Nduta (Tanzania) : kijana mkimbizi kutoka Burundi alipatikana akiwa maiti baada ya kukosekana
Mélance Kwizera mwenye umri wa miaka karibu 20 alipotea wiki moja iliyopita. Alipatikana akiwa maiti karibu na kambi na kuzikwa haraka na jamii ya eneo hilo. Wakimbizi wanaomba uchunguzi ufanyike. HABARI SOS Médias Burundi
Marafiki na majirani wa kijana huyo wanasema kuwa walimuona mara ya mwisho mwanzoni mwa wiki iliyopita.
” Wakati tulipomuona, alikuwa akitoka nje ya kambi akivalia sera za vuguvuga la wa scout. Alikuwa na mazoea ya kutoka kwenda kushiriki katika maombi pamoja na shughuli za kundi la scout. Lakini siku hiyo, huenda alitoka kwa ajili ya shughuli zingine au kwa ajili ya kutafuta kuni za kupikia. Tangu siku hiyo hakurudi”, wanasikitika.
Habari hiyo mbaya ilianza kusambaa ndani ya kambi jumatatu jioni.
” Watanzania walituarifu kuwa kijana wa vuguvugu la scout alipatikana akiwa amefariki karibu ya kambi. Wakati tulipoona picha, tulimufahamu. Alikuwa Mélance Kwizera. Walituonyesha mahali alipozikwa haraka ili kuepusha muili wake kuharibika “, marafiki zake wanaeleza.
Wakimbizi wanadai kuwa kisa hicho kinachoongeza idadi ya mauwaji mengine, visa vya watu kutekwa na kupotezwa kinaachiria kuwa uhusiano kati ya wakimbizi na jamii iliyowapokea sio mzuri hata kidogo.
Familia ya muhanga pamoja viongozi wa kundi la scout ndani ya kambi ya Nduta wanaomba uchunguzi wa kina wa polisi ufanyike kwa ajili ya kuonyesha mazingira ya mauwaji hayo.
Wakimbizi wanalaani visa vya mauwaji ya kawaida na ya kuvizia pamoja na watu kupotezwa ambavyo vimerudi kushuhudiwa ndani ya kambi hiyo inayowapa hifadhi wakimbizi kutoka Burundi zaidi ya elfu 76. Wakimbizi wawili wenye asili ya Burundi waliuwawa na wananchi wa Tanzania tarehe 14 februari iliyopita karibu na kambi ya Nduta wakiwatuhumu kuwabaka wanawake wa Tanzania waliokuwa wakitafuta kuni na wengine waliokuwa wakielekea shambani. Polisi eneo hilo ilifahamisha hayo na kudai kuwa kati ya wakimbizi 12 na 16 huuwawa kila mwaka nje ya kambi nchini Tanzania.
Wiki hii, wajumbe wa polisi kwa ushirikiano na viongozi wa kambi ya Nduta walizidisha mikutano ya kuhamasisha kuhusu ujirani mzuri kati ya wakimbizi na jamii iliyowapokea.
You might also like
Nyarugusu : yafungwa maduka ya dawa yasiyojulikana
Uwindaji wa wamiliki wa maduka ya dawa yasiyokuwa halali ulianzishwa ndani ya Nyarugusu. Shirika la Medical Team International linalohusika na sekta ya afya lina mpango wa kukataza tabia ya kujitibu
Rumonge : three young men sentenced to a life jail for the rape and murder of a minor
SOS Médias Burundi Rumonge, February 18, 2026 – Three young men were sentenced on Wednesday to life imprisonment by the Rumonge First Court in Burunga Province (southern Burundi) for the
Bujumbura : nearly 800 Congolese police and military personnel have fled to Burundi
At least 532 Congolese police officers fleeing clashes between the M23 and the Congolese army and its allies have already been officially listed by Burundian services. They are hosted in
