Nduta (Tanzania): mashirika mengi ya misaada yanapanga kusimamisha shughuli zao
Angalau mashirika makuu manne ya misaada yatasimamisha huduma zake kuanzia januari mwaka wa 2023. Yatasimamisha huduma kutokana na ukosefu wa fedha. HABARI SOS Médias Burundi
Mashirika ya misaada ambayo tayari yalifahamisha kuwa yatasimamisha huduma ni pamoja na Women’s Legal Aid Center ( WILAC) inayojihusisha na sekta ya sheria, PLAN International inayosaidia watoto wa chini ya miaka 18, HelpAge International inayojihusisha na watu wazima na walemavu na IRC inayoshughulikia unyanyasaji dhidi ya akinamama.
” Mashirika hayo hayatatoa tena huduma hapa kambini. Msiwe na wasi wasi, huduma na misaada iliyokuwa inatolewa na mashirika hayo, itatolewa na shirika jingine la Danish Refugee Council (DRC). Ni kama kupishana, hakuna kitakachobadilika”, alihakikisha mfanyakazi wa HCR ambayo inahusika na uratibu wa mashirika hayo kabla ya kufafanua kuwa ukosefu wa fedha ndio sababu ya kusimamisha shughuli.
Hata hivyo wakimbizi wanahofia madhara ya hatua hiyo.
” Vipi huduma zilizokuwa zikitolewa na mashirika manne na zitakuwa zikitolewa na shirika moja ?Ni jambo la kawaida kuwa ubora wa huduma utapungua. Harafu ni mashirika muhimu yanayofunga milango”, analalamila mkimbizi kutoka Burundi, akihofia vifo kutokea mnamo siku zijazo.
Usitishwaji wa huduma umepokelewa vibaya.
“Tumetelekezwa. Ni pia ni ujumbe mzito ambao tunapewa na Tanzania na HCR. Wanataka turudi nyumbani kwa hali zote. Na hayo ni baada ya ziara ya viongozi wa Burundi hapa”, aliendelea mkimbizi huyo kwa hasira.
Wanaomba HCR “kutoanguka katika mtego wa Burundi na Tanzania” , kinyume chake, “HCR itakubali matokeo”
Haijajulikana iwapo mashirika hayo yatasimamisha shughuli katika kambi ya Nyarugusu.
Tanzania ina jumla ya wakimbizi 126.000 kutoka Burundi
You might also like
World Refugee Day 2026 : between despair, pressure to return, and a protracted humanitarian crisis in the camps
From Nyarugusu to Kakuma, via Mahama, Nakivale, Meheba, Lusenda, and the reception sites in Burundi, Burundian and Congolese refugees are experiencing a World Refugee Day marked by reduced humanitarian assistance,
Nduta (Tanzania) : acute lack of blood bags in the midst of a malaria crisis
Blood bags are lacking in the health facilities of Nduta camp in Tanzania. The main cause is the withdrawal of blood donors due to poor feeding conditions. Hospitals worry as
Dzaleka (Malawi): reopening of schools delayed due to increase in cholera cases
Malawi has delayed the reopening of public schools in the country’s two main cities, Blantyre and Lilongwe, in an attempt to slow the upsurge in cholera deaths. The district of
