Kivu-kaskazini : vijiji vyasalia pasina wakaazi
Vijiji vingi katika eneo la Jomba wilaya ya Rutshuru mkoa wa Kivu kaskazini mashariki mwa DRC vimesabaki pasina wakaazi kutokana na mapigano kuibuka tena alhamisi kati ya jeshi la FARDC na kundi la M23. Vyanzo eneo hilo vinaarifu kuwa watu wanakimbilia hasa nchini Uganda na kwenye vituo ambako wanaona usalama ni wa hakika. HABARI SOS Médias Burundi
Viongozi tawala wanaeleza kuwa familia kutoka eneo la Ntamugenga na Tarika wanaendelea kuwasili eneo la Rubare mji ambao uko karibu na makao makuu ya Rutshuru.
Wakati huo huo, wakaazi wa maeneo ya kibanda na Rangira wanakwenda kwa wingi kwenye makao makuu ya wilaya ya Rutshuru.
Wakaazi wa Tchengerero na Kabindi wanakimbilia Bunagana na wengi wamevuka mpaka na kuingia nchini Uganda.
Hali ni hiyo pia kwa wakaazi wa Bunagana wanaokimbia eneo hilo la mpakani na kupata hifadhi nchini Uganda.
Wananchi waliokimbilia nchini Uganda walipelekwa katika kambi ya Nakivale, mbali na mpaka.
Jeshi la FARDC ( jeshi la jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo) linaendelea kutuhumu kundi la M23 kuanzisha mapigano kwa lengo la kuzuia nenda rudi kwenye barabara kuu inayotumiwa kupeleka misaada kwa jeshi katika ukanda huo wakati ambapo waasi upande wao wanasema ni jeshi la FARDC lililoshambulia ngome zake na hivyo wakalazimika kujihami.
You might also like
North Kivu: renewal of fighting between the FARDC and the M23 in Rutshuru
New clashes between the Armed Forces of the Democratic Republic of Congo (FARDC) and the M23 have broke out since Friday morning in several villages in the territory of Rutshuru,
Cibitoke: 23 gold miners arrested
23 gold miners from the communes of Mabayi and Bukinanyana in the Cibitoke province (northwestern Burundi) are detained in the local office of SNR (National Intelligence Service). The provincial governor
Gitega : a police officer in detention after killing cows
Majorique Irankunda, a police officer, was arrested on the morning of Monday, August 5. A police source indicates that he is held in the provincial police station cell. He is
