Rwanda-Burundi: Burundi yatangaza kufungua upya mipaka yake na Rwanda
Ni waziri wa Burundi wa ushirikiano wa kimataifa aliyetangaza hatua siku ya jumanne. Albert Shingiro hata hivyo alikariri nia ya serikali ya Burundi ya kuona Kigali inawafurusha wanamapinduzi inayowahudumia tangu 2015 kwa mjibu wa viongozi tawala nchini Burundi. HABARI SOS Médias Burundi
Waziri Shingiro alitangaza hayo katika jiji kuu la kibiashara Bujumbura kando na mkutano na wandishi wa habari ambapo alitoa ripoti ya yalitokekelezwa na wizara anayoiongoza kati ya julai na septemba iliyopita.
“Tulifungua mipaka yetu na Rwanda lakini hautajaacha sharti letu kuwa wanamapinduzi wanaohifadhiwa na kuwepa chakula na Kigali wanatakiwa kuletwa nchini Burundi […..], tunafikiria kuwa Rwanda, nchi rafiki haitachukuwa ujirani mwema, urafiki na ushirikiano na nchi yetu na kulipiza kwa kuwahudumia wanamapinduzi hao mjini Kigali ” alifahamisha Bwana Shingiro.
Anawachukulia wanamapinduzi hao kama “wageni wanaleta wasi wasi ” .
” Wanamapinduzi ni wageni wanaleta shida kwa serikali ya Rwanda. Nchi hiyo inatakiwa kutafuta mbinu za kumalizana wao”, alizidi kusema mwanadiplomasia huyo mkuu wa Burundi.
Wanamapinduzi wanaosemekana hapa, walijaribu kuipindua serikali ya hayati rais Pierre Nkurunziza mwezi mei mwaka wa 2015. Muhula wake wa mwisho uliyoleta utata ulifagombaniwa kinyume cha sheria, mahakama ya EAC ilitoa hukumu hiyo.
Mipaka kati ya Burundi na Rwanda imefungwa kwa kipindi cha miaka takriban sita. Hali hiyo ikachochewa na janga la COVID-19.
Kigali upande wake ilifungua mipaka yake na Burundi miezi kadhaa iliyopita.
You might also like
Rwanda-Burundi : games to strengthen police cooperation
Rwanda hosts regional competitions of the Eastern Africa Police Chiefs Cooperation Organization, EAPCCO. At the launch of the games, a Burundian police team crossed swords with that of Rwandan police.
Goma: large-scale protests
The city of Goma (capital of North Kivu, eastern DRC) woke up in great tension on Monday morning following a protest against the regional force of the EAC. The protesters
Burundi: 5 women’s organizations ask President Ndayishimiye to free eight activists, including six women
Five Burundian women’s organizations in exile demanded the Burundian president to release human rights defenders. In their letter, they say the persons concerned are illegally detained in reference to United
