Nduta (Tanzania): ghasia kati ya polisi na wakimbizi kutoka Burundi
Tangu weekendi iliyopita, polisi imekuwa katika harakati za kuwakamata wafanyabiashara wanaoendeshea shughuli zao nyumbani. Maduka pia yanachomwa moto. Hasira ya wakimbizi ilipanda hadi kuwarushia mawe polisi. HCR ilijaribu kutuliza hali. HABARI SOS Médias Burundi
Maeneo yaliyolengwa hasa ni yale ya zone 18, 20 na 21. Polisi ilitafuta bidhaa zilizohifadhiwa nyumbani na ambazo zinaendelea kuuzwa wakati ambapo masoko na maduka vilifungwa tena.
Hasira ilipanda pale ambapo polisi walibomoa nyumba zinazotumiwa kama maduka.
” Walikuwa wanamaliza kubomoa nyumba 10 zikiwemo zile za wajane kwa hoja kwamba walikuta ndani matunda, mboga boga na kreti ya soda kwa ajili ya kuuzisha. Kwa hiyo, hatungendelea kulea mikono. Baadhi yetu waliwarushia mawe askali polisi. Upande wao walitumia gesi ya kutoa machozi ili kutusambaratisha. Pande mbili zilipata majeruhi madogo” alieleza mkimbizi mmoja.
HCR iliingilia kati ili kutuliza hali
” Pasina kushituka , mfanyakazi wa HCR aliwasili na hakulaani visa hivyo vya kubomoa nyumba zilizojengwa na HCR kwa ajili ya wakimbizi. Alituelezea tu tusiwapigi tena mawe askali polisi, tuwaache wafanye kazi yao na tujiepushe kukabiliana nao, jambo linaloonyesha kuwa HCR haina nguvu au ni mshirika” wanalaani raia wa Burundi.
Kuitishwa……
Wakimbizi wengi hasa vijana walisimamishwa. Wanazuiliwa jela.
” Tunaomba HCR kutupilia mbali unyanyasaji unaofanywa dhidi yetu na kuchangia ili raia wenzetu waweze kuachiwa huru. Tuko katika matatizo hapa ndani ya kambi nchini Tanzania” wanazidi kusema wakimbizi kutoka burundi.
Wakimbizi wanadai kuwa ni njama za kuwalazimisha kurudi makwao sababu serikali ya burundi na ile ya Tanzania walikubaliana kuwa wakimbizi wote ni lazima warudi makwao ” kwa hiari au kwa nguvu “.
Wanaomba jamii ya kimataifa na HCR tawi la afrika mashariki kuingilia kati ili kuheshimisha makubaliano kuhusu haki za wakimbizi.
Nduta ndio kambi kubwa ya wakimbizi kutoka Burundi nchini Tanzania, ina zaidi ya wakimbizi elfu 76.
You might also like
South Kivu : a Burundian journalist arrested in Mulongwe, suspected of links with the Red-Tabara group
SOS Médias Burundi Mulongwe, April 17, 2025 – Burundian journalist Gérardine Ingabire, a refugee in the Democratic Republic of Congo and an employee of the community radio station Amani FM
Buhumuza : cholera outbreak, refugee buses at the heart of concerns
SOS Médias Burundi Ruyigi, December 28, 2025 – Residents of the districts of Butaganzwa and Ruyigi, in Buhumuza province in eastern Burundi, are expressing serious concern about the risk of
Nduta (Tanzania) : a Burundian refugee found dead in the camp
SOS Médias Burundi Nduta, August 30, 2025 – The lifeless body of a Burundian refugee, known as Adelin, was found on the morning of Friday, August 29, 2025, in a
