Nduta (Tanzania): mashirika mengi ya misaada yanapanga kusimamisha shughuli zao
Angalau mashirika makuu manne ya misaada yatasimamisha huduma zake kuanzia januari mwaka wa 2023. Yatasimamisha huduma kutokana na ukosefu wa fedha. HABARI SOS Médias Burundi
Mashirika ya misaada ambayo tayari yalifahamisha kuwa yatasimamisha huduma ni pamoja na Women’s Legal Aid Center ( WILAC) inayojihusisha na sekta ya sheria, PLAN International inayosaidia watoto wa chini ya miaka 18, HelpAge International inayojihusisha na watu wazima na walemavu na IRC inayoshughulikia unyanyasaji dhidi ya akinamama.
” Mashirika hayo hayatatoa tena huduma hapa kambini. Msiwe na wasi wasi, huduma na misaada iliyokuwa inatolewa na mashirika hayo, itatolewa na shirika jingine la Danish Refugee Council (DRC). Ni kama kupishana, hakuna kitakachobadilika”, alihakikisha mfanyakazi wa HCR ambayo inahusika na uratibu wa mashirika hayo kabla ya kufafanua kuwa ukosefu wa fedha ndio sababu ya kusimamisha shughuli.
Hata hivyo wakimbizi wanahofia madhara ya hatua hiyo.
” Vipi huduma zilizokuwa zikitolewa na mashirika manne na zitakuwa zikitolewa na shirika moja ?Ni jambo la kawaida kuwa ubora wa huduma utapungua. Harafu ni mashirika muhimu yanayofunga milango”, analalamila mkimbizi kutoka Burundi, akihofia vifo kutokea mnamo siku zijazo.
Usitishwaji wa huduma umepokelewa vibaya.
“Tumetelekezwa. Ni pia ni ujumbe mzito ambao tunapewa na Tanzania na HCR. Wanataka turudi nyumbani kwa hali zote. Na hayo ni baada ya ziara ya viongozi wa Burundi hapa”, aliendelea mkimbizi huyo kwa hasira.
Wanaomba HCR “kutoanguka katika mtego wa Burundi na Tanzania” , kinyume chake, “HCR itakubali matokeo”
Haijajulikana iwapo mashirika hayo yatasimamisha shughuli katika kambi ya Nyarugusu.
Tanzania ina jumla ya wakimbizi 126.000 kutoka Burundi
You might also like
Burundi : reduced medical surveillance, massive resettlement of Congolese refugees mixed with concerns with the election of Trump
Since last August, the IOM (International Organization for Migration)-Burundi office, has put in place temporary 21-day medical surveillance measures for refugees en route to the United States, in response to
Nduta (Tanzania): prohibited drinks leads to victims
Several types of prohibited drinks, sold clandestinely, threaten the lives of refugees. The police, accused of being lax, are called upon to ensure security. INFO SOS Médias Burundi The consumption
Cibitoke : 15 Congolese drowned in the Rusizi while trying to flee fighting in the DRC
While clashes between the M23 and the Congolese army intensify in South Kivu, refugees are trying to flee to Burundi. In less than 48 hours, 15 people have lost their
