Ituri: zaidi ya wananchi 200 waliuwawa na waasi katika kipindi cha miezi miwili
Tangu mwanzo wa mwaka 2023, hali ya usalama inazidi kuwa ya wasi wasi na kusikitisha katika mkoa wa Ituri karibu miaka miwili tangu kuanzisha serikali ya kijeshi. Wananchi wa kawaida wanaendelea kuuwawa na makundi ya silaha ya ndani na nje katika wilaya nyingi za mkoa wa Ituri mashariki mwa DRC. Mashirika ya kiraia yanatoa orodha ya wananchi wa kawaida 226 waliouwawa na makundi ya silaha katika miezi ya januari na februari. HABARI SOS Médias Burundi
Takwimu hizo ni za muda kulingana viongozi wa mashirika ya kiraia eneo hilo.
” Kuhusu hali ya februari 2023, tulihesabu watu 78 waliouwawa, 10 walijeruhiwa, 28 walitekwa, pikipiki 4 ziliibiwa na nyumba 379 kuchomwa moto. Hasabu hizo zinaongeza idadi ya waliouwawa kufikia watu 226 tangu januari 2023 hadi 28 februari 2023. Takwimu hizo zinasalia kuwa za muda”, anasema Dieudonné Lossa muakilishi wa shirika la wazalendo la Ituri.
Pamoja na hayo, analaani kuwa wakimbizi wa ndani wanaishi katika hali ngumu bila msaada wa serikali wala wa mashirika ya ndani na kimataifa.
Kwa kizingatiwa hali hiyo mbaya ya usalama eneo la Ituri, mashirika ya kiraia yanaomba serikali ya Kongo kuongeza idadi ya wanajeshi katika eneo lote la mkoa huo kwa ajili ya kulinda wananchi na mali zao.
Makundi mengi ya nje na ndani likiwemo kundi la ADF ( Nguvu zilizoungana kwa ajili ya demokrasia) yamekuwa chanzo cha mauwaji ya wananchi katika wilaya ya Irumu na Mambasa.
Mkoa wa Ituri pamoja na mkoa jirani wa Kivu kaskazini iko katika hali ya taharuki na utawala wa kijeshi tangu mei 2021, mfumo ambao hawukuweza kumaliza tatizo la usalama mdogo linaloendelea katika eneo hilo la Kongo.
You might also like
Cibitoke: 23 gold miners arrested
23 gold miners from the communes of Mabayi and Bukinanyana in the Cibitoke province (northwestern Burundi) are detained in the local office of SNR (National Intelligence Service). The provincial governor
Rwanda : zaidi ya wakimbizi wapya 3000 kutoka Kongo wapokelewa
HCR inafahamisha kuwa inaendelea kuwapokea wakimbizi kutoka Kongo wanaokimbilia nchini Rwanda. Zaidi ya wale 3000 tayari waliwasili wiki chache zilizopita. Kituo kipya cha muda kiliandaliwa eneo la Nkamira karibu na
Cibitoke: two Imbonerakure accused of theft beaten up in Rugombo
Two Imbonerakure (members of the CNDD-FDD party youth league) were caught stealing. Exasperated, residents rushed on them and seriously beat them up. Field owners demand that these thieves be punished
