Burundi: ni nani waliomuteka mwandishi wa habari Jérémie Misago ?
Mwenzetu hajulikani alipo tangu jumamosi iliyopita. Jumatatu hii, ameonekana ndani ya video akidai kuwa yuko salama bila hata hivyo kufahamisha malaha alipo. HABARI SOS Médias Burundi
Ni majira ya mchana ambapo video hiyo imetumwa kwa watu wake wa karibu. Mwandishi huyo ameonekana kama mtu aliyetulia. Amesema kuwa ” yuko salama” lakini hakubiani mahala alipo. Anafahamisha tu kuwa ” atasema yaliomukuta”.
Katika video hiyo isiokuwa ya kawaida”, mwandishi huyo Jérémie Misago anaeleza : ” Nilijikuta katika eneo hili la nchini kati bila kujuwa . Sikupanga hayo, ningepanga ningewafahamisha watu wa karibu na marafiki. Amehakikisha kuwa angewasili Bujumbura jumatatu jioni au jumanne asubuhi.
Mwenzetu huyo alionekana akiwa na mudhaifu, chini ya vitisho, akiwa amechoka na kuonekana kuogopa mtu aliyekuwa pembeni yake, akilazimika kukariri kwa vitu.
Katika tangazo, gazeti la Iwacu halikupenda kutoa maelezo zaidi na kupongeza polisi kwa “ushirikiano wake mzuri”.
Msemaji wa polisi ya Burundi (PNB), Désiré Nduwimana ametuhakikishia kuwa “polisi inafahamu tatizo hilo, vyombo vya usalama vinafanya kazi yao. Tutawambia maendeleo”.
Kwa mjibu wa mtalaam katia sayansi ya mawasiliano, kuona mwenzetu ameamuru kutuma video kuliko kurudi nyumbani ni jambo linaloleta wasi wasi.
“Ni ajabu. Katika hali kama hiyo, jambo la kwanza, mwandishi Jérémie Misago angetakiwa kurudi nyumbani kuliko kuchukua vidéo” amebaini mtalaam huyo.
You might also like
Lubero : a new deadly attack by the alleged ADF leaves ten dead
A group of men armed with machetes and rifles raided around midnight on the night of Saturday to Sunday in the village of Nguli, west of Muramba in the Bukenye
DRC : M23 announces a ceasefire
It is in a statement that the rebel group declared a ceasefire on Tuesday. Local actors and the international community had insisted on this ceasefire to allow above all the
Rwanda-DRC : maafisa wakuu wa Jeshi la Rwanda wanaohudumu katika mashirika ya kikanda wameitishwa
Rwanda imeitisha jumanne hii maafisa wakuu wa jeshi wanaohudumu katika mashirika ya kikanda ambao wako kwenye ardhi ya Kongo. Ni kufuatua hatua ya Kinshasa ya kuwafurusha wale maafisa ambao wanahudumu
