Burundi: ni nani waliomuteka mwandishi wa habari Jérémie Misago ?
Mwenzetu hajulikani alipo tangu jumamosi iliyopita. Jumatatu hii, ameonekana ndani ya video akidai kuwa yuko salama bila hata hivyo kufahamisha malaha alipo. HABARI SOS Médias Burundi
Ni majira ya mchana ambapo video hiyo imetumwa kwa watu wake wa karibu. Mwandishi huyo ameonekana kama mtu aliyetulia. Amesema kuwa ” yuko salama” lakini hakubiani mahala alipo. Anafahamisha tu kuwa ” atasema yaliomukuta”.
Katika video hiyo isiokuwa ya kawaida”, mwandishi huyo Jérémie Misago anaeleza : ” Nilijikuta katika eneo hili la nchini kati bila kujuwa . Sikupanga hayo, ningepanga ningewafahamisha watu wa karibu na marafiki. Amehakikisha kuwa angewasili Bujumbura jumatatu jioni au jumanne asubuhi.
Mwenzetu huyo alionekana akiwa na mudhaifu, chini ya vitisho, akiwa amechoka na kuonekana kuogopa mtu aliyekuwa pembeni yake, akilazimika kukariri kwa vitu.
Katika tangazo, gazeti la Iwacu halikupenda kutoa maelezo zaidi na kupongeza polisi kwa “ushirikiano wake mzuri”.
Msemaji wa polisi ya Burundi (PNB), Désiré Nduwimana ametuhakikishia kuwa “polisi inafahamu tatizo hilo, vyombo vya usalama vinafanya kazi yao. Tutawambia maendeleo”.
Kwa mjibu wa mtalaam katia sayansi ya mawasiliano, kuona mwenzetu ameamuru kutuma video kuliko kurudi nyumbani ni jambo linaloleta wasi wasi.
“Ni ajabu. Katika hali kama hiyo, jambo la kwanza, mwandishi Jérémie Misago angetakiwa kurudi nyumbani kuliko kuchukua vidéo” amebaini mtalaam huyo.
You might also like
DRC – Rutshuru : growing insecurity in the Busanza groupment
Résidents of Busanza groupment in the chiefdom of Bwisha, Rutshuru terrotory in North Kivu, eastern Democratic Republic of Congo, are indignant at the resurgence of insecurity, days after a similar
Vita nchini DRC: M23 yaacha sehemu ya ngome zake
Ijumaa hii, kundi la M23 limefahamisha rasmi kuwa wapiganaji wake wamejiondoa kwenye ngome zao za Kibumba. Ni kwenye umbali wa takriban kilometa 20 kutoka mjini Goma, makao makuu ya mkoa
North Kivu: part of the Busanza groupment annexed by Uganda ?
Residents of the Busanza groupement in the Rutshuru territory in the North Kivu province (eastern DRC) say Uganda has moved boundary markers marking the border between this country and the
