Nyarugusu (Tanzania) : zaidi ya wakimbizi mia moja wenye asili ya Burundi walazimishwa kurejea makwao kwa nguvu
Kwa sababu ya kutokuwepo wakati wa sensa kwa ajili ya uhakikisho ya mwaka wa 2021, shirika linalowahudumia wakimbizi (HCR), liliondoa wakimbizi wenye uraia wa Burundi zaidi ya mia moja kwenye orodha ya wale wanastahili kupewa misaada. HABARI SOS Medias Burundi
Chanzo cha mkasa huo ni sensa nyingine ya kuthibitisha iliyofanyika “kwa kushitukiza” ndani ya kambi ya Nyarugusu mwaka wa 2021.
” Watu wengi hawakuwa kambini. Walikuwa katika miji ya Dar Es Salam , Kigoma na Mwanza kwa ajili ya kutafuta ajira. Wengine walikuwa kwenye vyuo vikuu mbali mbali kusoma huku wengine hususan wasichana wakiwa waliolewa na raia wa Tanzania” wakimbizi walitoa ushuhuda huo.
Lakini kuanzia mwaka uliopita, wengi kati yao walirejea kambini wakitegemea kuendelea kupata misaada kutoka HCR.
Lakini kwa mshangao mkubwa, walifahamishwa kuwa hawatambuliki tena kama wakimbizi.
” Ni jambo lisiloeleweka. Unaweza kupata mume au mke ambaye sio mkimbizi wakati ambapo watoto ni wakimbizi. Mjumbe wa familia anaweza kukosekana kwenye orodha wakati wa ndugu zake ma kaka na ma dada wakiwepo” wakimbizi wanaeleza.
Wahusika waliamuru kutoa malalamiko ambayo yalichukuwa zaidi ya mwaka mmoja. Lakini mwisho hayakukubaliwa, kama ilivyotangaza Danish Refugee Council ( DRC).
Hivyo, kulingana na shirika la DRC, hadhi ya ukimbizi inarejeshwa wakati muhusika anapojiorodhesha ili ” kurejea makwao kwa hiari “
” zaidi ya 50 kati yao walirejeshwa wiki hii na wiki iliyopita sababu walikuwa hawana chaguo jingine. Wengine wanasubiri kuchukuwa njia hiyo sababu hawapati tena msaada. Wanapopatwa na maradhi, hawatibiwi. Ndani ya kambi wanatafutwa kama wahalifu”. watu wa karibu yao wanalaani na kukosoa ” mpango wa ulioundwa kwa ushirikiano kati ya Tanzania na Burundi “.
” Tunahofia hata usalama wao ndani ya kambi sababu kuna wengine ambao bado wanaojificha hapa. Mara baada ya kuwasili nchini Burundi, wakipata tatizo lolote, HCR itaulizwa “, wanasisitiza huku wakiomba hatua hiyo isimamishwe bila starti lolote na hatua ya kurejea iweze kuwa hiari wakati wa kurejesha wakimbizi.
Kambi ya Nyarugusu ina zaidi ya wakimbizi wa Burundi elfu 50.
You might also like
Picha ya wiki: Wakimbizi 1,150 wa Rwanda walirudishwa makwao katika muda wa saa 48
Goma, Mei 20, 2025 – Jumatatu hii, Mei 19, wakimbizi 790 wa Rwanda walirejeshwa nchini mwao kupitia kizuizi kikubwa cha Corniche, kati ya Goma (DRC) na Gisenyi (Rwanda). Wao ni
Zambia: wakimbizi wanashutumu kusimamishwa kwa muda mrefu kwa utoaji wa vibali vya kutoka kambini
Imepita zaidi ya miezi miwili tangu utoaji wa vibali vya kutoka kambini kusitishwa kwa muda katika takriban kambi zote za wakimbizi nchini Zambia. Sababu ni kwamba vibali hivi vitatolewa kwa
Uvira: UNHCR inahimiza wakimbizi kurejea
Mpango wa UNHCR wa “Nenda ukaone” umekuwa ukipanuka kote DRC katika siku za hivi karibuni. Kwa ushirikiano na mamlaka ya Burundi na Kongo, UNHCR ilikuwa na timu ya wakimbizi wa
