Gitega: wapinzani wawili wazuiliwa jela kwa zaidi ya mwezi

Gitega: wapinzani wawili wazuiliwa jela kwa zaidi ya mwezi

Wafuasi wawili wa chama cha CNL wa tarafa ya Bugendana mkoa wa Gitega (kati kati ya Burundi) wanazuiliwa jela kwa zaidi ya mwezi mmoja. Wanatuhumiwa kumubaka na kumuuwa mwanamke mmoja. Watuhumiwa wanakanusha madai hayo. Chama chao kinaomba waachiliwe huru. HABARI SOS Médias Burundi

Jonas Nsabimana na Jacques Habonimana, wawili hao wote wafuasi wa chama cha CNL walikamatwa tarehe 12 oktoba iliyopita nyumbani kwao. Walikamatwa na polisi.

Kisa hicho kilitokea katika kijiji cha Nyakeru tarafa ya Bugendana mkoa wa Gitega. Hayo ni baada ya kupatikana kwa muili wa Domine Ngendakumana mwenye umri wa miaka 37 mama wa watoto wawili.
Habari hiyo inathibitishwa na Epimac Mugisha kiongozi wa chama cha CNL tarafani Bugendana ambaye anazidi kuwa muathiriwa huyo aliuwawa baada ya kubakwa. Anatuhumu lakini kijana Imbonerakure ambaye alichangia kinywaji na muhanga huyo katika siku ya kuuwawa kwake.

Domine Ngendakumana na mfuasi huyo wa tawi la vijana wafuasi wa CNDD-FDD walitoka katika mgahawa huo wakiwa pamoja na kuelekea eneo moja, alisema.

Bwana Mugisha anahakikisha kuwa wafuasi hao wawili wa chama cha CNL hawana hatia.

” Walikamatwa kwa ushawishi wa mkuu wa kijiji cha Nyakeru kutokana na kuwa ni wafuasi wa CNL” anazidi kusema.
Anaomba waachiliwe huru.

Mkuu wa kijiji cha Nyakeru Juvenal Butoyi anakanusha madai hayo dhidi yake na kuongeza kuwa wapinzani hao walisimamishwa kwa ajili ya uchunguzi unaoendelea.

Wafuasi hao wawili wa chama kikuu cha upinzani wanazuiliwa kwa sasa ndani ya gereza kuu la Gitega (jiji kuu la kisiasa)

Previous Ituri and North Kivu: at least 18 civilians killed since Sunday
Next Burundi: makamu wa rais anathibitisha uwepo wa uhusiano mbaya kati ya viongozi wa nchi na wandishi wa habari

You might also like

Security

Mugina: Leaflets calling for the lynching of alleged witches

For two weeks, leaflets have been circulating in the commune of Mugina, in the province of Cibitoke (north-west Burundi), inciting violence against people accused of witchcraft. Faced with this alarming

Politic

Electoral violence : the Minister of the Interior acknowledges the involvement of members of the CNDD-FDD

SOS Médias Burundi Bujumbura, June 3, 2025 – Two days before the legislative and district elections, the Burundian Minister of the Interior acknowledged that members of the ruling CNDD-FDD party

Politic

Mitakataka : Manassé Nzobonimpa admits to having erased symbols of the Frodebu party

Manassé Nzobonimpa says he ordered the erasure of the symbols of the Sahwanya Frodebu party in the Mitakataka zone in the district and province of Bubanza (western Burundi). Former member