Nyarugusu (Tanzania) : zaidi ya wakimbizi mia moja wenye asili ya Burundi walazimishwa kurejea makwao kwa nguvu
Kwa sababu ya kutokuwepo wakati wa sensa kwa ajili ya uhakikisho ya mwaka wa 2021, shirika linalowahudumia wakimbizi (HCR), liliondoa wakimbizi wenye uraia wa Burundi zaidi ya mia moja kwenye orodha ya wale wanastahili kupewa misaada. HABARI SOS Medias Burundi
Chanzo cha mkasa huo ni sensa nyingine ya kuthibitisha iliyofanyika “kwa kushitukiza” ndani ya kambi ya Nyarugusu mwaka wa 2021.
” Watu wengi hawakuwa kambini. Walikuwa katika miji ya Dar Es Salam , Kigoma na Mwanza kwa ajili ya kutafuta ajira. Wengine walikuwa kwenye vyuo vikuu mbali mbali kusoma huku wengine hususan wasichana wakiwa waliolewa na raia wa Tanzania” wakimbizi walitoa ushuhuda huo.
Lakini kuanzia mwaka uliopita, wengi kati yao walirejea kambini wakitegemea kuendelea kupata misaada kutoka HCR.
Lakini kwa mshangao mkubwa, walifahamishwa kuwa hawatambuliki tena kama wakimbizi.
” Ni jambo lisiloeleweka. Unaweza kupata mume au mke ambaye sio mkimbizi wakati ambapo watoto ni wakimbizi. Mjumbe wa familia anaweza kukosekana kwenye orodha wakati wa ndugu zake ma kaka na ma dada wakiwepo” wakimbizi wanaeleza.
Wahusika waliamuru kutoa malalamiko ambayo yalichukuwa zaidi ya mwaka mmoja. Lakini mwisho hayakukubaliwa, kama ilivyotangaza Danish Refugee Council ( DRC).
Hivyo, kulingana na shirika la DRC, hadhi ya ukimbizi inarejeshwa wakati muhusika anapojiorodhesha ili ” kurejea makwao kwa hiari “
” zaidi ya 50 kati yao walirejeshwa wiki hii na wiki iliyopita sababu walikuwa hawana chaguo jingine. Wengine wanasubiri kuchukuwa njia hiyo sababu hawapati tena msaada. Wanapopatwa na maradhi, hawatibiwi. Ndani ya kambi wanatafutwa kama wahalifu”. watu wa karibu yao wanalaani na kukosoa ” mpango wa ulioundwa kwa ushirikiano kati ya Tanzania na Burundi “.
” Tunahofia hata usalama wao ndani ya kambi sababu kuna wengine ambao bado wanaojificha hapa. Mara baada ya kuwasili nchini Burundi, wakipata tatizo lolote, HCR itaulizwa “, wanasisitiza huku wakiomba hatua hiyo isimamishwe bila starti lolote na hatua ya kurejea iweze kuwa hiari wakati wa kurejesha wakimbizi.
Kambi ya Nyarugusu ina zaidi ya wakimbizi wa Burundi elfu 50.
You might also like
Burundi: Maelfu ya wakimbizi wa Kongo waachwa huku baadhi ya walimu wakirejea DRC
SOS Médias Burundi Bujumbura/Ruyigi, Februari 5, 2026 – Siku ya Alhamisi, Februari 5, walimu sitini na tano wakimbizi kutoka Kongo, wanaoishi katika mji mkuu wa kiuchumi wa Bujumbura, kilomita chache
Mahama (Rwanda): ukosefu wa makazi kwa wakimbizi wapya
Wakimbizi wapya, hasa Wakongo, wanatatizika kupata makazi katika kambi ya Mahama. Utawala unajenga zaidi ya nyumba 500 mpya. HABARI SOS Médias Burundi Walioathirika zaidi ni Wakongo waliohamishwa hivi karibuni katika
Kakuma (Kenya): wakimbizi waliandamana kudai kupata mgao na maji ya kunywa
Mwishoni mwa wiki iliyopita, wakimbizi kadhaa waliandamana katika ofisi ya UNHCR. Wanadai usambazaji wa maji ya kunywa ingawa kambi imetumia zaidi ya mwezi mmoja bila karibu tone la bidhaa hii
