Kivu-kaskazini : Mpatanishi Kenyatta ziarani eneo la vita
Katika shabaha ya jukumu lake alilopewa na jumuiya ya afrika mashariki, rais huyo mstaafu wa Kenya Uhuru Kenyatta jumanne hii amekuwa mjini Goma makao makuu ya mkoa wa Kivu-kaskazini mashariki mwa DRC. Katika ziara hiyo alijipa jukumu la kuwafariji wakimbizi wa vita waliokimbia ujio wa M23 katika eneo la Rutshuru. HABARI SOS Médias Burundi
Uhuru Kenyatta alipokelewa na gavana mwanajeshi wa Kivu-kaskazini luteni jemedali Constant Ndima na kamati yake ya usalama. Wote kwa pamoja walijielekeza kwenye kambi ya wakimbizi wa ndani ya Kanyaruchinya katika wilaya ya Nyiragongo ambayo inawapa hifadhi wakimbizi wa vita laki mbili waliotoroka ujio wa waasi wa M23 inayodhibiti eneo kubwa la Rutshuru.
Katika mkutano na wandishi wa habari, Bwana Kenyatta alisema kuwa anahofia janga la kibinadamu kutokea katika eneo la Nyiragongo ambako kuna ma mia ya wakimbizi.
” Kile nilichoona Goma na maeneo yake ya karibu kinasikitisha. Ni janga la kibinadamu linaloweza kutokea iwapo hakuna kitakachofanyika ” amebaini.
Uhuru Kenyatta aliyechaguliwa mwezi juni na marais wenzake kuwa mpatanishi katika mzozo nchini Kongo, aliwasili mjini Kinshasa (makao makuu ya DRC) jumamosi iliyopita. Tayari alikutana na ma wakuu wa mabaraza mawili ya bunge na seneti vya Kongo na wajumbe wa jamii zenye asili ya mikoa ya Kivu-kaskazini, kivu-kusini na Ituri pamoja pia na wawakilishi wa nchi zao.
Upande wa Kongo ulikariri daima tuhuma zake dhidi ya Rwanda ambayo wanasema kuwa inaunga mkono M23 madai rais wa Paul Kagame kwa mara nyingine wekendi iliyopita aliyakanusha akiwa katika mkutano na shirika la “Unity club ” jukwa la viongozi wa Rwanda lililoanzishwa na mke wa rais Jeanette Kagame.
You might also like
Rugombo : a body found not far from the border with the DRC
A decapitated body of a man was discovered in a corn and bean field in the locality of Rusiga, in the district of Rugombo, province of Cibitoke (northwest Burundi), not
Mabanda: two women accused of street fuel sales transferred to the Makamba prosecutor’s cell
Two women were transferred to the Makamba prosecutor’s cell (southern Burundi) for illegal fuel sales last Friday. They had been arrested by the Mabanda police (same province) near the communal
Kiliba : mwananchi ameuwawa na askali jeshi
Tukio hilo lilijiri katika eneo la Kiliba katika mkoa wa Kivu kusini mashariki mwa DRC siku ya jumanne. Aliyehusika na mauwaji hayo ni mwanajeshi wa Kongo anayehudumu katika sekta ya
