Nduta (Tanzania) : kijana mkimbizi kutoka Burundi alipatikana akiwa maiti baada ya kukosekana

Nduta (Tanzania) : kijana mkimbizi kutoka Burundi alipatikana akiwa maiti baada ya kukosekana

Mélance Kwizera mwenye umri wa miaka karibu 20 alipotea wiki moja iliyopita. Alipatikana akiwa maiti karibu na kambi na kuzikwa haraka na jamii ya eneo hilo. Wakimbizi wanaomba uchunguzi ufanyike. HABARI SOS Médias Burundi

Marafiki na majirani wa kijana huyo wanasema kuwa walimuona mara ya mwisho mwanzoni mwa wiki iliyopita.

” Wakati tulipomuona, alikuwa akitoka nje ya kambi akivalia sera za vuguvuga la wa scout. Alikuwa na mazoea ya kutoka kwenda kushiriki katika maombi pamoja na shughuli za kundi la scout. Lakini siku hiyo, huenda alitoka kwa ajili ya shughuli zingine au kwa ajili ya kutafuta kuni za kupikia. Tangu siku hiyo hakurudi”, wanasikitika.

Habari hiyo mbaya ilianza kusambaa ndani ya kambi jumatatu jioni.

” Watanzania walituarifu kuwa kijana wa vuguvugu la scout alipatikana akiwa amefariki karibu ya kambi. Wakati tulipoona picha, tulimufahamu. Alikuwa Mélance Kwizera. Walituonyesha mahali alipozikwa haraka ili kuepusha muili wake kuharibika “, marafiki zake wanaeleza.

Wakimbizi wanadai kuwa kisa hicho kinachoongeza idadi ya mauwaji mengine, visa vya watu kutekwa na kupotezwa kinaachiria kuwa uhusiano kati ya wakimbizi na jamii iliyowapokea sio mzuri hata kidogo.

Familia ya muhanga pamoja viongozi wa kundi la scout ndani ya kambi ya Nduta wanaomba uchunguzi wa kina wa polisi ufanyike kwa ajili ya kuonyesha mazingira ya mauwaji hayo.

Wakimbizi wanalaani visa vya mauwaji ya kawaida na ya kuvizia pamoja na watu kupotezwa ambavyo vimerudi kushuhudiwa ndani ya kambi hiyo inayowapa hifadhi wakimbizi kutoka Burundi zaidi ya elfu 76. Wakimbizi wawili wenye asili ya Burundi waliuwawa na wananchi wa Tanzania tarehe 14 februari iliyopita karibu na kambi ya Nduta wakiwatuhumu kuwabaka wanawake wa Tanzania waliokuwa wakitafuta kuni na wengine waliokuwa wakielekea shambani. Polisi eneo hilo ilifahamisha hayo na kudai kuwa kati ya wakimbizi 12 na 16 huuwawa kila mwaka nje ya kambi nchini Tanzania.

Wiki hii, wajumbe wa polisi kwa ushirikiano na viongozi wa kambi ya Nduta walizidisha mikutano ya kuhamasisha kuhusu ujirani mzuri kati ya wakimbizi na jamii iliyowapokea.

Previous Masisi : mapigano mapya kati ya FARDC na M23
Next Uvira: another more than 300 Burundians find refuge in DRC

You might also like

Security

Mahama (Rwanda) : the assassination of at least eight Burundian refugees creates psychosis

Criminality has increased over the past two weeks in the Mahama refugee camp, housing Burundians and Congolese in eastern Rwanda. The most targeted are Burundians while Congolese are singled out

Refugees

Mahama (Rwanda) : a bandit arrested

A young Burundian man was caught red-handed stealing from his compatriot. Seriously injured, he was arrested by the police. INFO SOS Médias Burundi The incident occurred on Wednesday night in

Refugees

Pregnant women in danger : the nurses’ strike already leaves four dead

SOS Médias Burundi, Dzaleka, August 27, 2025 – The Dzaleka refugee camp in Malawi is experiencing a serious health crisis. For two weeks, medical staff at the camp hospital have