Gitega: wapinzani wawili wazuiliwa jela kwa zaidi ya mwezi
Wafuasi wawili wa chama cha CNL wa tarafa ya Bugendana mkoa wa Gitega (kati kati ya Burundi) wanazuiliwa jela kwa zaidi ya mwezi mmoja. Wanatuhumiwa kumubaka na kumuuwa mwanamke mmoja. Watuhumiwa wanakanusha madai hayo. Chama chao kinaomba waachiliwe huru. HABARI SOS Médias Burundi
Jonas Nsabimana na Jacques Habonimana, wawili hao wote wafuasi wa chama cha CNL walikamatwa tarehe 12 oktoba iliyopita nyumbani kwao. Walikamatwa na polisi.
Kisa hicho kilitokea katika kijiji cha Nyakeru tarafa ya Bugendana mkoa wa Gitega. Hayo ni baada ya kupatikana kwa muili wa Domine Ngendakumana mwenye umri wa miaka 37 mama wa watoto wawili.
Habari hiyo inathibitishwa na Epimac Mugisha kiongozi wa chama cha CNL tarafani Bugendana ambaye anazidi kuwa muathiriwa huyo aliuwawa baada ya kubakwa. Anatuhumu lakini kijana Imbonerakure ambaye alichangia kinywaji na muhanga huyo katika siku ya kuuwawa kwake.
Domine Ngendakumana na mfuasi huyo wa tawi la vijana wafuasi wa CNDD-FDD walitoka katika mgahawa huo wakiwa pamoja na kuelekea eneo moja, alisema.
Bwana Mugisha anahakikisha kuwa wafuasi hao wawili wa chama cha CNL hawana hatia.
” Walikamatwa kwa ushawishi wa mkuu wa kijiji cha Nyakeru kutokana na kuwa ni wafuasi wa CNL” anazidi kusema.
Anaomba waachiliwe huru.
Mkuu wa kijiji cha Nyakeru Juvenal Butoyi anakanusha madai hayo dhidi yake na kuongeza kuwa wapinzani hao walisimamishwa kwa ajili ya uchunguzi unaoendelea.
Wafuasi hao wawili wa chama kikuu cha upinzani wanazuiliwa kwa sasa ndani ya gereza kuu la Gitega (jiji kuu la kisiasa)
You might also like
Crisis in eastern Congo : a blue helmet killed and another seriously injured in an attack against a Monusco plane
The Monusco (Mission of the United Nations organization in the DRC) announced the death of its blue helmet in a press release. It informs that he died following an attack
Rwanda-Burundi: Burundi yatangaza kufungua upya mipaka yake na Rwanda
Ni waziri wa Burundi wa ushirikiano wa kimataifa aliyetangaza hatua siku ya jumanne. Albert Shingiro hata hivyo alikariri nia ya serikali ya Burundi ya kuona Kigali inawafurusha wanamapinduzi inayowahudumia tangu
Goma: a journalist detained by intelligence
Jimmy Shukrani Bakomera, correspondent for the VOA (Voice of America) Kirundi-Kinyarwanda is detained by Congolese intelligence since Thursday. INFO SOS Médias Burundi Our colleague was arrested this Thursday midday at
