Rumonge: mkuu wa tarafa ya Rumonge amukuta mwenzake wa tarafa ya Buyengero gerezani
Jérémie Bizimana mkuu wa tarafa ya Rumonge mkoa wa Rumonge (Kusini-magharibi mwa Burundi) sasa ni yuko katika gereza la Murembwe tangu ijumaa. Alimkuta jela mwenzake wa tarafa ya Buyengero pamoja na mshahuri wa gavana anayehusika na fedha na utawala. Wanazuiliwa kwa kosa moja: ubadilifu na wizi wa mabati na mifuko ya simenti vilivyotolewa na ofisi ya rais kwa ajili ya ujenzi wa shule. HABARI SOS Médias Burundi
Jérémie Bizimana alihojiwa na mwendeshamashtaka mkuu wa mahakama ya rufaa mkoa wa Bururi( kusini mwa Burundi) siku ya ijumaa.
Baada ya mahojiano, mwendeshamashtaka aliamuru apelekwe kwenye gereza kuu la Murembwe kwenye kijiji cha Gatete tarafa na mkoa wa Rumonge kusini magharibi mwa Burundi.
Bwana Bizimana amekuwa mkuu wa tarafa wa pili mkoani Rumonge kupelekwa jela katika kipindi cha siku mbili.
Gratien Nduwayo mkuu wa tarafa ya Buyengero alitumwa gerezani siku ya jumatano majira ya saa kumi na moja akiambatana na baba yake mkwe ambaye ni mshahuri wa gavana anayehusika na fedha na utawala.
Wanatuhumiwa kosa la ubadilifu na wizi wa mabati na mifuko ya simenti iliyotolewa na ofisi ya rais wa jamuhuri ya Burundi kwa ujenzi wa shule.
Kwa mjibu wa vyanzo, viongozi wengine wengi wangetakiwa kuhojiwa katika kesi hiyo.
You might also like
Minembwe: the Burundian army threatens to attack the Twirwaneho armed group
Soldiers of the FDNB (Burundi National Defense Force) posted in South Kivu in the east of the DRC are increasing attacks against local and foreign armed groups. This Wednesday, they
Bujumbura : the secretary general of the CNDD-FDD is gradually recovering
Reverien Ndikuriyo is receiving treatment in a hospital in Dubai, the first city of the United Arab Emirates and capital of the emirate of Dubai. He was transferred there after
Nyanza-Lac: katika mkuu wa chama cha CNDD-FDD anatishia kuwauwa baadhi ya wafuasi
Ijumaa iliyopita, Reverien Ndikuriyo katibu mkuu wa chama cha CNDD-FDD alikuwa ziarani katika tarafa ya Nyanza-Lac mkoa wa Makamba (kusini mwa Burundi). Alitishia kuwauwa wafuasi wa chama wanaosota kidole kasoro
