Burundi: ni nani waliomuteka mwandishi wa habari Jérémie Misago ?

Burundi: ni nani waliomuteka mwandishi wa habari Jérémie Misago ?

Mwenzetu hajulikani alipo tangu jumamosi iliyopita. Jumatatu hii, ameonekana ndani ya video akidai kuwa yuko salama bila hata hivyo kufahamisha malaha alipo. HABARI SOS Médias Burundi

Ni majira ya mchana ambapo video hiyo imetumwa kwa watu wake wa karibu. Mwandishi huyo ameonekana kama mtu aliyetulia. Amesema kuwa ” yuko salama” lakini hakubiani mahala alipo. Anafahamisha tu kuwa ” atasema yaliomukuta”.

Katika video hiyo isiokuwa ya kawaida”, mwandishi huyo Jérémie Misago anaeleza : ” Nilijikuta katika eneo hili la nchini kati bila kujuwa . Sikupanga hayo, ningepanga ningewafahamisha watu wa karibu na marafiki. Amehakikisha kuwa angewasili Bujumbura jumatatu jioni au jumanne asubuhi.
Mwenzetu huyo alionekana akiwa na mudhaifu, chini ya vitisho, akiwa amechoka na kuonekana kuogopa mtu aliyekuwa pembeni yake, akilazimika kukariri kwa vitu.
Katika tangazo, gazeti la Iwacu halikupenda kutoa maelezo zaidi na kupongeza polisi kwa “ushirikiano wake mzuri”.

Msemaji wa polisi ya Burundi (PNB), Désiré Nduwimana ametuhakikishia kuwa “polisi inafahamu tatizo hilo, vyombo vya usalama vinafanya kazi yao. Tutawambia maendeleo”.

Kwa mjibu wa mtalaam katia sayansi ya mawasiliano, kuona mwenzetu ameamuru kutuma video kuliko kurudi nyumbani ni jambo linaloleta wasi wasi.

“Ni ajabu. Katika hali kama hiyo, jambo la kwanza, mwandishi Jérémie Misago angetakiwa kurudi nyumbani kuliko kuchukua vidéo” amebaini mtalaam huyo.

Previous Bukinanyana: waasi wa Rwanda wameuwawa na wengine kukamatwa
Next Cibitoke: three judicial police officers and an administrative officer detained for murder and corruption

You might also like

Security

Kivu-kaskazini: Jeshi na kundi la M23 wanapigana eneo la Rutshuru karibu na RN2

Mapigano kati ya jeshi la jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo na kundi la machi 23 yameshika kasi alhamisi hii 27 oktoba 2022 katika maeneo ya Chimirwa kwa takriban kilometa 4

Security

Burundi-DRC : Burundi sends other soldiers to Congo

According to the permanent secretary of the national security council, the second group of Burundian soldiers joined Congolese territory on Wednesday. At a time when the first group which went

Security

Cibitoke : Rwandan rebels killed in the intelligence service cell

Several Rwandan FLN rebels, incarcerated in the dungeon of the national intelligence service in Cibitoke (northwest Burundi), were killed. Sources within the police affirm that their bodies were immediately driven