Ngozi: uhaba wa chakula kwenye gereza kuu
wafungwa katika gereza kuu la Ngozi (kaskazini mwa Burundi) wanasema kuwa wanateseka kutokana na ukosefu wa chakula. Walioathirika zaidi ni wale wanaotoka katika mikoa ya Kirundo na Kayanza (kanda hiyo hiyo). Wanadai kuwa hawapati wageni kama wenzao wenye asili ya mkoa wa Ngozi kutokana na masafa marefu ambayo wajumbe wa familia zao wanatakiwa kufanya ili kufika kwenye gereza hilo. Wagonjwa hawawezi kumeza dawa wakati ambapo hakuna kitu tumboni. Wanaomba misaada. HABARI SOS Médias Burundi
Gereza hilo linawahifadhi wafungwa kutoka mikoa ya Ngozi, Kayanza, na Kirundo. Wafungwa katika gereza hilo wanaishi katika mazingira magumu kutoka na uhaba wa chakula.
” Wiki mbili zimemalizika pasina kupewa maharagwe. Ili kuweza kula ugali wao mdogo, baadhi hununua mboga boga lakini kwa wale ambao hawana uwezo, hutumia maji ya moto yaliyowekewa chumvi. Inakasirikisha “, anahakikisha mfungwa mmoja mwenye asili ya mkoa wa Kayanza.
“Tumezoea kula mara moja kwa siku nyakati za mchana peke”, alifamisha mfungwa mmoja.
Habari kutoka katika gereza hilo zinafamisha kuwa wafungwa wenye asili ya mikoa ya Kirundo na Kayanza wanaathiriwa zaidi na hali hiyo sababu wanakuwa mbali na familia zao zinazolazimika kusafiri masafa marefu ili kuweza kuwatembelea.
” Angalau hao wenye asili ya mkoa wa Ngozi wanapata urahisi kidogo kwa sababu wajumbe wa familia zao wanaweza kuwatembelea angalau mara tatu kwa wiki. Lakini sisi njaa inatumenya. Tunaweza kupata mgeni mara moja kwa mwezi”,alilalamika mfungwa mwengine.
Maradhi ya utapia mlo yanaanza kusambaa.
Wafungwa wenye maradhi yasiopona ambao wanalazimika kula kabla ya kutumia dawa wanaathiriwa zaidi na hali hiyo.
” wafungwa wenye HIV wanalazimika kutumia dawa pasina kula. Baadhi wanaanza kupata maradhi ambayo walikuwa hawana kama kuumwa tumbo, alitoa ushuhuda huo mfungwa wa zamani.
Gereza la Ngozi linawapa hifadhi wafungwa zaidi ya 1500 wakati uwezo wake ni kuwapokea watu 400 peke.
You might also like
Rumonge : the governor suspends activities of the EUSEBU church in his province
The governor of Rumonge province (southwestern Burundi) has suspended all activities of the EUSEBU church (Church for the Unity of the Holy Spirit in Burundi) in his province since April
Bunyoni affair: the commander of the riot unit replaced
It was the minister for internal affairs and security who decided that Police colonel Désiré Uwamahoro, commander for the controversial riot squad (BAE), be replaced by another colonel. Jonathan Sindayihebura
Burundi : an aberrant end of year
Townspeople of the commercial city of Bujumbura, where United Nations agencies and the central administration are concentrated, were not interested in celebrating as usual at the end of each year.
