Lusenda-Mulongwe : njaa yapiga hodi katika kambi za wakimbizi kutoka Burundi

Lusenda-Mulongwe : njaa yapiga hodi katika kambi za wakimbizi kutoka Burundi

Wakimbizi wa kambi za Lusenda na Mulongwe katika wilaya ya Fizi mkoa wa Kivu ya kusini mashariki mwa DRC wanasema kuwa wanakabiliana na uhaba wa chakula. PAM (WFP) shirika la mpango wa chakula duniani ambalo huwapatia msaada wa chakula, sasa ni miezi mitatu pasina kuwapa chakula. Wanahofia baa la njaa katika eneo hilo la Kongo ambapo maafisa wa usalama wanawaomba kuacha kutoka nje ya kambi kwa hofu ya kushambuliwa na kuuwawa na makundi ya silaha. HABARI SOS Médias Burundi

Kawaida shirika la PAM huwapa pesa wakimbizi ili waweze kununua wenyewe chakula wanachohitaji. Lakini sasa ni miezi mitatu bila wakimbizi hao kupewa msaada huo.

” Idadi kubwa kati yetu waliuzisha vifaa vya ndani ili kuendelea kuishi “, wakuu wa familia walisema.

Kwa mjibu wa Rémy Habumuremyi, muakilishi wa watu wanaotembea na ulemavu eneo la Lusenda, hali hiyo imewaathiri idadi kubwa na wajumbe wa shirika hilo.

” Hatuwezi kutoka nje ya kambi kwa ajili ya kutafuta kazi kwa raia wa Kongo” , analalamika.

Hali hiyo imepelekea wanafunzi kuacha shule kama alivyofanya kijana Rashidi.

” Nililazimika kuacha shule na kwenda kutafuta kazi kwa wavuvi katika ziwa Tanganyika sababu familia yangu inakabiliwa na umasikini mkubwa. Bila msaada wa chakula, familia haiwezi kuwapa chakula mimi na ma Kaka na dada zangu”, kujana huyo alitoa ushuhuda huo.

Baadhi ya akinamama kama Evelyne Kubwimana hushinda kutwa nzima kwenye fukwe la ziwa Tanganyika. Anaandaa chakula kwa ajili ya wavuvi.

” Hii inanisaidia kupata pesa ndogo kwa ajili ya kununua unga wa kusonga uhalifu na mboga za kutumia kwa watoto wangu”, alifafanua mwanamke huyo mwenye asili ya Burundi.

Katika kambi ya Lusenda, kila mkimbizi hupewa sarafu za Kongo 19500 kwa gharama ya chakula cha kila mwezi. Wakimbizi wanasema pesa hiyo “haitoshi”.

” Bei ya vyakula imepanda kwa kiwango kikubwa”, wakimbizi wanasema.

Hali ni kama hiyo katika kambi ya Mulongwe

Marie Kubwimana ni mkimbizi kutoka kambi ya Mulongwe. Anafahamisha kuwa alijiandikisha kwenye orodha ya wale wanaopendelea kurudi nchini kwa sababu ya ukosefu wa vyakula.

François Nizigiyimana pia alichukuwa msimamo huo. Kutokana na hali hiyo, wakimbizi wengi kutoka Burundi, wanaanza kuomba msaada nje ya kambi hususan kwenye fukwe za ziwa Tanganyika.

SOS Médias Burundi haikukufanikiwa kuwapata viongozi wa PAM ili wafafanuwe sababu za hali hiyo. Lakini kamati ya kitaifa inayohusika na wakimbizi wanahakikisha kuwa walipata taarifa hizo.

DRC inawapa hifadhi wakimbizi elfu 40 kutoka Burundi . Mwezi februari uliopita, warudi hao waliopewa hifadhi mashariki mwa nchi hiyo kubwa ya Afrika ya kati inayokabiliwa na usalama mdogo kwa takriban miaka 30 , walionyeshwa kwa baba mtakatifu François ambaye aliwapokea wahanga wa uhalifu unaofanyika mashariki mwa Kongo .

Previous Beni : zaidi ya watu 70 wauwawa katika kipindi cha siku 6
Next Goma : several private media deprived of access to information

You might also like

Refugees

Dzaleka (Malawi) : police demolish two refugee homes

Malawi police accuse two Ethiopian refugees of harboring armed bandits. Their homes were demolished on Monday. Dzaleka camp has been the scene of armed robberies recently. INFO SOS Médias Burundi

Diplomacy

World Refugee Day 2026 : between despair, pressure to return, and a protracted humanitarian crisis in the camps

From Nyarugusu to Kakuma, via Mahama, Nakivale, Meheba, Lusenda, and the reception sites in Burundi, Burundian and Congolese refugees are experiencing a World Refugee Day marked by reduced humanitarian assistance,

Refugees

Nduta (Tanzania): several humanitarian NGOs will suspend their activity

At least four main humanitarian NGOs will no longer provide their services to refugees from January 2023. They will suspend their activity for lack of financial means. INFO SOS Médias