Gitega: wapinzani wawili wazuiliwa jela kwa zaidi ya mwezi

Gitega: wapinzani wawili wazuiliwa jela kwa zaidi ya mwezi

Wafuasi wawili wa chama cha CNL wa tarafa ya Bugendana mkoa wa Gitega (kati kati ya Burundi) wanazuiliwa jela kwa zaidi ya mwezi mmoja. Wanatuhumiwa kumubaka na kumuuwa mwanamke mmoja. Watuhumiwa wanakanusha madai hayo. Chama chao kinaomba waachiliwe huru. HABARI SOS Médias Burundi

Jonas Nsabimana na Jacques Habonimana, wawili hao wote wafuasi wa chama cha CNL walikamatwa tarehe 12 oktoba iliyopita nyumbani kwao. Walikamatwa na polisi.

Kisa hicho kilitokea katika kijiji cha Nyakeru tarafa ya Bugendana mkoa wa Gitega. Hayo ni baada ya kupatikana kwa muili wa Domine Ngendakumana mwenye umri wa miaka 37 mama wa watoto wawili.
Habari hiyo inathibitishwa na Epimac Mugisha kiongozi wa chama cha CNL tarafani Bugendana ambaye anazidi kuwa muathiriwa huyo aliuwawa baada ya kubakwa. Anatuhumu lakini kijana Imbonerakure ambaye alichangia kinywaji na muhanga huyo katika siku ya kuuwawa kwake.

Domine Ngendakumana na mfuasi huyo wa tawi la vijana wafuasi wa CNDD-FDD walitoka katika mgahawa huo wakiwa pamoja na kuelekea eneo moja, alisema.

Bwana Mugisha anahakikisha kuwa wafuasi hao wawili wa chama cha CNL hawana hatia.

” Walikamatwa kwa ushawishi wa mkuu wa kijiji cha Nyakeru kutokana na kuwa ni wafuasi wa CNL” anazidi kusema.
Anaomba waachiliwe huru.

Mkuu wa kijiji cha Nyakeru Juvenal Butoyi anakanusha madai hayo dhidi yake na kuongeza kuwa wapinzani hao walisimamishwa kwa ajili ya uchunguzi unaoendelea.

Wafuasi hao wawili wa chama kikuu cha upinzani wanazuiliwa kwa sasa ndani ya gereza kuu la Gitega (jiji kuu la kisiasa)

Previous Ituri and North Kivu: at least 18 civilians killed since Sunday
Next Burundi: makamu wa rais anathibitisha uwepo wa uhusiano mbaya kati ya viongozi wa nchi na wandishi wa habari

You might also like

Human Rights

Crisis in eastern Congo : a blue helmet killed and another seriously injured in an attack against a Monusco plane

The Monusco (Mission of the United Nations organization in the DRC) announced the death of its blue helmet in a press release. It informs that he died following an attack

Politic

Rwanda-Burundi: Burundi yatangaza kufungua upya mipaka yake na Rwanda

Ni waziri wa Burundi wa ushirikiano wa kimataifa aliyetangaza hatua siku ya jumanne. Albert Shingiro hata hivyo alikariri nia ya serikali ya Burundi ya kuona Kigali inawafurusha wanamapinduzi inayowahudumia tangu

Politic

Goma: a journalist detained by intelligence

Jimmy Shukrani Bakomera, correspondent for the VOA (Voice of America) Kirundi-Kinyarwanda is detained by Congolese intelligence since Thursday. INFO SOS Médias Burundi Our colleague was arrested this Thursday midday at