Bukinanyana: waasi wa Rwanda wameuwawa na wengine kukamatwa

Bukinanyana: waasi wa Rwanda wameuwawa na wengine kukamatwa

Siku chache zilizopita, mapigano kati ya jeshi la Burundi dhidi ya watu wenye kubebelea silaha yalifanyika. Makabiliano yalifanyika katika msitu wa Kibira kwenye tarafa za Mabayi na Bukinanyana (mkoa wa Cibitoke, kaskazini magharibi mwa Burundi). HABARI SOS Médias Burundi

Vyanzo vya ndani vinafahamisha kuwa angalau waasi saba waliuwawa na wengine wanne kukamatwa.

Kwa mjibu wa mashahidi, mapigano makali yalisababisha wasiwasi miongoni mwa wananchi.

” Mapigano yalikuwa makali. Wanajeshi wa Burundi waliwashitukia waasi wa Rwanda na kuwashambulia ambao upande wao walijihami. Tayari miili saba imepatikana na waasi wane kukamatwa “. wanathibitisha mashahidi.

Kukimbia

Vyanzo katika jeshi ambao majina yalihifadhiwa wanaeleza kuwa walipewa amri ya kuwafurusha waasi. Na kuzidi kuwa : ” hata hivyo taarifa zilivuja .Tuko na uhakika kuwa walifahamu kuhusu mpango wetu wa kuwashambulia. Ni jambo lisilorahishishia idara ya upelelezi ili kutoa muelekeo wa operesheni uwanjani ” wanalaani.

Hofu

Familia nyingi zililazimika kutoroka makaazi yao wakihofia usalama wao,…..tuliyajuwa hayo. Mkuu wa tarafa ya Bukinanyana aliwaomba wakaazi kuwafichua wanaoshirikiana na waasi.
Kiongozi mmoja wa kijeshi alisisitiza juu ya kile alisema ” hali imedhibitiwa ” bila kutoa maoni yoyote kuhusu mapigano hayo yaliyoripotiwa na vyanzo vya ndani.

Previous Ituri: a new attack by ADF rebels leaves dead and injured in Irumu
Next Burundi: ni nani waliomuteka mwandishi wa habari Jérémie Misago ?

You might also like

Security

Mzozo mashariki mwa Kongo : askali mmoja wa kikosi cha umoja wa mataifa auwawa na mwingine kujeruhiwa vikali kutokana na shambulizi dhidi ya ndege la Monusco

Monusco (ujumbe wa umoja wa mataifa nchini DRC) umetangaza kifo cha askali wake kupitia tangazo. Ujumbe huo unafahamisha kuwa alifariki kutokana na shambulio dhidi ya moja kati ya ndege zake

Society

Bururi : three men and a woman sentenced for willful murder

Gabriel Nizigama, Leonidas Nditije and Leonidas Nyandwi were sentenced to life jail on Tuesday by the High Court of Bururi (southern Burundi). They are accused of having murdered Rosine Nimbona

Security

Giharo : the district police commissioner killed with machetes

Police Major Japhet Mukeshimana was killed on the evening of Tuesday, January 2, 2024. The tragedy took place in Nkanka village in Giharo district in Rutana province in southeast Burundi.