Nyarugusu (Tanzania): mkimbizi mwenye asili ya Burundi alipatikana akiwa maiti
Mkimbizi kutoka Burundi mwenye umri wa miaka takriban miaka 40 aliuwawa na watu wasiojulikana karibu ya kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu nchini Tanzania. Polisi inasema ni tukio la wizi lililokwenda vibaya. Watu wengi walisimamishwa kwa ajili ya uchunguzi. HABARI SOS Médias Burundi
Antoine Nsengiyumva mkaazi wa village 7 zone 11 katika kambi ya Nyarugusu nchini Tanzania. Muili wake uligunduliwa katika shamba la nyanya karibu na kambi hiyo.
Huenda akawa mjumbe wa genge la majambazi kulingana na polisi.
” Huenda alikuwa katika genge la majambazi watatu. Walienda kuiba katika shamba la nyanya nje ya kambi. Wamiliki wa shamba hilo pamoja na walinzi huenda waliwakamata wezi hao. Washirika wake walifanikiwa kukimbia na yeye akakamatwa na kupigwa hadi kufa. Alipata pia majeraha kwa kupigwa mapanga”, polisi ilifahamisha hayo na kuwaomba kuacha wizi na wakimbizi kuacha kujichukulia sheria mikononi katika kambi ya Nyarugusu na maeneo ya karibu.
” Pembeni ya maiti hiyo, kuliogotwa kitunga kinachojaa nyanya na vituguu ambavyo vilivunwa ndani ya shamba hilo na hivyo kuonekana kuwa taarifa za kuwa ni tukio la wizi lililokwenda vibaya zinaweza kuwa za ukweli”, polisi inazidi kufahamisha.
Polisi iliwaitisha wamiliki wote na walinzi wa mashamba ya karibu na eneo hilo ambako maiti hiyo ilipatikana. Uchunguzi tayari umeanzishwa.
Muhanga aliacha mjane na watoto watatu katika kambi ya Nyarugusu ambayo inawapa hifadhi zaidi ya wakimbizi elfu 50 kutoka Burundi.
You might also like
Nduta (Tanzania) : a camp turning into a savannah?
The Nduta camp in Tanzania, which hosts more than 58,000 Burundian refugees, seems to be gradually transforming into a savannah or a natural reserve. This situation, a direct consequence of
Gatumba attack : Burundian authorities announce they have contacted INTERPOL to find the perpetrators
The Burundian minister in charge of internal affairs announced Tuesday that Burundian authorities have contacted INTERPOL so that the perpetrators of the Gatumba massacres be repatriated and tried in the
Kivu-kaskazini : mandamano dhidi ya ziara ya rais Macron nchini DRC yanafahamisha bila ushawishi mkubwa
Mandamano hayo yaliandaliwa alhamisi hii mjini Goma tangu asubuhi. Makundi ya ushawishi pamoja vuguvugu la wananchi yanapinga ujio wa rais wa ufaransa Emmanuel Macron nchini Jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo.
