Gitega: wapinzani wawili wazuiliwa jela kwa zaidi ya mwezi
Wafuasi wawili wa chama cha CNL wa tarafa ya Bugendana mkoa wa Gitega (kati kati ya Burundi) wanazuiliwa jela kwa zaidi ya mwezi mmoja. Wanatuhumiwa kumubaka na kumuuwa mwanamke mmoja. Watuhumiwa wanakanusha madai hayo. Chama chao kinaomba waachiliwe huru. HABARI SOS Médias Burundi
Jonas Nsabimana na Jacques Habonimana, wawili hao wote wafuasi wa chama cha CNL walikamatwa tarehe 12 oktoba iliyopita nyumbani kwao. Walikamatwa na polisi.
Kisa hicho kilitokea katika kijiji cha Nyakeru tarafa ya Bugendana mkoa wa Gitega. Hayo ni baada ya kupatikana kwa muili wa Domine Ngendakumana mwenye umri wa miaka 37 mama wa watoto wawili.
Habari hiyo inathibitishwa na Epimac Mugisha kiongozi wa chama cha CNL tarafani Bugendana ambaye anazidi kuwa muathiriwa huyo aliuwawa baada ya kubakwa. Anatuhumu lakini kijana Imbonerakure ambaye alichangia kinywaji na muhanga huyo katika siku ya kuuwawa kwake.
Domine Ngendakumana na mfuasi huyo wa tawi la vijana wafuasi wa CNDD-FDD walitoka katika mgahawa huo wakiwa pamoja na kuelekea eneo moja, alisema.
Bwana Mugisha anahakikisha kuwa wafuasi hao wawili wa chama cha CNL hawana hatia.
” Walikamatwa kwa ushawishi wa mkuu wa kijiji cha Nyakeru kutokana na kuwa ni wafuasi wa CNL” anazidi kusema.
Anaomba waachiliwe huru.
Mkuu wa kijiji cha Nyakeru Juvenal Butoyi anakanusha madai hayo dhidi yake na kuongeza kuwa wapinzani hao walisimamishwa kwa ajili ya uchunguzi unaoendelea.
Wafuasi hao wawili wa chama kikuu cha upinzani wanazuiliwa kwa sasa ndani ya gereza kuu la Gitega (jiji kuu la kisiasa)
You might also like
Kayanza: forced contributions requested by the CNDD-FDD party
In Kayanza province in northern Burundi, the population is forced to contribute by force to the fundraising campaign of the presidential party for legislative election due in 2025. Each household
Goma (electoral campaign) : Moïse Katumbi promises a special fund of five billion dollars to pacify North Kivu and Ituri
Moïse Katumbi continues his electoral campaign. After the province of Ituri, Moïse Katumbi and his allies Matata Ponyo and Seth Kikuni arrived this Thursday in the city of Goma, capital
Kivu-kaskazini : mandamano dhidi ya ziara ya rais Macron nchini DRC yanafahamisha bila ushawishi mkubwa
Mandamano hayo yaliandaliwa alhamisi hii mjini Goma tangu asubuhi. Makundi ya ushawishi pamoja vuguvugu la wananchi yanapinga ujio wa rais wa ufaransa Emmanuel Macron nchini Jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo.
