Rumonge: mkuu wa tarafa ya Rumonge amukuta mwenzake wa tarafa ya Buyengero gerezani
Jérémie Bizimana mkuu wa tarafa ya Rumonge mkoa wa Rumonge (Kusini-magharibi mwa Burundi) sasa ni yuko katika gereza la Murembwe tangu ijumaa. Alimkuta jela mwenzake wa tarafa ya Buyengero pamoja na mshahuri wa gavana anayehusika na fedha na utawala. Wanazuiliwa kwa kosa moja: ubadilifu na wizi wa mabati na mifuko ya simenti vilivyotolewa na ofisi ya rais kwa ajili ya ujenzi wa shule. HABARI SOS Médias Burundi
Jérémie Bizimana alihojiwa na mwendeshamashtaka mkuu wa mahakama ya rufaa mkoa wa Bururi( kusini mwa Burundi) siku ya ijumaa.
Baada ya mahojiano, mwendeshamashtaka aliamuru apelekwe kwenye gereza kuu la Murembwe kwenye kijiji cha Gatete tarafa na mkoa wa Rumonge kusini magharibi mwa Burundi.
Bwana Bizimana amekuwa mkuu wa tarafa wa pili mkoani Rumonge kupelekwa jela katika kipindi cha siku mbili.
Gratien Nduwayo mkuu wa tarafa ya Buyengero alitumwa gerezani siku ya jumatano majira ya saa kumi na moja akiambatana na baba yake mkwe ambaye ni mshahuri wa gavana anayehusika na fedha na utawala.
Wanatuhumiwa kosa la ubadilifu na wizi wa mabati na mifuko ya simenti iliyotolewa na ofisi ya rais wa jamuhuri ya Burundi kwa ujenzi wa shule.
Kwa mjibu wa vyanzo, viongozi wengine wengi wangetakiwa kuhojiwa katika kesi hiyo.
You might also like
Burundi : the fuel shortage paralyzes transportation throughout Bujumbura
SOS Médias Burundi Bujumbura, April 28, 2026 — Since Monday, April 27, 2026, a severe disruption to public transportation has been observed throughout Bujumbura, the commercial capital of Burundi. The
Cibitoke: low attendance despite the reopening of the Burundi-Rwanda border
More than two months after the reopening of border posts in the districts of Rugombo, Mabayi and Bukinanyana of the province of Cibitoke (northwest Burundi), there is a low influx
Burundi : a woman takes on the role of ombudsman for the first time
This is Aimee Laurentine Kanyana. This former justice minister was approved this Thursday by the two chambers of the Burundian parliament. INFO SOS Médias Burundi Aimée Laurentine Kanyana was in
