Rwanda-Burundi: Burundi yatangaza kufungua upya mipaka yake na Rwanda
Ni waziri wa Burundi wa ushirikiano wa kimataifa aliyetangaza hatua siku ya jumanne. Albert Shingiro hata hivyo alikariri nia ya serikali ya Burundi ya kuona Kigali inawafurusha wanamapinduzi inayowahudumia tangu 2015 kwa mjibu wa viongozi tawala nchini Burundi. HABARI SOS Médias Burundi
Waziri Shingiro alitangaza hayo katika jiji kuu la kibiashara Bujumbura kando na mkutano na wandishi wa habari ambapo alitoa ripoti ya yalitokekelezwa na wizara anayoiongoza kati ya julai na septemba iliyopita.
“Tulifungua mipaka yetu na Rwanda lakini hautajaacha sharti letu kuwa wanamapinduzi wanaohifadhiwa na kuwepa chakula na Kigali wanatakiwa kuletwa nchini Burundi […..], tunafikiria kuwa Rwanda, nchi rafiki haitachukuwa ujirani mwema, urafiki na ushirikiano na nchi yetu na kulipiza kwa kuwahudumia wanamapinduzi hao mjini Kigali ” alifahamisha Bwana Shingiro.
Anawachukulia wanamapinduzi hao kama “wageni wanaleta wasi wasi ” .
” Wanamapinduzi ni wageni wanaleta shida kwa serikali ya Rwanda. Nchi hiyo inatakiwa kutafuta mbinu za kumalizana wao”, alizidi kusema mwanadiplomasia huyo mkuu wa Burundi.
Wanamapinduzi wanaosemekana hapa, walijaribu kuipindua serikali ya hayati rais Pierre Nkurunziza mwezi mei mwaka wa 2015. Muhula wake wa mwisho uliyoleta utata ulifagombaniwa kinyume cha sheria, mahakama ya EAC ilitoa hukumu hiyo.
Mipaka kati ya Burundi na Rwanda imefungwa kwa kipindi cha miaka takriban sita. Hali hiyo ikachochewa na janga la COVID-19.
Kigali upande wake ilifungua mipaka yake na Burundi miezi kadhaa iliyopita.
About author
You might also like
Crisis in Eastern Congo : Rwanda and Tanzania receive more than 8,000 new Congolese refugees
In Rwanda, the UNHCR, which gives the figures, explains that humanitarian needs are multiplying as the number of Congolese fleeing to Rwanda in search of safety continues to increase. They
Bujumbura : chama cha CNL chazuiliwa kuadhimisha kumbukumbu ya miaka minne
Waziri wa mambo ya ndani na usalama aliamuru kupiga marufuku sherehe za maadhimisho ya miaka minne ya uhai wa chama cha CNL na zile za kutakiana rheli za mwaka mpya
Burundi : President Neva’s speech to reinforce the acts of violence of Imbonerakure, according to Carina Tertsakian
President Évariste Ndayishimiye praised on Saturday August 26, 2023, the role of the Imbonerakure in the night patrols and securing the borders. According to Carina Tertsakian, associate researcher at the