Rumonge: mkuu wa tarafa ya Rumonge amukuta mwenzake wa tarafa ya Buyengero gerezani
Jérémie Bizimana mkuu wa tarafa ya Rumonge mkoa wa Rumonge (Kusini-magharibi mwa Burundi) sasa ni yuko katika gereza la Murembwe tangu ijumaa. Alimkuta jela mwenzake wa tarafa ya Buyengero pamoja na mshahuri wa gavana anayehusika na fedha na utawala. Wanazuiliwa kwa kosa moja: ubadilifu na wizi wa mabati na mifuko ya simenti vilivyotolewa na ofisi ya rais kwa ajili ya ujenzi wa shule. HABARI SOS Médias Burundi
Jérémie Bizimana alihojiwa na mwendeshamashtaka mkuu wa mahakama ya rufaa mkoa wa Bururi( kusini mwa Burundi) siku ya ijumaa.
Baada ya mahojiano, mwendeshamashtaka aliamuru apelekwe kwenye gereza kuu la Murembwe kwenye kijiji cha Gatete tarafa na mkoa wa Rumonge kusini magharibi mwa Burundi.
Bwana Bizimana amekuwa mkuu wa tarafa wa pili mkoani Rumonge kupelekwa jela katika kipindi cha siku mbili.
Gratien Nduwayo mkuu wa tarafa ya Buyengero alitumwa gerezani siku ya jumatano majira ya saa kumi na moja akiambatana na baba yake mkwe ambaye ni mshahuri wa gavana anayehusika na fedha na utawala.
Wanatuhumiwa kosa la ubadilifu na wizi wa mabati na mifuko ya simenti iliyotolewa na ofisi ya rais wa jamuhuri ya Burundi kwa ujenzi wa shule.
Kwa mjibu wa vyanzo, viongozi wengine wengi wangetakiwa kuhojiwa katika kesi hiyo.
You might also like
Bujumbura : Rubirizi zone chief dismissed for insubordination and mismanagement
SOS Médias Burundi Bujumbura, June 2, 2025 — Jean Marie Nahishakiye, Rubirizi zone chief in Mutimbuzi district, Bujumbura province (west), was dismisses from his duties on Tuesday, May 27. Bujumbura
Kira Hospital case : Burundi faces serious consequences
The major shareholder of Burundi’s most prestigious clinic, Kira Hospital, wrote to the Burundian Minister of Justice to denounce the deliberate blocking of the dispossession file of the majority private
DRC : the EAC urges clarifications on the deportation of Rwandan officers
In a letter sent on February 1, 2023 to Christophe Apala, the Congolese Deputy Prime Minister at the same time Minister of Foreign Affairs, the Secretary General of the East
