte Thérèse de Mushasha secondary school in Gitega (political capital) was killed with clubs by people not yet
