Nyarugusu (Tanzania): mkimbizi mwenye asili ya Burundi alipatikana akiwa maiti
Mkimbizi kutoka Burundi mwenye umri wa miaka takriban miaka 40 aliuwawa na watu wasiojulikana karibu ya kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu nchini Tanzania. Polisi inasema ni tukio la wizi lililokwenda vibaya. Watu wengi walisimamishwa kwa ajili ya uchunguzi. HABARI SOS Médias Burundi
Antoine Nsengiyumva mkaazi wa village 7 zone 11 katika kambi ya Nyarugusu nchini Tanzania. Muili wake uligunduliwa katika shamba la nyanya karibu na kambi hiyo.
Huenda akawa mjumbe wa genge la majambazi kulingana na polisi.
” Huenda alikuwa katika genge la majambazi watatu. Walienda kuiba katika shamba la nyanya nje ya kambi. Wamiliki wa shamba hilo pamoja na walinzi huenda waliwakamata wezi hao. Washirika wake walifanikiwa kukimbia na yeye akakamatwa na kupigwa hadi kufa. Alipata pia majeraha kwa kupigwa mapanga”, polisi ilifahamisha hayo na kuwaomba kuacha wizi na wakimbizi kuacha kujichukulia sheria mikononi katika kambi ya Nyarugusu na maeneo ya karibu.
” Pembeni ya maiti hiyo, kuliogotwa kitunga kinachojaa nyanya na vituguu ambavyo vilivunwa ndani ya shamba hilo na hivyo kuonekana kuwa taarifa za kuwa ni tukio la wizi lililokwenda vibaya zinaweza kuwa za ukweli”, polisi inazidi kufahamisha.
Polisi iliwaitisha wamiliki wote na walinzi wa mashamba ya karibu na eneo hilo ambako maiti hiyo ilipatikana. Uchunguzi tayari umeanzishwa.
Muhanga aliacha mjane na watoto watatu katika kambi ya Nyarugusu ambayo inawapa hifadhi zaidi ya wakimbizi elfu 50 kutoka Burundi.
You might also like
Kakuma (Kenya) : Zaidi ya watu 200 wanaotafuta hifadhi ya ukimbizi wakubaliwa
Zaidi ya watu 200 walipokelewa katika vituo viwili vya muda ndani ya kambi ya wakimbizi ya Kakuma kaskazini magharibi mwa Kenya mnamo siku zilizopita. Hayo ni wakati ambapo zaidi ya
Malawi : three refugee women, including a Burundian woman, accuse a police officer of sexual harassment and rape
SOS Médias Burundi Dzaleka, April 30, 2025 – Three refugee women, including a Burundian woman, have filed a complaint of sexual harassment and rape against a police officer assigned to
Goma: mwandishi wa habari Jimmy Shukrani Bakomera aachiliwa huru
Mwenzetu huyo amechikiwa huru ijumaa hii asubuhi. Alikuwa katika gereza la ANR ( idara ya ujasusi ya Kongo) katika mji wa Goma (makao makuu ya mkoa wa Kivu kaskazini) tangu
