Ngozi: uhaba wa chakula kwenye gereza kuu
wafungwa katika gereza kuu la Ngozi (kaskazini mwa Burundi) wanasema kuwa wanateseka kutokana na ukosefu wa chakula. Walioathirika zaidi ni wale wanaotoka katika mikoa ya Kirundo na Kayanza (kanda hiyo hiyo). Wanadai kuwa hawapati wageni kama wenzao wenye asili ya mkoa wa Ngozi kutokana na masafa marefu ambayo wajumbe wa familia zao wanatakiwa kufanya ili kufika kwenye gereza hilo. Wagonjwa hawawezi kumeza dawa wakati ambapo hakuna kitu tumboni. Wanaomba misaada. HABARI SOS Médias Burundi
Gereza hilo linawahifadhi wafungwa kutoka mikoa ya Ngozi, Kayanza, na Kirundo. Wafungwa katika gereza hilo wanaishi katika mazingira magumu kutoka na uhaba wa chakula.
” Wiki mbili zimemalizika pasina kupewa maharagwe. Ili kuweza kula ugali wao mdogo, baadhi hununua mboga boga lakini kwa wale ambao hawana uwezo, hutumia maji ya moto yaliyowekewa chumvi. Inakasirikisha “, anahakikisha mfungwa mmoja mwenye asili ya mkoa wa Kayanza.
“Tumezoea kula mara moja kwa siku nyakati za mchana peke”, alifamisha mfungwa mmoja.
Habari kutoka katika gereza hilo zinafamisha kuwa wafungwa wenye asili ya mikoa ya Kirundo na Kayanza wanaathiriwa zaidi na hali hiyo sababu wanakuwa mbali na familia zao zinazolazimika kusafiri masafa marefu ili kuweza kuwatembelea.
” Angalau hao wenye asili ya mkoa wa Ngozi wanapata urahisi kidogo kwa sababu wajumbe wa familia zao wanaweza kuwatembelea angalau mara tatu kwa wiki. Lakini sisi njaa inatumenya. Tunaweza kupata mgeni mara moja kwa mwezi”,alilalamika mfungwa mwengine.
Maradhi ya utapia mlo yanaanza kusambaa.
Wafungwa wenye maradhi yasiopona ambao wanalazimika kula kabla ya kutumia dawa wanaathiriwa zaidi na hali hiyo.
” wafungwa wenye HIV wanalazimika kutumia dawa pasina kula. Baadhi wanaanza kupata maradhi ambayo walikuwa hawana kama kuumwa tumbo, alitoa ushuhuda huo mfungwa wa zamani.
Gereza la Ngozi linawapa hifadhi wafungwa zaidi ya 1500 wakati uwezo wake ni kuwapokea watu 400 peke.
You might also like
International Refugee Day: between hope and resignation among Burundian refugees
Every June 20, the world celebrates Refugee Day, an opportunity to think of them and defend, protect and promote their rights, according to the UNHCR. For more than 300,000 Burundians
Burundi: lawyer Tony Germain Nkina released
His release took place on Tuesday morning. A week ago, this former Burundian activist was acquitted by the Ngozi Court of Appeal (northern Burundi) before the Ngozi prosecutor’s office objected.
Cibitoke: more than 150 students in a classroom
Schoolchildren are sitting on the bare ground for lack of benches, desks and classrooms across the communal capitals of Rugombo, Mugina and Buganda, Cibitoke province (north-west Burundi). Parents request the
