Bukinanyana: waasi wa Rwanda wameuwawa na wengine kukamatwa
Siku chache zilizopita, mapigano kati ya jeshi la Burundi dhidi ya watu wenye kubebelea silaha yalifanyika. Makabiliano yalifanyika katika msitu wa Kibira kwenye tarafa za Mabayi na Bukinanyana (mkoa wa Cibitoke, kaskazini magharibi mwa Burundi). HABARI SOS Médias Burundi
Vyanzo vya ndani vinafahamisha kuwa angalau waasi saba waliuwawa na wengine wanne kukamatwa.
Kwa mjibu wa mashahidi, mapigano makali yalisababisha wasiwasi miongoni mwa wananchi.
” Mapigano yalikuwa makali. Wanajeshi wa Burundi waliwashitukia waasi wa Rwanda na kuwashambulia ambao upande wao walijihami. Tayari miili saba imepatikana na waasi wane kukamatwa “. wanathibitisha mashahidi.
Kukimbia
Vyanzo katika jeshi ambao majina yalihifadhiwa wanaeleza kuwa walipewa amri ya kuwafurusha waasi. Na kuzidi kuwa : ” hata hivyo taarifa zilivuja .Tuko na uhakika kuwa walifahamu kuhusu mpango wetu wa kuwashambulia. Ni jambo lisilorahishishia idara ya upelelezi ili kutoa muelekeo wa operesheni uwanjani ” wanalaani.
Hofu
Familia nyingi zililazimika kutoroka makaazi yao wakihofia usalama wao,…..tuliyajuwa hayo. Mkuu wa tarafa ya Bukinanyana aliwaomba wakaazi kuwafichua wanaoshirikiana na waasi.
Kiongozi mmoja wa kijeshi alisisitiza juu ya kile alisema ” hali imedhibitiwa ” bila kutoa maoni yoyote kuhusu mapigano hayo yaliyoripotiwa na vyanzo vya ndani.
You might also like
Nyabitsinda: a CNL headquarters destroyed and burned
A CNL party headquarters on Nyaruganda hill was destroyed and burned during the night of 19 January. It is in the commune of Nyabitsinda (province of Ruyigi, eastern Burundi). The
Butaganzwa : a woman killed, her husband injured with a machete
A woman was killed and her husband injured with a machete in the village of Kivumu, in the district of Butaganzwa in the province of Ruyigi (eastern Burundi) on Friday
Rwanda-DRC : jeshi la Rwanda lashambulia ndege ya kivita ya Kongo ndani ya anga ya Kongo (Tangazo)
Serikali ya Kongo inatuhumu jeshi la Rwanda kushambulia ndege yake ya kivita ya Kongo ndani ya anga ya DRC. Ni kulingana na tangazo la viongozi wa Kongo la jumanne hii
