Ituri: zaidi ya wananchi 200 waliuwawa na waasi katika kipindi cha miezi miwili
Tangu mwanzo wa mwaka 2023, hali ya usalama inazidi kuwa ya wasi wasi na kusikitisha katika mkoa wa Ituri karibu miaka miwili tangu kuanzisha serikali ya kijeshi. Wananchi wa kawaida wanaendelea kuuwawa na makundi ya silaha ya ndani na nje katika wilaya nyingi za mkoa wa Ituri mashariki mwa DRC. Mashirika ya kiraia yanatoa orodha ya wananchi wa kawaida 226 waliouwawa na makundi ya silaha katika miezi ya januari na februari. HABARI SOS Médias Burundi
Takwimu hizo ni za muda kulingana viongozi wa mashirika ya kiraia eneo hilo.
” Kuhusu hali ya februari 2023, tulihesabu watu 78 waliouwawa, 10 walijeruhiwa, 28 walitekwa, pikipiki 4 ziliibiwa na nyumba 379 kuchomwa moto. Hasabu hizo zinaongeza idadi ya waliouwawa kufikia watu 226 tangu januari 2023 hadi 28 februari 2023. Takwimu hizo zinasalia kuwa za muda”, anasema Dieudonné Lossa muakilishi wa shirika la wazalendo la Ituri.
Pamoja na hayo, analaani kuwa wakimbizi wa ndani wanaishi katika hali ngumu bila msaada wa serikali wala wa mashirika ya ndani na kimataifa.
Kwa kizingatiwa hali hiyo mbaya ya usalama eneo la Ituri, mashirika ya kiraia yanaomba serikali ya Kongo kuongeza idadi ya wanajeshi katika eneo lote la mkoa huo kwa ajili ya kulinda wananchi na mali zao.
Makundi mengi ya nje na ndani likiwemo kundi la ADF ( Nguvu zilizoungana kwa ajili ya demokrasia) yamekuwa chanzo cha mauwaji ya wananchi katika wilaya ya Irumu na Mambasa.
Mkoa wa Ituri pamoja na mkoa jirani wa Kivu kaskazini iko katika hali ya taharuki na utawala wa kijeshi tangu mei 2021, mfumo ambao hawukuweza kumaliza tatizo la usalama mdogo linaloendelea katika eneo hilo la Kongo.
You might also like
Mabayi : three men profiting greatly from the presence of Rwandan rebels arrested
Three men from the district of Mabayi in the province of Cibitoke (northwest Burundi) were arrested last Saturday. They are suspected of profiting greatly from the presence of Rwandan rebels
Nyarugusu (Tanzania) : armed robbery
A trader in zone 11 was attacked at his home by armed men who have not yet been identified. Two refugees, including a Burundian, were seriously injured. The incident took
Bujumbura attack : Burundian authorities took official stock and accused Rwanda again
After Friday’s early evening grenade attack on a public transport bus parking lot in the commercial city Bujumbura, Burundian authorities reported 38 injured, including 5 seriously. A spokesperson for the
