Uvira : mwanajeshi mmoja na wananchi wawili wauwawa
Raia wawili wa kawaida, waliuwawa na watu wanaobebelea silaha. Na mwanajeshi mmoja wa Kongo pia aliuwawa. Waliouwawa walikuwa miongoni mwa kundi la vijana walinzi wa amani wanaofanya doria usiku. Mwanajeshi huyo upande wake, alipigwa na wananchi. HABARI SOS Médias Burundi
Hali hiyo ilianza jumamosi jioni katika kata ya Kasenga. Ni katika mji wa Uvira katika mkoa wa Kivu ya kusini mashariki mwa DRC.
Wezi wanaotumia silaha walijaribu kuiba katika maduka, vijana walinzi wakawafuatilia. Kijana mmoja aliuwawa wa watu hao wanaobebelea silaha. Katika kuwafuatilia, wezi hao , vijana hao walinzi wa amani, walipofika mbali, walikutana na wanajeshi wa Kongo, vijana hao wakishirikiana na wakaazi wengine wakawakabili wanajeshi hao. Wakajaribu kumpiga mawe mwanajeshi anayetuhumiwa kujumuika na genge hilo la wezi. Alipelekwa kwenye hospitali ya Uvira akiwa katika hali mbaya.
Jumapili asubuhi, hali hiyo iliibuka tena. Wakati vijana hao wakipeleka muili wa ndugu yao wakakutana na askali jeshi na kumushambulia na kutaka kumpiga mawe. Alifuatua risasi dhidi yao na kuwauwa wawili kati yao.
Wakaazi walimufuatilia mwanajeshi huyo na kumuuwa kwa kumpiga mawe. Kupitia tangazo, jeshi la Kongo linathibitisha kifo cha mwanajeshi huyo na wananchi wawili na kuzidi kuwa watu wengi watatu akiwemo mwanajeshi mmoja walijeruhiwa.
” Mwanajeshi huyo alikuwa katika hali mahtuti ” , jeshi la Kongo linafahamisha na kukumbusha kuwa usalama wa wananchi na mali zao ni jukumu la taasisi za ulinzi na usalama “.
Wakaazi wa mkoa wa Kivu kusini waliozungumza na SOS Médias Burundi wanawaomba viongozi wa Kongo” kusimamisha shughuli za vijana walinzi wa kawaida ambao wana utawala usiokuwa na mipaka”.
Kamanda wa sekta ya operesheni ya Sokola 2 anataja kisa hicho kilichosababisha kifo cha mwanajeshi kuwa ni kitendo dhidi ya uzalendo.
You might also like
Cankuzo-Ruyigi: access to public services conditioned by the payment of forced contributions of the CNDD-FDD
The forced contributions that were decided by the presidential party in order to finance its electoral campaign for the 2025 legislative elections, have not spared the provinces of Cankuzo and
Makamba : chumba cha kuhifadhi maiti hakifanyi kazi kwa takriban mwaka mmoja sasa
Kwa mjibu wa wafanyakazi kwenye hospitali hiyo ya Makamba ( kusini mwa Burundi) pamoja na familia zilizokosa watu, chumba cha kuhifadhi maiti sasa ni takriban mwaka mmoja kikiwa hakifanyi kazi.
Irumu: about fifteen people manage to escape from the hands of ADF fighters
It was in the territory of Irumu, in the province of Ituri in the east of the DRC that the concerned persons were able to escape from posts of the
