Kivu-kaskazini : Mpatanishi Kenyatta ziarani eneo la vita
Katika shabaha ya jukumu lake alilopewa na jumuiya ya afrika mashariki, rais huyo mstaafu wa Kenya Uhuru Kenyatta jumanne hii amekuwa mjini Goma makao makuu ya mkoa wa Kivu-kaskazini mashariki mwa DRC. Katika ziara hiyo alijipa jukumu la kuwafariji wakimbizi wa vita waliokimbia ujio wa M23 katika eneo la Rutshuru. HABARI SOS Médias Burundi
Uhuru Kenyatta alipokelewa na gavana mwanajeshi wa Kivu-kaskazini luteni jemedali Constant Ndima na kamati yake ya usalama. Wote kwa pamoja walijielekeza kwenye kambi ya wakimbizi wa ndani ya Kanyaruchinya katika wilaya ya Nyiragongo ambayo inawapa hifadhi wakimbizi wa vita laki mbili waliotoroka ujio wa waasi wa M23 inayodhibiti eneo kubwa la Rutshuru.
Katika mkutano na wandishi wa habari, Bwana Kenyatta alisema kuwa anahofia janga la kibinadamu kutokea katika eneo la Nyiragongo ambako kuna ma mia ya wakimbizi.
” Kile nilichoona Goma na maeneo yake ya karibu kinasikitisha. Ni janga la kibinadamu linaloweza kutokea iwapo hakuna kitakachofanyika ” amebaini.
Uhuru Kenyatta aliyechaguliwa mwezi juni na marais wenzake kuwa mpatanishi katika mzozo nchini Kongo, aliwasili mjini Kinshasa (makao makuu ya DRC) jumamosi iliyopita. Tayari alikutana na ma wakuu wa mabaraza mawili ya bunge na seneti vya Kongo na wajumbe wa jamii zenye asili ya mikoa ya Kivu-kaskazini, kivu-kusini na Ituri pamoja pia na wawakilishi wa nchi zao.
Upande wa Kongo ulikariri daima tuhuma zake dhidi ya Rwanda ambayo wanasema kuwa inaunga mkono M23 madai rais wa Paul Kagame kwa mara nyingine wekendi iliyopita aliyakanusha akiwa katika mkutano na shirika la “Unity club ” jukwa la viongozi wa Rwanda lililoanzishwa na mke wa rais Jeanette Kagame.
You might also like
Rumonge : four Ugandans arrested
Cabura John, 24 years old, Balijuka Hillary Gahwa, 29 years old, Ajuna Robert, 26 years old, and Kasaija Enock, 23 years old, were arrested on Thursday. Their arrest took place
Makamba : taxi drivers on strike against untimely police fines
Drivers of so-called probox transport vehicles have been on strike since Monday. They are protesting against untimely fines imposed on them. They are either accused of improper loading or exceeding
Gitega: a body of a sixty-year-old discovered
The body of Félicité Mvuyekure was discovered on Saturday in the village of Mirama. It is in the district and province of Gitega (central Burundi). A woman suspected of having
